< Wyjścia 37 >
1 Uczynił też Besaleel skrzynię z drzewa sytym, a była półtrzecia łokcia długość jej, a półtora łokcia szerokość jej, także półtora łokcia wysokość jej.
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 I powlókł ją złotem szczerem wewnątrz, i zewnątrz, i uczynił jej koronę złotą w około.
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 Ulał też do niej cztery kolce złote do czterech węgłów jej: dwa kolce po jednej stronie jej, a dwa kolce po drugiej stronie jej.
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 Uczynił i drążki z drzewa sytym, a powlókł je złotem.
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 I przewlekł drążki przez kolce po stronach skrzyni, aby na nich noszona była skrzynia.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 Uczynił też ubłagalnią ze złota szczerego: półtrzecia łokcia długość jej, a półtora łokcia szerokość jej.
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 Urobił i dwa Cheruby złote, z ciągnionego złota urobił je na obu końcach ubłagalni.
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 Cheruba jednego na jednym końcu, a Cheruba drugiego na drugim końcu; na ubłagalni uczynił Cheruby na obu końcach jej.
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 Którzy Cherubowie mieli rozciągnione skrzydła, z wierzchu zakrywając skrzydłami swemi ubłagalnią, a twarzy ich były jednemu ku drugiemu; ku ubłagalni były twarzy Cherubów.
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 Przytem sprawił stół z drzewa sytym, dwa łokcie długość jego, i łokieć szerokość jego, a półtora łokcia wysokość jego.
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 I powlókł go złotem szczerem, i uczynił mu koronę złotą w około.
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 Uczynił mu też listwę na dłoń w szerz w około; uczynił też i koronę złotą w około onej listwy.
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 I ulał do niego cztery kolce złote, które kolce przyprawił na czterech rogach, u czterech nóg jego.
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 Na przeciwko onej listwie były kolce, w które zawłaczano drążki do noszenia stołu.
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 Porobił i drążki z drzewa sytym, i powlókł je złotem do noszenia stołu.
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 Poczynił też naczynia do stołu należące, misy jego i przystawki jego, i kubki jego, i czasze do nalewania ofiar mokrych, z szczerego złota.
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 Urobił też świecznik ze złota szczerego, z ciągnionego złota uczynił świecznik ten, słupiec jego, i pręty jego, czaszki jego, gałki jego, i kwiaty jego z tegoż były.
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 A sześć prętów wychodziło po stronach jego: trzy pręty z jednej strony świecznika, a trzy pręty z drugiej strony świecznika.
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 Trzy czaszki na kształt orzecha migdałowego na pręcie jednym, także gałka i kwiat; i trzy czaszki na kształt orzecha migdałowego na pręcie drugim, także gałka i kwiat; tak było na wszystkich sześciu prętach wychodzących z świecznika.
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 Ale na świeczniku były cztery czaszki na kształt orzecha migdałowego, gałki jego i kwiaty jego.
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 I była gałka pod dwiema prętami jego, także gałka pod drugiemi dwiema prętami jego, i zaś gałka pod innemi dwiema prętami jego; tak było pod sześcią prętów wychodzących z niego.
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 Gałki ich i pręty ich z niego były; to wszystko ze złota całokowane było, ze złota szczerego.
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 Uczynił też siedem lamp do niego, i nożyczki do nich i kaganki jego ze złota szczerego.
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 Z talentu złota szczerego uczynił go, i wszystko naczynie jego.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 Uczynił też ołtarz do kadzenia z drzewa sytym, na łokieć wzdłuż, i na łokieć wszerz, czworograniasty, a na dwa łokcie wzwyż, a z niego wychodziły rogi jego.
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 I powlókł go złotem szczerem, wierzch jego, i ściany jego w około, i rogi jego; uczynił mu też koronę złotą w około.
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 Po dwu także kolcach złotych uczynił u niego, pod koroną jego, we dwu kątach jego, po obu stronach jego przez które przewłaczano drążki, aby był noszony na nich.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 Uczynił też drążki z drzewa sytym i powlókł je złotem.
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 Uczynił też olejek pomazywania świętego, i kadzenie wonne, robotą aptekarską.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.