< Galacjan 2 >
1 Potem po czternastu latach wstąpiłem zasię do Jeruzalemu z Barnabaszem, wziąwszy z sobą i Tytusa.
Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
2 A wstąpiłem według objawienia i przełożyłem im Ewangieliję, którą każę między poganami, a zwłaszcza zacniejszym, bym snać nadaremno nie bieżał, albo przedtem nie biegał.
Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
3 Ale ani Tytus, który ze mną był, będąc Grekiem, nie był przymuszony obrzezać się,
Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
4 A to dla wprowadzonych fałszywych braci, którzy się wkradli, aby wyszpiegowali wolność naszę, którą mamy w Chrystusie Jezusie, aby nas w niewolę podbili.
ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
5 Którymeśmy i na chwilkę nie ustąpili, i nie poddali się, aby u was prawda Ewangielii została.
Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
6 A od tych, którzy się zdadzą być czemś, (acz jakimi niekiedy byli, nic mi na tem; bo osoby człowieczej Bóg nie przyjmuje), ci mówię, którzy się zdali być czemś, nic mi nie przydali.
Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi—kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje—watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
7 Owszem, przeciwnym obyczajem, widząc, iż mi jest zwierzona Ewangielija między nieobrzezanymi, jako Piotrowi między obrzezanymi,
Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
8 (Albowiem ten, który był skuteczny przez Piotra w apostolstwie między obrzezanymi, skuteczny był i we mnie między poganami.)
Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
9 I poznawszy łaskę mnie daną, Jakób i Kiefas, i Jan, którzy się zdadzą być filarami, podali prawicę mnie i Barnabaszowi na towarzystwo, abyśmy my między poganami, a oni między obrzezanymi kazali.
Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
10 Tylko upomnieli, abyśmy na ubogich pamiętali, o com się też pilnie starał, abym to uczynił.
Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
11 A gdy przyszedł Piotr do Antyjochii, sprzeciwiłem się mu w twarz; i był godzien nagany.
Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
12 Albowiem przedtem, niż przyszli niektórzy od Jakóba, wespół z poganami jadał; a gdy ci przyszli, schraniał się i odłączał, bojąc się tych, którzy byli z obrzezania.
Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
13 A wespół z nim obłudnie się obchodzili i drudzy Żydzi, tak że i Barnabasz uwiedziony był tą ich obłudą.
Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
14 Ale gdym obaczył, iż nie prosto chodzą w prawdzie Ewangielii, rzekłem Piotrowi przed wszystkimi: Ponieważ ty, będąc Żydem, po pogańsku żyjesz a nie po żydowsku, czemuż pogan przymuszasz po żydowsku żyć?
Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: “Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?”
15 My, którzyśmy z przyrodzenia Żydowie a nie z pogan grzesznicy,
Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
16 Wiedząc, iż nie bywa usprawiedliwiony człowiek z uczynków zakonu, ale przez wiarę w Jezusa Chrystusa, i myśmy w Jezusa Chrystusa uwierzyli, abyśmy byli usprawiedliwieni z wiary Chrystusowej, a nie z uczynków zakonu, przeto że nie będzie usprawiedliwione z uczynków zakonu żadne ciało.
Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
17 A jeźli my szukając, abyśmy byli usprawiedliwieni w Chrystusie, znajdujemy się też grzesznikami, tedyć Chrystus jest sługą grzechu? Nie daj tego Boże!
Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
18 Albowiem jeźli to, com zburzył, znowu zasię buduję, przestępcą samego siebie czynię.
Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
19 Bom ja przez zakon zakonowi umarł, abym żył Bogu.
Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
20 Z Chrystusem jestem ukrzyżowany, a żyję już nie ja, lecz żyje we mnie Chrystus; a to że teraz w ciele żyję, w wierze Syna Bożego żyję, który mię umiłował i wydał samego siebie za mię.
na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
21 Nie odrzucam tej łaski Bożej; bo jeźli przez zakon jest sprawiedliwość, tedyć Chrystus próżno umarł.
Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!