< II Królewska 11 >

1 Tedy Atalija, matka Ochozyjaszowa, widząc iż umarł syn jej, powstała, i wytraciła wszystko nasienie królewskie.
Basi Athalia, mama yake na Ahazia, alipoona kwamba mtoto wake amekufa, aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme.
2 Ale wziąwszy Josaba, córka króla Jorama, siostra Ochzyjaszowa, Joaza, syna Ochozyjaszowego, ukradła go z pośrodku synów królewskich, które zabijano; tego i z mamką jego w pokoju łożnicy skryła przed Ataliją, i nie zabito go.
Lakini Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu na dada wa Ahazia, akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa.
3 I był przy niej w domu Pańskim skryty przez sześć lat, których Atalija królowała nad ziemią.
Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi.
4 Potem roku siódmego posławszy Jojada, przyzwał rotmistrzów, hetmanów i żołnierzy, i wprowadził je do siebie do domu Pańskiego, a uczyniwszy z nimi przymierze, przywiódł, je do przysięgi w domu Pańskim, i ukazał im syna królewskiego.
Katika mwaka wa saba, Yehoyada alituma ujumbe na kuleta maamiri jeshi mamia wa Wakari na wa walinzi, na kuwaleta kwake mwenyewe, ndani ya nyumba ya Yahwe. Akafanya agano pamoja nao, na kuwaapisha kiapo katika nyumba ya Yahwe. Kisha akawaonyesha mtoto wa mfalme.
5 I rozkazał im, mówiąc: Toć jest co uczynicie: trzecia część z was, którzy przychodzicie w sabat, a trzymywacie straż, niech będzie przy domu królewskim:
Akawaamuru, akisema, “Hivi ndivyo mnavyotakiwa kufanya. Theluthi yenu mtakaokuja kwenye Sabato mtakuwa mkiiangalia nyumba ya mfalme,
6 A trzecia część z was zostanie w bramie Sur; trzecia część zasię będzie w bramie, która jest za żołnierzami; a będziecie trzymali straż przy tym domu dla jakiego gwałtu.
na theluthi mtakuwa langoni mwa Suri, na theluthi langoni nyuma ya walinzi.”
7 A dwie części z was wszystkich wychodzących w sabat niech trzymają straż domu Pańskiego około króla.
Makundi mengine mawili ambayo hayatumikii Sabato, Mtayalinda juu ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya mfalme.
8 A tak obstąpicie króla około, każdy mając broń swą w rękach swych; a ktobykolwiek przyszedł do waszego szyku, niech będzie zabity, a wy będziecie przy królu, gdy wychodzić i wchodzić będzie.
Ni lazima mumzunguke mfalme, kila mmoja na silaha zake kwenye mkono wake. Yeyote aingiaye ndani ya safu, auwawe. Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo.
9 I uczynili rotmistrze oni według wszystkiego, co im był rozkazał Jojada kapłan; a wziąwszy każdy męże swe, którzy przychodzili w sabat, i którzy odchodzili w sabat, przyszli do Jojady kapłana.
Hivyo mamia ya maamri jeshi wakatii kila kitu Yehoyada kuhani alichokiamuru. Kila mmoja akachukua watu wake, wale ambao walitakiwa kuja kutumika siku ya hiyo Sabato, na wale ambao wataacha kuitumika kwenye hiyo Sabato; ndipo wakaja kwa Yehoyada kuhani.
10 Tedy dał kapłan rotmistrzom włócznie i tarcze, które były króla Dawida, które były w domu Pańskim.
Kisha Yehoyada yule kuhani akawapa mikuki na ngao mamia wa maamri jeshi ambayo ilikuwa mali ya mfalme Daudi ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe.
11 I stali żołnierze, każdy mając broń swoję w rękach swych, od prawej strony domu aż do lewej strony domu przeciwko ołtarzowi, i przeciwko domowi około króla zewsząd.
Basi walinzi wakasimama, kila mtu na silaha kwenye mkono wake, kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu, wakimzunguka mfalme.
12 Tedy wywiódł syna królewskiego, i włożył nań koronę, i świadectwo. I uczynili go królem, i pomazali go, a klaskając rękoma mówili: Niech żyje król!
Kisha Yehoyada akamleta nje mtoto wa mfalme Yoashi, na kumvalisha taji la kifalme, na kumpatia mikataba ya agano. Kisha wakamfanya mfalme na kummiminia mafuta. Wakapiga makofi wakisema, “Mfalme na aishi!”
13 Wtem usłyszawszy Atalija krzyk zbiegającego się ludu, weszła do ludu do domu Pańskiego.
Wakati Athalia aliposikia sauti za walinzi na za watu, alikuja kwa wale watu kwenye nyumba ya Yahwe.
14 A gdy ujrzała, że oto król stał na majestacie według zwyczaju, a książęta i trąby około króla, a wszystek lud ziemi weselący się, i trąbiący w trąby, rozdarła Atalija odzienie swoje, i wołała: Sprzysiężenie, sprzysiężenie!
Akatazama, na, kisha, yule mfalme alikuwa amesimama kwenye nguzo, kama ilivyokuwa desturi, na manahodha na wapiga mabaragumu walikuwa karibu na mfalme. Watu wote wa nchi hiyo walikuwa wakifurahi na kupiga matarumbeta. Kisha Athalia akachana mavazi yake kwa hasira na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”
15 Przetoż rozkazał Jojada kapłan rotmistrzom, którzy byli nad wojskiem, i rzekł do nich: Wywiedźcie ją z zagrodzenia kościoła, a ktobykolwiek chciał iść za nią, niech zabity będzie mieczem; bo rzekł był kapłan: Niech nie będzie zabita w domu Pańskim.
Ndipo Yehoyada yule kuhani akawaagiza maamri jeshi wa mamia ambao waliokuwa juu ya jeshi, akisema, “Mtoeni kwenye safu.” Atakayemfuata, muueni kwa upanga.” Kwa kuwa kuhani alisema, “Msimwache auawe kwenye nyumba ya Yahwe.”
16 I uczynili jej plac; a gdy przyszła na drogę, którą wodzono konie do domu królewskiego, tamże jest zabita.
Hivyo wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko.
17 Tedy uczynił Jojada przymierze między Panem, i między królem, i między ludem, aby byli ludem Pańskim; także między królem i między ludem.
Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yahwe na mfalme na watu, ambao wangekuwa watu wa Yahwe, na pia kati ya mfalme na watu.
18 I wszedł wszystek lud onej ziemi do domu Baalowego, i zburzyli go; ołtarze jego i obrazy jego połamali do szczętu; nadto Matana, kapłana Baalowego, zabili przed ołtarzami. I postanowił znowu kapłan przełożone nad domem Pańskim.
Basi watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuingusha chini. Wakaangusha madhabahu ya Baali na sanamu zake wakazivunja vipande vipande, na kumuua Matani, mfalme wa Baali, mbele ya haya madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawachagua walinzi juu ya hekalu la Yahwe.
19 Potem wziąwszy rotmistrze, i hetmany, i żołnierze, i wszystek lud onej ziemi, prowadzili króla z domu Pańskiego, i przyszli drogą aż ku bramie żołnierzy, do domu królewskiego. I usiadł na stolicy królewskiej.
Yehoyada akawachukua maamiri jeshi wa mamia, Wakari, walinzi, na watu wote wa nchi, na kwa pamoja wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme, wakaingia kwa njia ya lango la walinzi. Yoashi akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi cha mfalme.
20 I weselił się wszystek lud onej ziemi, a miasto się uspokoiło, gdy Ataliją zabito mieczem podle domu królewskiego.
Hivyo watu wote wa nchi wakamsifu, na nchi ilikuwa kimya baada ya Athalia kuuawa kwa upanga kwenye nyumba ya mfalme.
21 A było siedm lat Joazowi, gdy począł królować.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba tangu alipoanza kutawala.

< II Królewska 11 >