< II Samuela 21 >

1 I był głód za dni Dawidowych przez trzy lata, jednego roku po drugim. Tedy szukał Dawid oblicza Pańskiego, któremu rzekł Pan: Dla Saula, i dla domu jego krwawego, przeto iż pomordował Gabaonity.
Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2 Przyzwał tedy król Gabaonitów, i rzekł do nich: (A ci Gabaonitowie nie byli z synów Izraelskich, ale z ostatków Amorejczyków, którym acz byli synowie Izraelscy przysięgli, wszakże je usiłował Saul wyplenić z gorliwości swej dla synów Izraelskich i Judzkich.)
Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
3 I rzekł Dawid do Gabaonitów: Cóż wam mam uczynić? a czem was ubłagać, abyście błogosławili dziedzictwu Pańskiemu?
Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
4 I odpowiedzieli mu Gabaonitowie: Nie idzie nam o srebro ani o złoto z Saulem, i z domem jego, ani o to, żebyśmy zabili kogo w Izraelu. A on rzekł: Cokolwiek rzeczecie, uczynię wam.
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
5 Którzy rzekli do króla: Męża, który nas wygubił, i na tem był, aby nas do szczętu wytracił, żeby nas nic nie zostało we wszystkich granicach Izraelskich.
Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
6 Wydajcie nam siedmiu mężów z synów jego, a powiesimy je Panu w Gabaa Saula, niekiedy wybranego Pańskiego. Tedy rzekł: Wydam.
tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 Lecz sfolgował król Mefibosetowi, synowi Jonatana, syna Saulowego, dla przysięgi Pańskiej, która była między nimi, między Dawidem i między Jonatanem, synem Saulowym.
Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
8 Ale wziął król dwóch synów Resfy, córki Ai, które porodziła Saulowi, Armoniego i Mefiboseta, i pięciu synów Micholi, córki Saulowej, które porodziła Adryjelowi, synowi Barsyla Meholatyckiego,
Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
9 I wydał je w ręce Gabaonitów, i powiesili je na górze przed Panem. I umarli oni siedmiu pospołu, a pobici są w pierwsze dni żniwa, na początku żniwa jęczmiennego.
Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
10 A wziąwszy Resfa, córka Ai, wór, ropostarła go na skale, na początku żniwa, ażby na nie kropił deszcz z nieba, i nie dopuszczała ptastwu powietrznemu, padać na nie we dnie, ani zwierzowi polnemu w nocy.
Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
11 Tedy oznajmiono Dawidowi, co uczyniła Resfa, córka Ai, założnica Saulowa.
Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
12 Przetoż szedłszy Dawid wziął kości Saulowe, i kości Jonatana, syna jego od starszych Jabez Galaadskiego, którzy je byli ukradli z ulicy Betsańskiej, kędy je byli zawiesili Filistynowie onegoż dnia, gdy porazili Filistynowie Saula w Gielboe.
alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
13 A tak wziął stamtąd kości Saulowe i kości Jonatana, syna jego; zebrano też kości powieszonych,
Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 I pogrzebli kości Saulowe i Jonatana, syna jego, w ziemi Benjamina w Sela, grobie Cysa, ojca jego, a uczynili wszystko, co był rozkazał król; a tak potem ubłagany był Bóg ziemi.
Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 I była zasię wojna między Filistynami i Izraelem; i ciągnął Dawid i słudzy jego z nim, a walczył przeciwko Filistynom, tak, że ustał Dawid.
Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
16 Tedy Jesbibenob, który był z synów jednego olbrzyma, (a grot drzewca jego ważył trzy sta syklów miedzi, a miał przepasany miecz nowy) umyślił był zabić Dawida.
Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
17 Ale go ratował Abisaj, syn Sarwii, a raniwszy Filistyna zabił go. Przetoż przysięgli mężowie Dawidowi, mówiąc mu: Nie pójdziesz więcej z nami na wojnę, abyś nie zgasił pochodni Izraelskiej.
Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
18 I stało się potem, że była znowu wojna w Gob z Filistynami, i zabił Sobochaj Husatycki Safa, który był z synów tegoż olbrzyma.
Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
19 Była też jeszcze inna wojna w Gob z Filistynami, kędy zabił Elhana, syna Jaara Oregim, Betlehemczyk, brata Golijatowego z Giet, którego drzewce u włóczni było jako nawój tkacki.
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
20 Nadto jeszcze była wojna w Giet, kędy był mąż wielkiego wzrostu, mając po sześć palców u rąk swoich, i po sześć palców u nóg swoich, wszystkich dwadzieścia i cztery; a ten też był synem tegoż olbrzyma.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
21 Ten gdy urągał Izraelowi, zabił go Jonatan, syn Samaa, brata Dawidowego.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 Ci czterej byli synowie jednego olbrzyma z Giet, a ci polegli od ręki Dawidowej, i od ręki sług jego.
Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

< II Samuela 21 >