< Ozeasza 10 >
1 Izrael jest macicą próżną, owoc przynosi sobie; czem więcej miewał owocu swego, tem więcej nabudował ołtarzów; a czem obfitsza jest ziemia jego, tem więcej nastawiał obrazów.
Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
2 Rozdziela się serce ich, przetoż winnymi są; on pokruszy ołtarze ich, i obrazy ich popsuje.
Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 Ponieważ mówią: Nie mamy króla, nawet nie boimy się Pana, a król nam co uczyni?
Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
4 Mówią słowa, przysięgając kłamliwie, gdy czynią przymierze; i wzrośnie sąd jako jad na zagonach polnych.
Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
5 Dla jałowic Bet Aweńskich zatrwożą się obywatele Samaryjscy, gdy kwilić będą nad nim, lud jego, i popije go, (którzy się więc radowali z niego) przeto, że sława jego odchodzi od niego.
Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
6 Nawet i sam do Assyryi zaprowadzony będzie za dar królowi Jareb; zawstydzi się Efraim, i zasroma się Izrael za radę swoję.
Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 Wycięty będzie król Samaryjski, jako piana na wierzchu wody.
Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
8 I będą wyżyny Awenu wytracone, grzech Izraelski; ciernie i oset wyrośnie na ołtarzach ich; a rzekną górom: Przykryjcie nas; a pagórkom: Upadnijcie na nas.
Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
9 Ode dni Gabaa grzeszyłeś, Izraelu! tam się ostali, nie zachwyciła ich w Gabaa bitwa przeciwko synom nieprawości podniesiona.
“Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
10 Przetoż ich pokarzę według upodobania mego; bo się zbiorą na nich narody, aby byli karani dla dwojakich nieprawości swoich.
Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 Bo Efraim jest jako jałowica wyuczona, kocha się w młóceniu, chociażem Ja następował na cudny kark jej, abym do jazdy używał Efraima, Juda aby orał, a Jakób aby włóczył.
Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
12 I mówiłem: Siejcie sobie ku sprawiedliwości; żnijcie ku miłosierdziu, orzcie sobie nowinę; bo czas jest szukać Pana, aż przyjdzie, i spuści na was sprawiedliwość jako deszcz.
Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 Aleście orali niepobożność, żęliście nieprawość, jedliście owoc kłamstwa; albowiem ufasz w drodze swej i w mnóstwie mocarzów twoich.
Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
14 Dlategoż powstanie rozruch między ludem twoim, a wszystkie zamki twoje poburzone będą, tak jako poburzył Salman Bet Arbel w dzień bitwy; matki z synami roztrącone będą.
mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 Oto tak wam uczyni Betel dla wielkiej złości waszej; król Izraelski na świtaniu do szczętu zgładzony będzie.
Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.