< Kolosan 1 >
1 Paweł, Apostoł Jezusa Chrystusa przez wolę Bożą, i Tymoteusz brat,
Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:
2 Tym, którzy są w Kolosiech, świętym i wiernym braciom w Chrystusie Jezusie. Łaska wam i pokój niech będzie od Boga, Ojca naszego, i od Pana Jezusa Chrystusa.
Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai: Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.
3 Dziękujemy Bogu i Ojcu Pana naszego Jezusa Chrystusa, zawsze modląc się za was,
Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi,
4 Usłyszawszy o wierze waszej w Chrystusie Jezusie i miłości przeciwko wszystkim świętym,
kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote:
5 Dla nadziei onej wam odłożonej w niebiesiech, o którejście przedtem słyszeli przez słowo prawdy, to jest Ewangielii,
imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili
6 Która przyszła do was jako i na wszystek świat, i przynosi owoc, jako i u was, od onego dnia, któregoście usłyszeli i poznali łaskę Bożą w prawdzie.
iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote.
7 Jakoście się też nauczyli od Epafry, miłego spółsługi naszego, który jest wiernym sługą Chrystusowym dla was;
Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu,
8 Który też oznajmił nam miłość waszę w duchu.
ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.
9 Dlatego i my od onego dnia, któregośmy to usłyszeli, nie przestajemy się za was modlić i prosić, abyście byli napełnieni znajomością woli jego we wszelkiej mądrości i w wyrozumieniu duchownem.
Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu.
10 Abyście chodzili przystojnie przed Panem ku wszelkiemu jego upodobaniu, w każdym uczynku dobrym owoc przynosząc i rosnąc w znajomości Bożej,
Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu,
11 Wszelką mocą umocnieni będąc według chwalebnej mocy jego, ku wszelkiej cierpliwości i nieskwapliwości z radością,
mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha
12 Dziękując Ojcu, który nas godnymi uczynił, abyśmy byli uczestnikami dziedzictwa świętych w światłości;
mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
13 Który nas wyrwał z mocy ciemności i przeniósł do królestwa Syna swego miłego,
Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
14 W którym mamy odkupienie przez krew jego, to jest odpuszczenie grzechów;
ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
15 Który jest obrazem Boga niewidzialnego i pierworodny wszystkich rzeczy stworzonych.
Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Albowiem przezeń stworzone są wszystkie rzeczy, które są na niebie i na ziemi, widzialne i niewidzialne, bądź trony, bądź państwa, bądź księstwa, bądź zwierzchności, wszystko przezeń i dla niego stworzone jest.
Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
17 A on jest przed wszystkimi i wszystko w nim stoi.
Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
18 On też jest głową ciała, to jest kościoła, który jest początkiem i pierworodnym z umarłych, aby on między wszystkimi przodkował;
Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote.
19 Ponieważ się upodobało Ojcu, aby w nim wszystka zupełność mieszkała.
Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake,
20 I żeby przezeń z sobą pojednał wszystko, uczyniwszy pokój przez krew krzyża jego; przezeń, mówię, tak to, co jest na ziemi, jako i to, co jest na niebiesiech.
na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.
21 I was, którzyście niekiedy byli oddaleni i nieprzyjaciele umysłem w złośliwych uczynkach, teraz też pojednał.
Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya.
22 Ciałem własnem swojem przez śmierć, aby was wystawił świętemi i niepokalanemi, i bez nagany przed obliczem swojem;
Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama,
23 Jeźli tylko trwacie w wierze ugruntowani i utwierdzeni, a nie poruszeni od nadziei Ewangielii, którąście słyszeli, która jest kazana wszelkiemu stworzeniu, które jest pod niebem, której ja Paweł stałem się sługą;
ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.
24 Który się teraz raduję w doległościach moich dla was i dopełniam ostatków ucisków Chrystusowych na ciele mojem za ciało jego, które jest kościół.
Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
25 Któregom się ja stał sługą według daru Bożego, który mi jest dany dla was, abym wypełnił słowo Boże,
Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu:
26 To jest, tajemnicę onę, która była zakryta od wieków i od rodzajów, ale teraz objawiona jest świętym jego. (aiōn )
Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn )
27 Którym chciał Bóg oznajmić, jakie jest bogactwo tej tajemnicy chwalebnej między poganami, która jest Chrystus między wami, nadzieja ona chwały;
Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.
28 Którego my opowiadamy, napominając każdego człowieka i ucząc każdego człowieka we wszelkiej mądrości, abyśmy wystawili każdego człowieka doskonałym w Chrystusie Jezusie;
Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo.
29 W czem też pracuję, bojując według skutecznej mocy jego, która we mnie dzieło swoje potężnie sprawuje.
Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.