< II Samuela 2 >
1 I stało się potem, że pytał Dawid Pana, mówiąc: Mamże iść do któregokolwiek miasta Judzkiego? Któremu Pan odpowiedział: Idź. I rzekł Dawid: Dokądże pójdę? I odpowiedział: Do Hebronu.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 Tedy tam jechał Dawid, także i dwie żony jego, Achinoam Jezreelitka, i Abigail żona przedtem Nabalowa z Karmelu.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Także męże swe, którzy z nim byli, zabrał Dawid, każdego z domem jego, i mieszkali w miastach Hebrońskich.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Przyszli potem mężowie Juda, i pomazali tam Dawida za króla nad domem Juda; tedy opowiadano Dawidowi, mówiąc: Mężowie z Jabes Galaad ci pogrzebli Saula.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 Tedy wyprawił Dawid posły do mężów z Jabes Galaad, i rzekł do nich: Błogosławieniście wy od Pana, którzyście ucznili to miłosierdzie nad Panem waszym Saulem, żeście go pogrzebli.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Przetoż teraz niech uczyni Pan z wami miłosierdzie, i prawdę, a ja też oddam wam to dobrodziejstwo, żeście uczynili tę rzecz.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Teraz tedy niech się zmacniają ręce wasze, a bądźcie mężnymi; bo choć umarł Saul, pan wasz, wszakże mnie pomazał dom Juda za króla nad sobą.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 A Abner, syn Nera, hetman nad wojskiem Saulowem, wziął Izboseta syna Saulowego, i przyprowadził go do Machanaim,
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 I uczynił go królem nad Gaaladem, i nad Assury, i nad Jezreelem, i nad Efraimem, i nad Benjaminem, i nad wszystkim Izraelem.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Czterdzieści lat miał Izboset, syn Saula, gdy począł królować nad Izraelem, a dwa lata królował; tylko dom Juda stał przy Dawidzie.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 I była liczba dni, których był Dawid królem w Hebronie nad domem Judzkim, siedm lat i sześć miesięcy.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Potem wyszedł Abner, syn Nera, i słudzy Izboseta, syna Saulowego, z Machanaim do Gabaonu.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Joab także, syn Sarwii, z sługami Dawidowymi wyszli, i spotkali się z sobą prawie u stawu Gabaońskiego, i zostali jedni na jednej stronie stawu, a drudzy na drugiej stronie stawu.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Tedy rzekł Abner do Joaba: Niech teraz wstaną młodzieńcy, a poigrają przed nami. I rzekł Joab: Niech wstaną.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Wstali tedy; i wyszło w liczbie dwanaście z Benjamińczyków ze strony Izboseta, syna Saulowego, a dwanaście z sług Dawidowych.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Którzy uchwyciwszy się, każdy za głowę przeciwnika swego, utopił miecz swój w boku jeden drugiego, i polegli pospołu. Przetoż nazwano miejsce ono Helkatassurym, które jest w Gabaonie.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 I była bitwa bardzo sroga dnia onego, a porażon jest Abner i mężowie Izraelscy od sług Dawidowych.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 I byli też tam trzej synowie Sarwii: Joab, Abisaj, i Asael; ale Asael był prędkich nóg, jako dzika koza.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 I gonił Asael Abnera, a nie ustąpił idąc ani na prawo ani na lewo, ścigając Abnera.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 A obejrzawszy się Abner nazad, rzekł: Tyżeś jest Asael? A on mu odpowiedział: Ja.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Tedy mu rzekł Abner: Uchyl się na prawą stronę twoję, albo na lewą stronę twoję, a pojmij sobie jednego z młodzieńców, i weźmij sobie łupy z niego; ale Asael nie chciał od niego ustąpić.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Tedy po wtóre rzekł Abner do Asaela: Idź precz ode mnie, bym cię snać nie przebił ku ziemi; bo jakoże bym śmiał podnieść twarz moję na Joaba, brata twego?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 A gdy nie chciał ustąpić, uderzył go Abner końcem włóczni pod piąte żebro, tak iż wyszła włócznia na drugą stronę. Tamże padł, i umarł na onemże miejscu, a wszyscy, którzy przychodzili do onego miejsca, gdzie poległ Asael i umarł, zastanawiali się.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Wszakże gonili Joab i Abisaj Abnera; i zachodziło słońce, gdy przyszli do pagórka Amma, który jest przeciw Gia na drodze pustyni Gabaońskiej.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Tedy się zebrali synowie Benjaminowi do Abnera, skupiwszy się w jeden huf, i stanęli na wierzchu jednego pagórka.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 I zawołał Abner na Joaba i rzekł: Izali się na wieki będzie srożył ten miecz? azaż nie wiesz, że na ostatku bywa gorzkość? i dokądże nie rzeczesz ludowi, aby się wrócił od pogoni braci swych?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Tedy rzekł Joab: Jako żywy Bóg, byś ty był nie wyzywał, zarazby się był z poranku lud wrócił, każdy od pogoni braci swych.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 A tak zatrąbił Joab w trąbę i zastanowił się wszystek lud, a nie gonili dalej Izraela, ani się więcej potykali.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Ale Abner i mężowie jego szli polem całą onę noc, a przeprawiwszy się przez Jordan, przeszli przez wszystko Betoron, aż przyszli do Mahanaim.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 A Joab wróciwszy się z pogoni za Abnerem, zebrał wszystek lud, i nie dostawało mu sług Dawidowych dziewiętnastu mężów, i Asaela.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Ale słudzy Dawidowi pobili z Benjamińczyków, i z mężów Abnerowych trzy sta i sześćdziesiąt mężów, którzy tam pomarli.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 A wziąwszy Asaela, pogrzebli go w grobie ojca jego, który był w Betlehem; potem szli całą noc Joab i mężowie jego, a na świtaniu przyszli do Hebronu.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.