< Izajasza 22 >
1 Brzemię doliny widzenia. Cóż ci się stało, żeś wszystka na dachy wystąpiła?
Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
2 Miasto pełne wrzasku, i zgiełku, miasto weselące się! Pobici twoi nie są pobici mieczem, ani zginęli w bitwie.
Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
3 Wszyscy książęta twoi naporząd się rozpierzchnęli, od strzelców powiązani są wespół, i ci, którzy z daleka uciekają.
Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
4 Dlategom rzekł: Odstąpcie odemnie, abym gorzko płakał; nie kwapcie się, cieszyć mię w spustoszeniu córki ludu mojego.
Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
5 Albowiem to jest dzień ucisku i podeptania, i zamięszania od Pana, Pana zastępów, w dolinie widzenia, dzień burzenia murów, i wołania na góry.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
6 Elam też wziął sajdak z wozami ludu wojennego, a Kir okazał tarczę swoję.
Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
7 I stało się, że wyborne doliny twoje napełnione były wozami, a jezdni się potężnie zaszańcowali u bramy.
Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
8 I odkryta była zasłona Judowa; a poglądałeś dnia onego na zbrojownię w domu lasu.
ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
9 I poglądaliście na rozwaliny miasta Dawidowego, bo ich wiele było; i zgromadziły się wody sadzawki dolnej.
mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
10 Także policzyliście domy w Jeruzalemie, a rozwaliliście domy na oprawę murów.
Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
11 Uczyniliście też przekop między dwoma murami, dla wód stawu starego, a nie oglądaliście się na tego, co go sprawił, a tego, który go zdawna zbudował, nie widzieliście.
Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
12 Nadto, gdy wołał Pan, Pan zastępów, dnia onego do płaczu i do narzekania, i do obłysienia się, i do przepasania się worem;
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
13 A oto radość i wesele wasze, zabijać woły, i bić owce, a jedząc mięso, i pijąc wino, mówić: Jedzmy, pijmy, bo jutro pomrzemy.
Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
14 Aleć to doszło uszów moich, mówi Pan zastępów. Przetoż wam ta nieprawość nie będzie odpuszczona; aż pomrzecie, mówi Pan, Pan zastępów.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
15 Tak mówi Pan, Pan zastępów: Idź, wnijdź do tego podskarbiego, do Sobny, który jest przełożonym w domu, i rzecz:
Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
16 Co ty tu masz? albo kogo tu masz, żeś tu sobie wykował grób? Wykowałeś sobie na wysokiem miejscu grób swój, a wystawiłeś na skale przybytek swój?
Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
17 Oto Pan, który cię przykrył jako zacnego męża, a który cię kosztownie przyodział,
“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
18 Prędko cię zatoczy jako kulę do ziemi szerokiej i przestronnej; tam umrzesz, tam i wozy sławy twojej zginą, o hańbo domu Pana swego!
Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
19 A tak wypędzę cię z stanowiska twego, a z urzędu twego złożę cię.
Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
20 A dnia onego przyzwię sługę swego Elijakima, syna Helkijaszowego;
“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
21 I oblekę go w szatę twoję, i pasem twoim potwierdzę go, panowanie też twoje dam w rękę jego; i będzie za ojca obywatelom Jeruzalemskim, i domowi Judzkiemu.
Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 I położę klucz domu Dawidowego na ramieniu jego; gdy otworzy, nikt nie zawrze, a gdy zawrze, nikt nie otworzy.
Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
23 I wbiję go jako gwóźdź na miejscu pewnem, a będzie stolicą chwały domu ojca swego.
Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
24 A zawiśnie na nim wszystka sława domu ojca jego, synowie i córki, i wszystko naczynie by najmniejsze, od naczynia, z którego piją, aż do każdego naczynia winnego.
Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
25 Dnia onego, mówi Pan zastępów, będzie wyjęty gwóźdź, który był wbity na miejscu pewnem, a będzie przycięty i upadnie; odcięte będzie i brzemię, które jest na nim; bo Pan mówił.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.