< II Koryntian 9 >
1 Lecz o usłudze, która się dzieje świętym, niepotrzebna mi jest wam pisać.
Kuhusiana na huduma kwa ajili ya waumini, ni bora zaidi kwangu kuwaandikia.
2 Bo znam ochotę umysłu waszego, którą się ja chlubię z was u Macedończyków, iż Achaja gotowa była od przeszłego roku; a ta wasza gorliwość wiele ich pobudziła.
Ninajua kuhusu shauku yenu, ambayo nilijivunia kwa watu wa Makedonia. Niliwaambia kwamba Akaya imekuwa tayari tangu mwaka uliopita. Hamu yenu imewatia moyo wengi wao kutenda.
3 Posłałem tedy tych braci, żeby chluba nasza, którą mamy z was, nie była daremna z tej miary, ale abyście (jakom powiedział), gotowymi byli;
Sasa, nimewatuma ndugu ili kwamba majivuno yetu kuhusu ninyi yasiwe ya bure, na ili kwamba mngekuwa tayari, kama nilivyosema mngekuwa.
4 Abyśmy snać, jeźliby ze mną przyszli Macedończycy, a znaleźli was niegotowymi, nie zawstydzili się my, (że nie rzekę wy), za tak bezpieczną chlubę.
Vinginevyo, kama mtu yeyote wa Makedonia akija pamoja nami na kuwakuta hamjawa tayari, tungeona haya — sisemi chochote kuhusu ninyi—kwa kuwa jasiri sana katika ninyi.
5 Zdało mi się tedy za rzecz potrzebną, napomnieć braci, aby do was wprzód poszli i pierwej zgotowali przedtem opowiedzianą waszę szczodrobliwość, aby była gotowa tak jako szczodrobliwość, a nie jako rzecz przymuszona.
Hivyo niliona ilikuwa muhimu kuwasihi ndugu kuja kwenu na kufanya mipango mapema kwa ajili ya zawadi mlizoahidi. Hii ni hivyo ili kwamba ziwe tayari kama baraka, na si kama kitu kilichoamriwa.
6 Ale tak mówię: Kto skąpo sieje, skąpo też żąć będzie; a kto obficie sieje, obficie też żąć będzie.
Wazo ni hili: mtu apandaye haba pia atavuna haba, na yeyote apandaye kwa lengo la baraka pia atavuna baraka.
7 Każdy jako umyślił w sercu swem, tak niech uczyni, nie z zamarszczeniem ani z przymuszenia; albowiem ochotnego dawcę Bóg miłuje.
Basi na kila mmoja atoe kama alivyopanga moyoni mwake. Basi naye asitoe kwa huzuni au kwa kulazimishwa. Kwa kuwa Mungu humpenda yule atoaye kwa furaha.
8 A mocen jest Bóg uczynić, aby obfitowała na was wszelka łaska, abyście mając we wszystkiem zawsze wszelaki dostatek, obfitowali ku wszelakiemu uczynkowi dobremu,
Na Mungu anaweza kuizidishia kila baraka kwa ajili yenu, ili kwamba, kila wakati, katika mambo yote, muweze kupata yote mnayohitaji. Hii itakuwa ili kwamba mueze kuzidisha kila tendo jema.
9 Jako napisane: Rozproszył, dał ubogim, sprawiedliwość jego zostaje na wieki. (aiōn )
Ni kama ilivyoandikwa: “Ametapanya utajiri wake na kuutoa kwa maskini. Haki yake yadumu milele.” (aiōn )
10 A ten, który daje nasienie siejącemu, niechże i wam da chleb ku jedzeniu i rozmnoży nasienie wasze, i przysporzy urodzajów sprawiedliwości waszej,
Naye atoaye mbegu kwa mpanzi na mkate kwa ajili ya chakula, pia atatoa na kuzidisha mbegu yenu kwa ajili ya kupanda. Yeye ataongeza mavuno ya haki yenu.
11 Abyście z każdej miary byli ubogaceni ku wszelkiej prostości, która sprawuje przez nas, aby dzięki Bogu czynione były.
Mtatajirishwa kwa kila namna ili kwamba muweze kuwa wakarimu. Hii italeta shukrani kwa Mungu kupitia sisi.
12 Albowiem usługiwanie tej ofiary nie tylko dopełnia niedostatki świętych, ale też opływa przez wielkie dziękczynienia na Boga przez pochwałę tej posługi;
Kwa kufanya huduma hii sio tu inagusa mahitaji ya waumini. Pia huzidisha katika matendo mengi ya shukrani kwa Mungu.
13 Gdy Boga chwalą za wasze poddaństwo Ewangielii Chrystusowej, za szczerość w udzielaniu przeciwko sobie i przeciwko wszystkim innym;
Kwa sababu ya kupimwa kwenu na kuthibitishwa kwa huduma hii, pia mtamtukuza Mungu kwa utii kwa ukiri wenu wa injili ya Kristo. Pia mtamtukuza Mungu kwa ukarimu wa karama yenu kwao na kwa kila mmoja.
14 I modlą się za wami, żądając was dla łaski Bożej obfitującej w was.
Wanawatamani, na wanaomba kwa ajili yenu. Wanafanya hivi kwa sababu ya neema kubwa ya Mungu iliyo juu yenu.
15 Lecz Bogu niech będzie chwała za niewypowiedziany dar jego.
Shukrani ziwe kwa Mungu kwa karama yake isiyoelezeka!