< Wyjścia 1 >

1 Teć są imiona synów Izraelskich, którzy weszli do Egiptu z Jakóbem; każdy z domem swym weszli:
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
2 Ruben, Symeon, Lewi, i Judas.
Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
3 Isaszar, Zabulon, i Benjamin.
Isakari, Zabuloni na Benyamini;
4 Dan, i Neftali, Gad, i Aser.
Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
5 A było wszystkich dusz, które wyszły z biódr Jakóbowych, siedmdziesiąt dusz; a Józef był przedtem w Egipcie.
Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
6 I umarł Józef, i wszyscy bracia jego, i wszystek on rodzaj.
Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
7 A synowie Izraelscy rozrodzili się, i rozpłodzili się, i rozmnożyli się, i zmocnili się bardzo wielce, a napełniona jest ziemia nimi.
lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
8 Między tem powstał król nowy nad Egiptem, który nie znał Józefa;
Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
9 I rzekł do ludu swego: Oto lud synów Izraelskich wielki, i możniejszy nad nas.
Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
10 Przetoż mądrze sobie pocznijmy z nimi, by się snać nie rozmnożył, a jeźliby przypadła wojna, aby się nie przyłączył i on do nieprzyjaciół naszych, i nie walczył przeciwko nam, i nie uszedł z ziemi.
Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
11 A tak ustawili nad nimi poborcę, aby go dręczyli ciężarami swemi; i zbudował lud Izraelski miasta składu Faraonowi: Pytom i Rameses.
Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
12 Ale im więcej go trapili, tem więcej się rozmnażał, i tem więcej rósł, tak, iż ściśnieni byli dla synów Izraelskich.
Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
13 I podbili Egipczanie syny Izraelskie w niewolą ciężką.
kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
14 I przykrzyli im żywot ich robotą ciężką około gliny, i około cegieł, i około każdej roboty na polu, mimo wszelaką robotę swą, do której ich używali bez litości.
Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
15 I rozkazał król Egipski babom Hebrejskim, z których imię jednej Zefora, a imię drugiej Fua;
Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
16 A rzekł: Gdy będziecie babić niewiastom Hebrejskim, a ujrzycie że rodzą, byłliby syn, zabijcież go, a jeźli córka, niech żywa zostanie.
“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
17 Ale baby one bały się Boga, i nie czyniły, jako im rozkazał król Egipski, ale żywo zachowywały chłopiątka.
Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
18 Zaczem wezwawszy król Egipski onych bab, mówił do nich: Czemuście to uczyniły, żeście żywo zachowały chłopiątka?
Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
19 I odpowiedziały baby Faraonowi: Iż nie są jako niewiasty Egipskie, niewiasty Hebrejskie; bo są duże, pierwej niż przyjdzie do nich baba, rodzą.
Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
20 I czynił dobrze Bóg onym babom; i krzewił się lud, i zmocnili się bardzo.
Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
21 I stało się, przeto że się bały one baby Boga, pobudował im domy.
Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
22 Tedy rozkazał Farao wszystkiemu ludowi swemu, mówiąc: Każdego syna, który się urodzi, w rzekę go wrzućcie, a każdą córkę żywo zachowajcie.
Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”

< Wyjścia 1 >