< II Kronik 26 >
1 Tedy wszystek lud Judzki wzięli Uzyjasza, który miał szesnaście lat, i postanowili go królem miasto ojca jego Amazyjasza.
Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
2 Ten pobudował Elat, a przywrócił je do Judy, gdy zasnął król z ojcami swymi.
Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
3 Szesnaście lat było Uzyjaszowi, gdy królować począł, a pięćdziesiąt i dwa lata królował w Jeruzalemie; a imię matki jego Jechalija z Jeruzalemu.
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
4 Ten czynił, co było dobrego w oczach Pańskich według wszystkiego, jako czynił Amazyjasz, ojciec jego.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
5 I szukał Boga za dnia Zacharyjasza, rozumiejącego widzenia Boże; a po wszystkie one dni, których szukał Pana, szczęścił go Bóg.
Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
6 Bo ruszywszy się, walczył z Filistynami, i poburzył mury w Get, i mury w Jabnie, i mury w Azocie, a pobudował miasta w Azocie i w ziemi Filistyńskiej.
Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
7 Albowiem pomagał mu Bóg przeciw Filistynom, i przeciw Arabczykom, którzy mieszkali w Gurbaalu, i przeciw Mahunitom.
Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
8 I dawali Ammonitowie Uzyjaszowi dary, a rozniosło się imię jego aż do samego Egiptu; bo się był zmocnił nader bardzo.
Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
9 I budował Uzyjasz wieże w Jeruzalemie nad bramą narożną, i nad bramą doliny, i nad Mikzoa, i umocnił je.
Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
10 Pobudował też wieże na puszczy, i pokopał wiele studzien; bo miał bardzo wiele stad, tak w dolinach, jako i w równinach, i rolników, i winiarzy po górach, i na Karmelu: albowiem się kochał w uprawianiu ról.
Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
11 Miał też Uzyjasz wojsko gotowe do bitwy, które wychodziło na wojnę w pocztach swych według liczby, jako byli obliczeni przez Jechijela kanclerza, i Maasajasza kapłana, pod sprawą Hananijasza, książęcia królewskiego.
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
12 Wszystka liczba przedniejszych z domów ojcowskich, ludzi rycerskich, dwa tysiące i sześć set.
Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
13 A pod sprawą ich ludu walecznego trzy kroć i sto tysięcy, i siedm tysięcy i pięć set, ludu sposobnego do wojny, na pomoc królowi przeciw nieprzyjacielowi.
Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
14 I zgotował Uzyjasz wszystkiemu onemu wojsku tarcze i drzewce, i przyłbice, i pancerze, i łuki, i kamienie do proc.
Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
15 Naczynił też w Jeruzalemie sztuk wojennych bardzo misternych, aby były na wieżach, i na węgłach ku wypuszczaniu strzał, i kamienia wielkiego; i rozniosło się imię jego daleko, przeto, że miał dziwną pomoc, aż się zmocnił.
Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
16 Ale gdy się zmocnił, podniosło się serce jego ku zginieniu jego, i wystąpił przeciw Panu, Bogu swemu, i wszedł do kościoła Pańskiego, aby kadził na ołtarzu kadzenia.
Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
17 I wszedł za nim Azaryjasz kapłan, a z nim kapłanów Pańskich ośmdziesiąt, mężów dużych.
Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
18 I stanęli przeciw Uzyjaszowi królowi, a mówili mu: Nie twoja to rzecz Uzyjaszu! kadzić Panu, ale kapłanów, synów Aaronowych, którzy są poświęceni, aby kadzili. Wynijdźże z świątnicy; albowiemeś wystąpił, a nie będzieć to ku sławie przed Panem Bogiem.
Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
19 Przetoż się rozgniewał Uzyjasz, mając w rękach swych kadzielnicę, aby kadził. A gdy się srożył przeciwko kapłanom, trąd wystąpił na czoło jego przed kapłanami w domu Pańskim u ołtarza kadzenia.
Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
20 A wejrzawszy nań Azaryjasz, kapłan najwyższy, i wszyscy kapłani, a oto był trędowatym na czole swojem; przetoż prędko wygnali go stamtąd; owszem i sam pospieszał wynijść, przeto, iż go zaraził Pan.
Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
21 A tak był król Uzyjasz trędowatym aż do dnia śmierci swej, i mieszkał w domu osobnym, będąc trędowatym; albowiem był wyłączon z domu Pańskiego; międzytem Joatam, syn jego, był nad domem królewskim, sądząc lud ziemi.
Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
22 A inne sprawy Uzyjaszowe, pierwsze i poślednie, opisał prorok Izajasz, syn Amosowy.
Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23 I zasnął Uzyjasz z ojcami swymi, a pochowano go z ojcami jego na polu grobów królewskich; bo mówili: Trędowaty jest. A królował Joatam, syn jego, miasto niego.
Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.