< Kaznodziei 10 >

1 Jako muchy zdechłe zasmradzają i psują olejek aptekarski: tak człowieka z mądrości i z sławy zacnago trochę głupstwa oszpeca.
Kama nzi walio kufa husababisha manukato kutoa harufu ya uozo, hivyo hivyo upumbavu kidogo hushinda hekima na heshima.
2 Serce mądrego jest po prawej stronie jego; ale serce głupiego po lewej stronie jego.
Moyo wa mtu mwenye hekima huelekea kulia, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
3 I na ten czas, gdy głupi drogą idzie, serce jego niedostatek cierpi; bo pokazuje wszystkim, że głupim jest.
Wakati mpumbavu anapotembea barabarani, fikira zake zina upungufu, ikithibitisha kwa kila mtu kwamba ni mpumbavu.
4 Jeźliby duch panującego powstał przeciwko tobie, nie opuszczaj miejsca twego; albowiem pokora wstręt czyni grzechom wielkim.
Kama jaziba za mtawala zikiinuka kinyume na wewe, usiache kazi yako. Utulivu unaweza kutuliza ukatili mkubwa.
5 Jest złe, którem widział pod słońcem, to jest, błąd, który pochodzi od zwierzchności:
Kuna uovu niliouona chini ya jua, aina ya kosa ambalo huja kutoka kwa mtawala:
6 Że głupi wywyższani bywają w godności wielkiej, a bogaci w mądrość nisko siadają;
Wapumbavu wanapewa nafasi za uongozi, wakati watu walio faulu wanapewa nafasi za chini.
7 Widziałem sługi na koniach, a książąt chodzących piechotą jako sługi.
Nimewaona watumwa wakipanda farasi, na watu walio faulu wakitembea kama watumwa juu ya ardhi.
8 kto kopie dół, sam weń wpada; a kto rozrzuca płot, wąż go ukąsi.
Yeyote anayechimba shimo anaweza kutumbukia yake, na popote mtu anayevunja ukuja, nyoka anaweza kumuuma.
9 Kto przenosi kamienie, urazi się niemi; a kto łupie drwa, niebezpieczen jest od nich.
Yeyote achongaye mwawe, anaweza kuumizwa nayo. Na mtu achongaye mbao, anaweza kujihatarisha kwa hiyo.
10 Jeźliże się stępi żelazo, a nie naostrzyłby ostrza jego, tedy mocy przyłożyć musi; ale to daleko lepiej mądrość sprawić może.
Kama chuma bapa kisicho na makali, na mtu hainoi, kisha ni lazima atumie nguvu nyingi, lakini hekima hutoa faida kwa ufaulu.
11 Jeźli ukąsi wąż przed zaklęciem, nic nie pomogą słowa zaklinacza.
Kama nyoka akiuma kabla hajafurahi, hivyo hakuna faida kwa mfurahishaji.
12 Słowa ust mądrego są wdzięczne; ale wargi głupiego pożerają go.
Maneno ya kinywa cha mtu mwenye hekima yana huruma. Lakini midomo ya mpumbavu humumeza mwenyewe.
13 Początek słów ust jego głupstwo, a koniec powieści jego wielkie błazeństwo.
Kama maneno yanavyo anza kutiririka mdomoni mwa mpumbavu, ujinga hutoka, na mwisho mdomo wake hutiririka wazimu mbaya.
14 Bo głupi wiele mówi, choć nie wie ten człowiek, co ma być. Albowiem któż mu oznajmi, co po nim nastanie?
Mpumbavu huongeza maneno, lakini hakuna ajuaye kinachokuja. Ni nani ajuaye baada yake?
15 Głupi pracują aż do ustania, a przecie nie mogą dojść do miasta.
Jasho la wapumbavu huwavaa wao, hivyo hawajui hata barabara ya kwenda mjini.
16 Biada tobie, ziemio! której król jest dziecięciem, i której książęta rano biesiadują.
Ole wako ardhi kama mfalme wako ni kijana mdogo, na kama viongozi wako huanza karamu ahsubuhi!
17 Błogosławionaś ty, ziemio! której król jest synem zacnych, a której książęta czasu słusznego jadają dla posilenia, a nie dla opilstwa.
Lakini umebarikiwa ardhi kama mfalme wako ni mwana wa waungwana, na kama vingozi wako hula wakati muafaka, kwa nguvu, na sio kwa ulevi.
18 Dla lenistwa się dach pochyla, a dla osłabiałych rąk przecieka dom.
Kwa sababu ya uvivu paa huanguka. Na kwa sababu isiyo fanya kazi nyumba hupata ufa.
19 Dla uweselenia gotują uczty, i wino rozwesela żywot; ale pieniądze do wszystkiego dopomagają.
Watu huandaa chakula kwa kicheko, divai huleta furaha maishani, na fedha hutimiza hitaji kwa kila kitu.
20 Ani w myśli twojej królowi nie złorzecz, ani w skrytym pokoju twoim nie przeklinaj bogatego; albowiem i ptak niebieski doniósłby ten głos; a to, co ma skrzydła, objawiłoby powieść twoję.
Usimlaani mfalme, hata katika akili, na usiwalaani wenye mali katika chumba chako cha kulala. Kwa kuwa ndege wa angani inaweza kuchukua maneno yako. Chochote kilicho na mabawa kinaweza kusambaza jambo.

< Kaznodziei 10 >