< Galacjan 2 >
1 Potem po czternastu latach wstąpiłem zasię do Jeruzalemu z Barnabaszem, wziąwszy z sobą i Tytusa.
Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
2 A wstąpiłem według objawienia i przełożyłem im Ewangieliję, którą każę między poganami, a zwłaszcza zacniejszym, bym snać nadaremno nie bieżał, albo przedtem nie biegał.
Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
3 Ale ani Tytus, który ze mną był, będąc Grekiem, nie był przymuszony obrzezać się,
Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
4 A to dla wprowadzonych fałszywych braci, którzy się wkradli, aby wyszpiegowali wolność naszę, którą mamy w Chrystusie Jezusie, aby nas w niewolę podbili.
Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
5 Którymeśmy i na chwilkę nie ustąpili, i nie poddali się, aby u was prawda Ewangielii została.
hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
6 A od tych, którzy się zdadzą być czemś, (acz jakimi niekiedy byli, nic mi na tem; bo osoby człowieczej Bóg nie przyjmuje), ci mówię, którzy się zdali być czemś, nic mi nie przydali.
Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote.
7 Owszem, przeciwnym obyczajem, widząc, iż mi jest zwierzona Ewangielija między nieobrzezanymi, jako Piotrowi między obrzezanymi,
Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi.
8 (Albowiem ten, który był skuteczny przez Piotra w apostolstwie między obrzezanymi, skuteczny był i we mnie między poganami.)
Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa.
9 I poznawszy łaskę mnie daną, Jakób i Kiefas, i Jan, którzy się zdadzą być filarami, podali prawicę mnie i Barnabaszowi na towarzystwo, abyśmy my między poganami, a oni między obrzezanymi kazali.
Basi, Yakobo, Kefa na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi.
10 Tylko upomnieli, abyśmy na ubogich pamiętali, o com się też pilnie starał, abym to uczynił.
Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.
11 A gdy przyszedł Piotr do Antyjochii, sprzeciwiłem się mu w twarz; i był godzien nagany.
Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpinga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosea kwa wazi.
12 Albowiem przedtem, niż przyszli niektórzy od Jakóba, wespół z poganami jadał; a gdy ci przyszli, schraniał się i odłączał, bojąc się tych, którzy byli z obrzezania.
Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu wa Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
13 A wespół z nim obłudnie się obchodzili i drudzy Żydzi, tak że i Barnabasz uwiedziony był tą ich obłudą.
Pia Wayahudi wengine waliungana naye katika unafiki huu, hata Barnaba naye akapotoshwa na unafiki wao.
14 Ale gdym obaczył, iż nie prosto chodzą w prawdzie Ewangielii, rzekłem Piotrowi przed wszystkimi: Ponieważ ty, będąc Żydem, po pogańsku żyjesz a nie po żydowsku, czemuż pogan przymuszasz po żydowsku żyć?
Nilipoona kwamba hawatendi sawasawa na kweli ya Injili, nilimwambia Petro mbele ya wote, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu wa Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?
15 My, którzyśmy z przyrodzenia Żydowie a nie z pogan grzesznicy,
“Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,
16 Wiedząc, iż nie bywa usprawiedliwiony człowiek z uczynków zakonu, ale przez wiarę w Jezusa Chrystusa, i myśmy w Jezusa Chrystusa uwierzyli, abyśmy byli usprawiedliwieni z wiary Chrystusowej, a nie z uczynków zakonu, przeto że nie będzie usprawiedliwione z uczynków zakonu żadne ciało.
bado tunajua ya kwamba mtu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hivyo sisi pia, tumemwamini Kristo Yesu ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Kristo, wala si kwa matendo ya sheria, kwa sababu kwa kushika sheria hakuna hata mtu mmoja atakayehesabiwa haki.
17 A jeźli my szukając, abyśmy byli usprawiedliwieni w Chrystusie, znajdujemy się też grzesznikami, tedyć Chrystus jest sługą grzechu? Nie daj tego Boże!
“Lakini tukitafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, inakuwa dhahiri kwamba sisi ni wenye dhambi. Je, ina maana kwamba Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!
18 Albowiem jeźli to, com zburzył, znowu zasię buduję, przestępcą samego siebie czynię.
Lakini ikiwa mimi ninajenga tena kile ambacho nimekwisha kukibomoa, basi ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji.
19 Bom ja przez zakon zakonowi umarł, abym żył Bogu.
Kwa maana mimi kwa njia ya sheria, nimeifia sheria ili nipate kuishi kwa ajili ya Mungu.
20 Z Chrystusem jestem ukrzyżowany, a żyję już nie ja, lecz żyje we mnie Chrystus; a to że teraz w ciele żyję, w wierze Syna Bożego żyję, który mię umiłował i wydał samego siebie za mię.
Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu.
21 Nie odrzucam tej łaski Bożej; bo jeźli przez zakon jest sprawiedliwość, tedyć Chrystus próżno umarł.
Siibatilishi neema ya Mungu, kwa maana kama haki ingeweza kupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure!”