< Dzieje 13 >

1 A byli w Antyjochii we zborze, który tam był, niektórzy prorocy i nauczyciele, jako Barnabasz i Symeon, którego zwano Niger, i Lucyjus Cyrenejczyk, i Manahen, który był wychowany z Herodem Tetrarchą, i Saul.
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2 A gdy oni służbę Pańską jawnie odprawiali i pościli, rzekł im Duch Święty: Odłączcie mi Barnabasza i Saula do tej sprawy, do którejm ich powołał.
Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
3 Tedy poszcząc i modląc się, i wkładając na nie ręce, odprawili je.
Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4 Oni tedy wysłani będąc od Ducha Świętego, przyszli do Seleucyi, a stamtąd płynęli do Cypru.
Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5 A gdy byli w Salaminie, opowiadali słowo Boże w bóżnicach żydowskich, a mieli z sobą i Jana do usługi.
Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6 A przeszedłszy onę wyspę aż do Pafu, znaleźli tam jakiegoś czarnoksiężnika, fałszywego proroka, Żyda, któremu imię było Barjezus.
Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7 Który był przy zacnym staroście, Sergijuszu Pawle, mężu roztropnym. Ten przyzwawszy Barnabasza i Saula, pragnął słuchać słowa Bożego.
Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8 Lecz się im sprzeciwił Elimas, on czarnoksiężnik, (albowiem się tak wykłada imię jego), starając się, jakoby starostę od wiary odwrócił:
Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9 Tedy Saul, (którego zowią i Pawłem) napełniony będąc Ducha Świętego, a pilnie na niego patrząc,
Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10 Rzekł: O pełny wszelkiej zdrady i wszelkiej przewrotności, synu dyjabelski, nieprzyjacielu wszelkiej sprawiedliwości! nie przestanieszże podwracać prostych dróg Pańskich?
akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11 A oto teraz ręka Pańska nad tobą: i będziesz ślepym, nie widząc słońca aż do czasu. A zarazem przypadła na niego chmura i ciemność, a błąkając się szukał, kto by go wiódł za rękę.
Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12 Tedy widząc starosta, co się stało, uwierzył, zdumiewając się nad nauką Pańską.
Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13 A puściwszy się z Pafu Paweł i ci, którzy z nim byli, przyszli do Pergi Pamfiliejskiej. A Jan odszedłszy od nich, wrócił się do Jeruzalemu.
Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14 A oni odszedłszy z Pergi, przyszli do Antyjochii Pisydejskiej, a wszedłszy do bóżnicy w dzień sobotni, usiedli.
Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15 A po przeczytaniu zakonu i proroków, posłali do nich przełożeni bóżnicy, mówiąc: Mężowie bracia! macieli wolę jakie napominanie uczynić do ludu, mówcie.
Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
16 Tedy powstawszy Paweł, a ręką skinąwszy rzekł: Mężowie Izraelscy i którzy się boicie Boga! słuchajcie:
Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17 Bóg ludu tego Izraelskiego wybrał ojców naszych i wywyższył lud, gdy byli przychodniami w ziemi egipskiej, i w ramieniu wyciągnionem wywiódł je z niej.
Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18 I przez czas czterdziestu lat znosił obyczaje ich na puszczy.
Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19 A wygładziwszy siedm narodów w ziemi Chananejskiej, losem rozdzielił między nie onę ziemię ich.
Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20 A potem około czterysta i pięćdziesiąt lat dawał im sędziów, aż do Samuela proroka.
Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 A od onego czasu prosili o króla. I dał im Bóg Saula, syna Cysowego, męża z pokolenia Benjaminowego, przez lat czterdzieści.
Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22 A gdy go odrzucił, wzbudził im Dawida za króla, któremu też świadectwo wydawając powiedział: Znalazłem Dawida, syna Jessego, męża według serca mego, który będzie czynił wszystkę wolę moję.
Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23 Z jegoż nasienia Bóg według obietnicy wzbudził Izraelowi zbawiciela Jezusa.
Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24 Przed którego przyjściem kazał Jan chrzest pokuty wszystkiemu ludowi Izraelskiemu.
Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25 A gdy Jan dokonał biegu swego, rzekł: Kim mię być mniemacie? Nie jestem ja, ale oto idzie za mną, u którego nóg obuwia nie jestem godzien rozwiązać.
Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26 Mężowie bracia, synowie narodu Abrahamowego i którzy się między wami Boga boją! wamci słowo zbawienia tego posłane jest.
“Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 Albowiem ci, co mieszkają w Jeruzalemie i przełożeni ich, nie znając tego Jezusa i głosów prorockich, które przez każdy sabat bywają czytane, wypełnili je, osądziwszy go.
Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28 A żadnej przyczyny śmierci w nim nie znalazłszy, prosili Piłata, aby był zabity.
Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29 A gdy wykonali wszystko, co o nim było napisane, zdjąwszy go z drzewa, włożyli go do grobu.
Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30 Ale go Bóg wzbudził od umarłych.
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 Który widziany jest przez wiele dni od tych, którzy z nim pospołu przyszli z Galilei do Jeruzalemu, którzy są świadkami jego przed ludem.
Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32 I my wam opowiadamy tę obietnicę, która się ojcom stała, iż ją Bóg wypełnił nam, dziatkom ich, wzbudziwszy Jezusa.
Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33 Jako też w Psalmie wtórym napisane jest: Syn mój jesteś ty, jam ciebie dziś spłodził.
Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34 A iż go wzbudził od umarłych, aby się więcej nie wrócił do skażenia, tak powiedział: Dam wam święte dobrodziejstwa Dawidowe wierne.
Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35 Przeto i indziej powiada: Nie dasz Świętemu twemu widzieć skażenia.
Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36 Albowiemci Dawid za wieku swego usłużywszy woli Bożej, zasnął i przyłączony jest do ojców swoich, a widział skażenie.
Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37 Lecz ten, którego Bóg wzbudził, nie widział skażenia.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38 Niechże wam tedy będzie wiadomo, mężowie bracia, iż się wam przez tego opowiada odpuszczenie grzechów:
Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39 I od wszystkiego od czegoście nie mogli być przez zakon Mojżeszowy usprawiedliwieni, przez tego każdy wierzący usprawiedliwiony bywa.
na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40 A przetoż patrzcie, aby na was nie przyszło to, co powiedziano w prorokach:
Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41 Obaczcie wy wzgardziciele i dziwujcie się, a wniwecz się obróćcie; bo ja sprawuję sprawę za dni waszych, sprawę, której nie wierzycie, choćby wam kto o niej powiadał.
Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
42 A gdy oni wychodzili z bóżnicy żydowskiej, prosili ich poganie, aby i w drugi sabat mówili do nich też słowa.
Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43 A po rozpuszczeniu zgromadzenia, poszło wiele Żydów i nabożnych nowowierników za Pawłem i Barnabaszem, którzy mówiąc do nich, radzili im, aby trwali w łasce Bożej.
Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44 A w drugi sabat niemal wszystko miasto się zgromadziło na słuchanie słowa Bożego.
Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 Tedy Żydowie widząc lud, napełnieni są zazdrością i sprzeciwiali się temu, co Paweł powiadał, mówiąc przeciwko temu i bluźniąc.
Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46 A Paweł i Barnabasz, bezpiecznie mówiąc, rzekli: Wamci najpierwej miało być opowiadane słowo Boże; ale ponieważ je odrzucacie, a sądzicie się być niegodnymi żywota wiecznego, oto się obracamy do pogan. (aiōnios g166)
Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
47 Albowiem nam tak rozkazał Pan, mówiąc: Położyłem cię światłością poganom, abyś był zbawieniem aż do krajów ziemi.
Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
48 A słysząc to poganie, radowali się i wielbili słowo Pańskie, i uwierzyli, ilekolwiek ich było sporządzonych do żywota wiecznego. (aiōnios g166)
Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
49 I roznosiło się słowo Pańskie po wszystkiej onej krainie.
Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50 A Żydowie poduszczali niewiasty nabożne i uczciwe, i przedniejsze w mieście; a wzbudzili prześladowanie przeciwko Pawłowi i przeciwko Barnabaszowi, i wygnali je z granic swoich.
Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51 A oni otrząsnąwszy proch z nóg swoich na nie, przyszli do Ikonii.
Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52 A uczniowie byli napełnieni radości i Ducha Świętego.
Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.

< Dzieje 13 >