< Ezechiela 13 >

1 I stało się słowo Pańskie do mnie, mówiąc:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Synu człowieczy! prorokuj przeciw prorokom Izraelskim, którzy prorokują, a rzecz prorokującym z serca swego: Słuchajcie słowa Pańskiego.
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
3 Tak mówi panujący Pan: Biada prorokom głupim, którzy idą za duchem swoim, choć nic nie widzieli!
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
4 Izraelu! Prorocy twoi są jako liszki na puszczy.
Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
5 Nie wstępujcie na przerwane miejsca, ani grodzcie płotu około domu Izraelskiego, żeby się mógł ostać w bitwie w dzień Pański.
Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
6 Widzą marność i wieszczbę kłamliwą; powiadają: Pan mówi, choć ich Pan nie posłał; i cieszą lud, aby tylko utwierdzili słowo swe.
Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
7 Izali widzenia marnego nie widzicie, a wieszczby kłamliwej nie opowiadacie? I mówicie: Pan mówił, chociażem Ja nie mówił.
Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
8 Przetoż tak mówi panujący Pan: Ponieważ mówicie marność, a widzicie kłamstwo, przetoż oto Ja jestem przeciwko wam, mówi panujący Pan.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
9 Bo ręka moja będzie przeciwko prorokom, którzy widzą marność, a opowiadają kłamstwo; w zgromadzeniu ludu mego nie będą, a w poczet domu Izraelskiego nie będą wpisani, i do ziemi Izraelskiej nie wnijdą; a dowiecie się, żem Ja panujący Pan.
Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
10 Przeto, przeto mówię, że w błąd wprowadzili lud mój, mówiąc: Pokój, choć nie było pokoju; jeden zaiste zbudował ścianę glinianą, drudzy ją tynkowali wapnem nieczynionem.
“‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
11 Mówże do tych, którzy ją tynkują wapnem nieczynionem: Upadnie to, przyjdzie deszcz gwałtowny, a wy, kamienie gradowe! spadniecie, i wiatr wichrowaty rozwali ją.
kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
12 A oto gdy upadnie ona ściana, izali wam nie rzeką: Gdzież jest ono tynkowanie, któremeście tynkowali?
Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
13 Prztoż tak mówi panujący Pan! Rozwalę ją, mówię, wiatrem wichrowatym w zapalczywości mojej, i deszcz gwałtowny w popędliwości mojej przyjdzie, a kamienie gradowe w rozgniewaniu mojem na zniszczenie jej.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
14 Bo obalę tę ścianę, którąście potynkowali wapnem nieczynionem, a zrównam ją z ziemią, tak, że odkryty będzie grunt jej, i upadnie, i skażeni będziecie w pośrodku jej, i dowiecie się, żem Ja Pan.
Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
15 A gdy wykonam popędliwość moję nad tą ścianą, i nad tymi, którzy ją tynkowali wapnem nieczynionem, rzekę do was: Niemasz już onej ściany, niemasz i tych, którzy ją tynkowali,
Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
16 To jest, proroków Izraelskich, którzy prorokują o Jeruzalemie, i ogłaszają mu widzenie pokoju, choć niemasz pokoju, mówi panujący Pan.
wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
17 Ale ty, synu człowieczy! obróć twarz twoję przeciwko córkom ludu swego, które prorokują z serca swego, a prorokuj przeciwko nim,
“Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
18 I rzecz: Tak mówi panujący Pan: Biada tym, które szyją wezgłówka pod wszelkie łokcie rąk ludu mojego, a czynią duchny na głowy wszelkiego wzrostu, aby łowiły dusze! izali łowić macie dusze ludu mego, abyście się żywić mogły?
na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
19 Bo mię podawacie w lekkość u ludu mego dla garści jęczmienia, i dla kęsa chleba, zabijając dusze, które nie umrą, a ożywiając dusze, które żywe nie będą, kłamiąc ludowi memu, którzy słuchają kłamstwa.
Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
20 Dlatego, tak mówi panujący Pan: Oto Ja będę przeciwko wezgłówkom waszym, któremi wy tam dusze łowicie, abyście je zwiodły; bo je stargnę z ramion waszych, a wypuszczę dusze, które wy łowicie, abyście je zwiodły;
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
21 I rozerwę duchny wasze, a wybawię lud mój z ręki waszej, abyście ich więcej nie mogły łowić ręką swoją; a dowiecie się, żem Ja Pan.
Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
22 Przeto, że zasmucacie serce sprawiedliwego kłamstwy, chociażem go Ja nie zasmucił, a zmacniacie ręce niezbożnego, aby się nie odwrócił od złej drogi swojej, ożywiając go;
Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
23 Przetoż nie będziecie więcej widywać marności, ani wieszczby więcej prorokować będziecie; bo wyrwę lud mój z ręki waszej, a dowiecie się, żem Ja Pan.
kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”

< Ezechiela 13 >