< II Królewska 10 >

1 A miał Achab siedmdziesiąt synów w Samaryi. I napisał Jehu list, a posłał go do Samaryi do książąt Jezreelskich, i do starszych i do tych, którzy wychowywali syny Achabowe, w te słowa:
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 Skoro was dojdzie ten list, gdyż u was są synowie pana waszego, i u was wozy, i konie, i miasto obronne, i rynsztunek;
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 Obierzcież najgodniejszego i najsposobniejszego z synów pana waszego, a posadźcie na stolicy ojca jego, i walczcie o dom pana waszego.
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 Ale się oni bardzo bojąc rzekli: Oto dwaj królowie nie ostali się przed nim, a jakoż my się ostoimy?
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 A tak posłał ten, który był sprawcą domu, i ten, który był sprawcą miasta, i starsi, i ci, którzy wychowywali syny królewskie, do Jehu, mówiąc: Słudzyśmy twoi, a co nam rozkażesz, uczynimy. Nie postanowiemy króla żadnego; co dobrego jest w oczach twoich, czyń.
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 I napisał do nich list drugi, mówiąc: Jeźliście moi, a głosu mego słuchacie, weźmijcież głowy synów pana waszego, a przyjdźcie do mnie jutro o tym czasie do Jezreel. A synów królewskich było siedmdziesiąt mężów u najprzedniejszych w mieście, którzy je wychowywali.
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 A gdy ich list doszedł, wziąwszy syny królewskie, pobili onych siedmdziesiąt mężów, a składłszy głowy ich do koszów, posłali je do niego do Jezreela.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 I przyszedł poseł, który mu oznajmił, mówiąc: Przyniesiono głowy synów królewskich. A on rzekł: Składźcie je na dwie kupie u wejścia bramy aż do poranku.
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 A gdy rano wyszedł, stanął, i rzekł do wszystkiego ludu: Sprawiedliwiście wy. Otom się ja sprzysiągł przeciwko panu memu, i zabiłem go; ale te wszystkie któż pobił?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Wiedzcież teraz, że nie upadło próżno żadne z słów Pańskich na ziemię, które mówił Pan przeciwko domowi Achabowemu, gdyż uczynił Pan, co był powiedział przez sługę swego Elijasza.
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 A tak pobił Jehu wszystkie, którzy pozostali z domu Achabowego w Jezreelu, i wszystkie najprzedniejsze jego, i przyjaciele jego, i kapłany jego, tak iż nie zostawił po nim żadnego żywego.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 Potem wstawszy odszedł, i pojechał do Samaryi. A gdy był a domu, gdzie pasterze strzygali owce na drodze,
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 Tedy Jehu znalazł u braci Ochozyjasza króla Judzkiego, i rzekł: Któście wy? I odpowiedzieli: Braciaśmy Ochozyjaszowi, a idziemy, abyśmy pozdrowili syny królewskie, i syny królowej.
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 Tedy rzekł: Pojmajcie je żywo. I pojmali je żywo, i pobili je u studni onegoż domu, gdzie strzygano owce, czterdziestu i dwóch mężów, i nie zostawił żadnego z nich.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 Potem odjechawszy stamtąd, trafił Jonadaba, syna Rechabowego, idącego przeciwko sobie, a pozdrowił go i rzekł do niego: Jestże serce twoje szczere, jako serce moje z sercem twojem? I odpowiedział mu Jonadab: Jest. A jest? rzekł Jehu, dajże mi rękę twoję. Tedy mu dał rękę swą; i kazał mu wsiąść do siebie na wóz.
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 I rzekł: Jedź ze mną, a przypatrz się gorliwości mojej za Pana. A tak wiózł go na wozie swoim.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 A gdy przyjechał do Samaryi, bił wszystkie, którzy byli pozostali z domu Achabowego w Samaryi, i wytracił je według słowa Pańskiego, który mówił do Elijasza.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 Zatem zebrał Jehu wszystek lud, i rzekł do niego: Achab służył Baalowi mało, Jehu mu będzie służył więcej.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 Przetoż teraz wszystkich proroków Baalowych, i wszystkich sług jego, i wszystkich kapłanów jego, zwołajcie do mnie aż do jednego; albowiem ofiarę wielką będę sprawował Baalowi. Ktoby się kolwiek nie stawił, nie zostanie żyw. A to Jehu chytrze czynił, chcąc wytracić chwalce Baalowe.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 Nadto rzekł Jehu: Zapowiedzcie święto Baalowi. I obwołano je.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 I rozesłał Jehu do wszystkiego Izraela. I zeszli się wszyscy chwalcy Baalowi, tak że nie został żaden, któryby nie przyszedł. I weszli do kościoła Baalowego, a napełniony był dom Baalowy od końca aż do końca.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 Tedy rzekł temu, który był nad szatami: Wynieś szaty wszystkim chwalcom Baalowym. I wyniósł im szaty.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 Zatem wszedł Jehu i Jonadab, syn Rechabowy, do domu Baalowego, i rzekł chwalcom Baalowym: Dowiedzcie się, a obaczcie, by snać nie był kto z wami z chwalców Pańskich, oprócz samych chwalców Baalowych.
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 A tak weszli, aby sprawowali ofiary, i całopalenia. Ale Jehu sporządził był sobie na dworze ośmdziesiąt mężów, którym był rzekł: Jeźliby kto uszedł z ludu tego, który ja podawam w ręce wasze, dusza wasza będzie za duszę onego.
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 A gdy się dokończyły ofiary całopalenia, rzekł Jehu żołnierzom i rotmistrzom swym: Wnijdzcie, a pomordujcie je, aby żaden nie uszedł. A tak pomordowali je ostrzem miecza, i rozrzucili je żołnierze i rotmistrze; potem odeszli do każdego miasta, gdzie był dom Baalowy.
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 A wyrzuciwszy bałwany z domu Baalowego, popalili je.
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 Obalili też słup Baalowy, obalili i dom jego, a uczynili z niego wychody, aż do tego czasu.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 A tak wygładził Jehu Baala z Izraela.
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 Wszakże od grzechów Jeroboama, syna Nabatowego, który do grzechu przywiódł Izraela, nie odstąpił Jehu, ani opuścił cielców złotych, które były w Betel, i które były w Dan.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 Tedy rzekł Pan do Jehu: Ponieważeś się pilnie starał, abyś uczynił, co dobrego jest w oczach moich, według wszystkiego, co było w sercu mojem, uczyniłeś domowi Achabowemu: synowie twoi aż do czwartego pokolenia siedzieć będą na stolicy Izraelskiej.
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 Ale Jehu nie strzegł tego, aby chodził w zakonie Pana, Boga Izraelskiego, ze wszystkiego serca swego, ani odstąpił od grzechów Jeroboamowych, który do grzechu przywiódł Izraela.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 W one dni począł Pan umniejszać Izraela: bo je poraził Hazael po wszystkich granicach Izraelskich:
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 Od Jordanu aż na wschód słońca, wszystkę ziemię Galaadską, Gadową, i Rubenową, i Manasesową od Aroer, które jest u potoku Arnon, i Galaad, i Basan.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 Ale ostatek spraw Jehu, i wszystko, co czynił, i wszystka moc jego, azaż tego nie napisano w kronikach królów Izraelskich?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 I zasnął Jehu z ojcami swymi, i pochowali go w Samaryi; a królował Joachaz, syn jego, miasto niego.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 A czas, którego królował Jehu nad Izraelem w Samaryi, było dwadzieścia i ośm lat.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< II Królewska 10 >