< Aggeusza 1 >
1 Roku wtórego Daryjusza króla, miesiąca szóstego, dnia pierwszego tegoż miesiąca, stało się słowo Pańskie przez Aggieusza proroka do Zorobabela, syna Salatyjelowego, książęcia Judzkiego, i do Jesuego, syna Jozedekowego, kapłana najwyższego, mówiąc:
Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
2 Tak powiada Pan zastępów, mówiąc: Ten lud mówi: Jeszcze nie przyszedł czas, czas budowania domu Pańskiego.
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
3 Przetoż się stało słowo Pańskie przez Aggieusza proroka, mówiąc:
Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
4 Izali wam jest czas, abyście mieszkali w domach waszych listwowanych, a dom ten aby pusty stał?
“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
5 Teraz tedy tak mówi Pan zastępów: Uważajcież, jako się wam powodzi;
Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
6 Siejecie wiele, a mało zbieracie; jecie, ale się nie nasycacie; pijecie, ale nie ugaszacie pragnienia; obłóczycie się, ale się nikt nie może zagrzać, a ten, co sobie zapłatę zgromadza, zgromadza ją do worka dziurawego.
Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
7 Tak mówi Pan zastępów: Uważajcie, jako się wam powodzi;
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
8 Wstąpcie na tę górę, i zwoźcie drzewo; budujcie ten dom, a zakocham się w nim, i będę uwielbiony, mówiPan.
Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
9 Poglądacie na wiele, a oto, mało dostawacie, a co wnosicie do domu, to Ja rozdmuchywam; dlaczego? mówi Pan zastępów; dlatego, że dom mój jest pusty, a międzytem się każdy z was stara o dom swój.
“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
10 Przetoż się nad wami niebo zawarło, aby rosy nie dawało; ziemia także zawarła się, aby nie wydawała urodzaju swego.
Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
11 A tak przyzwałem suszę na tę ziemię, i na te góry, i na pszenicę, i na moszcz, i na oliwę, i na to, coby miała wydać ziemia, i na ludzi i na bydło, i na wszystkę pracę ręczną.
Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
12 Tedy usłuchał Zorobabel, syn Salatyjelowy, i Jesua, syn Jozedekowy, kapłan najwyższy, i wszystkie ostatki ludu, głosu Pana, Boga swego, i słów Aggieusza proroka, ponieważ go posłał Pan, Bóg ich; bo się lud bał oblicza Pańskiego.
Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
13 Tedy Aggieusz, poseł Pański, rzekł do ludu, będąc w poselstwie Pańskiem, mówiąc: Jam z wami, mówi Pan.
Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
14 Wtem wzbudził Pan ducha Zorobabela, syna Salatyjelowego, książęcia Judzkiego, i ducha Jesuego, syna Jozedekowego, kapłana najwyższego, i ducha ostatków wszystkiego ludu, że przyszedłszy robili około domu Pana zastępów, Boga swego.
Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
15 Dnia dwudziestego i czwartego, miesiąca szóstego, roku wtórego Daryjusza króla;
katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.