< I Tesaloniczan 2 >
1 Albowiem wy sami wiecie, bracia! że przyjście nasze do was nie było próżne;
Ndugu, ninyi wenyewe mnafahamu kwamba ziara yetu kwenu haikuwa bure.
2 Ale chociażeśmy i przedtem cierpieli, i zelżeni byli (jako wiecie) w mieście Filipach, wszakże bezpiecznieśmy sobie poczęli w Bogu naszym, w opowiadaniu u was Ewangielii Bożej z wielkim bojem,
Mnajua jinsi tulivyodhulumiwa na kutukanwa kule Filipi kabla ya kufika kwenu Thesalonike. Ingawa kulikuwa na upinzani mwingi, Mungu wetu alitujalia uhodari wa kuwahubirieni Habari Njema yake.
3 Albowiem napominanie nasze nie było z oszukania, ani z nieczystości, ani z zdrady;
Jambo tunalosisitiza kwenu si jambo linalotegemea uongo au nia mbaya; wala hatupendi kumdanganya mtu yeyote.
4 Ale jako nas Bóg sobie upodobał, żeby nam była zwierzona Ewangielija, tak mówimy, nie jako ludziom się podobając, ale Bogu, który sobie upodobywa serca nasze.
Sisi twanena daima kama atakavyo Mungu kwani yeye alituona kwamba tunafaa, akatukabidhi hii Habari Njema. Si nia yetu kuwapendeza watu hata kidogo, bali twataka kumpendeza Mungu ambaye anajua mioyo yetu mpaka ndani.
5 Albowiem nigdyśmy nie używali mowy pochlebnej, jako wiecie; aniśmy pod zasłoną czego łakomstwu dogadzali; Bóg jest świadkiem;
Ninyi mnajua kwamba sisi hatukuja kwenu na maneno matamu ya kubembeleza wala hatukutumia maneno ya kijanja ya kuficha ubinafsi fulani; Mungu ni shahidi!
6 Aniśmy szukali od ludzi chwały, ani od was, ani od inszych, mogąc wam być ciężkimi, jako Apostołowie Chrystusowi;
Hatukutafuta sifa kutoka kwa watu, wala kutoka kwenu, wala kutoka kwa mtu yeyote,
7 Aleśmy byli skromnymi między wami, jako gdy mamka odchowuje dziatki swoje.
ingawa sisi tukiwa mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulikuwa Wapole kati yenu kama alivyo mama kwa watoto wake.
8 Tak wam życzliwymi będąc, gotowiśmy byli użyczyć wam nie tylko Ewangielii Bożej, ale też i dusz naszych, dlatego iżeście nam miłymi byli.
Tuliwapenda ninyi sana hata tukawa tayari kuwashirikisha si tu Habari Njema ya Mungu, bali pia na maisha yetu. Ndivyo mlivyokuwa wapenzi wetu!
9 Albowiem pamiętajcie, bracia! pracę naszę i trudy, gdyż w nocy i we dnie robiąc, abyśmy żadnego z was nie obciążyli, kazaliśmy u was Ewangielię Bożą.
Ndugu, mnakumbuka jinsi tulivyofanya kazi na kutaabika. Tulipowaleteeni Habari Njema ya Mungu tulifanya kazi mchana na usiku kusudi tusiwe mzigo kwa mtu yeyote miongoni mwenu.
10 Wyście świadkami i Bóg, żeśmy świętobliwie i sprawiedliwie, i bez nagany żyli między wami, którzyście uwierzyli.
Ninyi mnaweza kushuhudia, na Mungu pia ni shahidi, jinsi mwenendo wetu kati yenu ninyi mnaoamini ulivyokuwa mzuri, mwadilifu na usio na lawama.
11 Jakoż wiecie, żeśmy każdego z was, jako ojciec dziatki swoje, napominali i cieszyli,
Mnajua kwamba sisi tulimtendea kila mmoja wenu kama vile baba anavyowatendea watoto wake mwenyewe.
12 I oświadczali się, abyście chodzili godnie Bogu, który was powołał do swego królestwa i do chwały.
Tuliwapeni moyo, tuliwafarijini na kuwahimiza ili mpate kuishi maisha yampendezayo Mungu ambaye aliwaiteni mshiriki Utawala na utukufu wake.
13 Przetoż i my dziękujemy Bogu bez przestanku, iż przyjąwszy słowo Boże, któreście słyszeli od nas, przyjęliście nie jako słowo ludzkie, ale (jako w prawdzie jest) jako słowo Boże, które też skuteczne jest w was, którzy wierzycie.
Tena tunayo sababu nyingine ya kumshukuru Mungu: tulipowaleteeni ujumbe wa Mungu, ninyi mliusikia mkaupokea, si kama vile ujumbe wa binadamu, bali kama ujumbe wa Mungu, na kweli ndivyo ulivyo. Maana Mungu anafanya kazi ndani yenu ninyi mnaoamini.
14 Albowiem wy, bracia! staliście się naśladowcami zborów Bożych, które są w żydowskiej ziemi, w Chrystusie Jezusie; boście i wy też cierpieli od ziomków waszych, jako i oni od Żydów.
Ndugu, ninyi mmepatwa na mambo yaleyale yaliyoyapata makanisa ya Mungu kule Yudea, mambo yaliyowapata watu walio wake Kristo Yesu. Ninyi mlidhulumiwa na wananchi wenzenu kama vile wao walivyodhulumiwa na wenzao Wayahudi,
15 Którzy i Pana Jezusa zabili, i swoich własnych proroków, i nas wygnali, a Bogu się nie podobają, i wszystkim ludziom są przeciwni,
ambao walimuua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa na sisi pia. Watu hao wanamchukiza Mungu, tena ni adui za kila mtu!
16 Zabraniając nam, żebyśmy nie mówili poganom, żeby byli zbawieni, aby tak zawsze dopełniali grzechów swoich; albowiem przyszedł na nich gniew aż do końca.
Hata walijaribu kutuzuia kuwahubiria watu wa mataifa mengine ujumbe utakaowaletea wokovu. Ndivyo walivyokamilisha orodha ya dhambi zote walizotenda siku zote. Lakini sasa hasira ya Mungu imewaangukia.
17 Lecz my, bracia! będąc pozbawieni was na chwileczkę obliczem, nie sercem, tem pilniejśmy się starali oglądać oblicze wasze z wielką żądnością.
Ndugu, kuachana kwetu nanyi kulikuwa kwa muda tu, tena kuachana huko kulikuwa kwa mwili tu na si kwa roho. Kitambo kifupi baadaye, tulishikwa na hamu kubwa ya kuwaoneni tena!
18 Dlategośmy chcieli przyjść do was (zwłaszcza ja Paweł) i raz, i drugi; ale nam przekaził szatan.
Kwa hiyo tuliamua kuwatembeleeni tena. Nami, Paulo, nilijaribu kuja kwenu zaidi ya mara moja, lakini Shetani alituzuia.
19 Albowiem któraż jest nadzieja nasza, albo radość, albo korona chluby? Izali nie wy przed oblicznością Pana naszego, Jezusa Chrystusa w przyjście jego?
Je, tutakaposimama mbele ya Bwana Yesu wakati atakapokuja, fahari ya ushindi wetu itakuwa nini? Itakuwa ni ninyi wenyewe; ninyi ndio tumaini letu na furaha yetu.
20 Wy zaiste jesteście chwałą naszą i radością.
Naam, ninyi ni utukufu wetu na furaha yetu!