< II Tesaloniczan 2 >
1 A prosimy was, bracia! przez przyjście Pana naszego Jezusa Chrystusa i nasze zgromadzenie do niego,
Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
2 Abyście się nie zaraz dali zrażać z zmysłu waszego, ani sobą trwożyć, lub przez ducha lub przez mowę, lub przez list, jakoby od nas pisany, jakoby nadchodził dzień Chrystusowy.
msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
3 Niech was nikt nie zwodzi żadnym sposobem; albowiem nie przyjdzie on dzień, ażby pierwej przyszło odstąpienie i byłby objawiony człowiek on grzechu, on syn zatracenia.
Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
4 Który się sprzeciwia i wynosi nad to wszystko, co się zowie Bogiem, albo co ma Boską cześć, tak iż on w kościele Bożym jako Bóg usiądzie, udawając się za Boga.
Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
5 Izali nie pamiętacie, iż jeszcze z wami będąc, o temem wam powiadał?
Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
6 A teraz wiecie, co przeszkadza, aby był objawiony czasu swego.
Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
7 Albowiem się już sprawuje tajemnica nieprawości, tylko że ten, który teraz przeszkadza, przeszkadzać będzie, ażby był z pośrodku odjęty.
Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
8 A tedy objawiony będzie on niezbożnik, którego Pan zabije duchem ust swoich i zniesie objawieniem przyjścia swego.
Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
9 Którego niezbożnika przyjście jest podług skutku szatańskiego, ze wszelką mocą i znakami, i cudami kłamliwemi,
Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
10 I ze wszystkiem oszukaniem nieprawości w tych, którzy giną, przeto iż miłości prawdy nie przyjęli, aby byli zbawieni.
na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
11 A przetoż pośle im Bóg skutek błędów, aby wierzyli kłamstwu,
Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
12 Aby byli osądzeni wszyscy, którzy nie uwierzyli prawdzie, ale sobie upodobali niesprawiedliwość.
Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
13 Lecz my powinniśmy Bogu dziękować zawsze za was, bracia umiłowani od Pana! iż was Bóg od początku wybrał ku zbawieniu w poświęceniu Ducha i w wierze prawdy,
Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
14 Do czego was powołał przez Ewangieliję naszę ku dostąpieniu chwały Pana naszego, Jezusa Chrystusa.
Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15 Przetoż, bracia! stójcie, a trzymajcie się nauki podanej, którejście się nauczyli lub przez mowę, lub przez list nasz.
Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
16 A sam Pan nasz, Jezus Chrystus i Bóg a Ojciec nasz, który nas umiłował i dał pociechę wieczną, i nadzieję dobrą przez łaskę, (aiōnios )
Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios )
17 Niech cieszy serca wasze i utwierdza was w każdej mowie i w uczynku dobrym.
aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.