< I Samuela 2 >

1 Tedy się modliła Anna, i rzekła: Rozweseliło się serce moje w Panu, wywyższon jest róg mój w Panu, rozszerzyły się usta moje przeciw nieprzyjaciołom moim; albowiemem się rozradowała w zbawieniu twojem.
Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 Niemaszci świętego jako Pan; bo niemasz innego oprócz ciebie, i niemasz tak mocnego, jak Bóg nasz.
“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
3 Niemówcież napotem słów pysznych, a niech nie wychodzą słowa harde z ust waszych; albowiem Bóg jest umiejętności Panem, a nadawają się sprawy jego.
“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
4 Łuk i mocarze pokruszeni są, a mdli przepasani są mocą.
“Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
5 Którzy byli nasyceni, najmują się za chleb, a głodni przestali łaknąć; tak iż niepłodna siedmioro porodziła, a która rodziła wiele dziatek, zemdlała.
Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
6 Pan zabija i ożywia, wwodzi do grobu i wywodzi. (Sheol h7585)
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
7 Pan ubogiego czyni i zbogaca, uniża i wywyższa.
Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
8 Wzbudza z prochu ubogiego, a z gnoju podnosi żebraka, aby je posadził z książęty, a dał im stolicę chwalebną osiadać; albowiem Pańskie są grunty ziemi, a na nich założył świat.
Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
9 Nóg świętych swoich ochrania, a niepobożni w ciemnościach zamilkną; bo nie w sile swojej będzie się mąż zmacniał.
Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
10 Pan pokruszy przeciwniki swoje, a zagrzmi na nie z nieba; Pan będzie sądził granice ziemi, a da moc królowi swemu, i wywyższy róg pomazańca swego.
wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
11 A tak odszedł Elkana do Ramaty do domu swego, a dziecię służyło Panu przed Heli kapłanem.
Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
12 Ale synowie Heli byli synowie bezbożni, a nie znali Pana.
Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
13 Albowiem obyczaj kapłanów ten był około ludu: ktokolwiek sprawował ofiary, przychodził sługa kapłański, gdy warzono mięso, mając widełki o trzech zębach w ręce swojej.
Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
14 I wrażał je w statek, albo w kocieł, albo w panew, albo w garniec, a coklowiek wyjął widełkami, to sobie brał kapłan. Tak czynili wszystkim Izraelczykom, którzy tam do Sylo przychodzili.
Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
15 Także pierwej niż zapalono tłustość, tedy przychodził sługa kapłański, a mówił do człowieka ofiarującego: Oddaj mięso, abym je upiekł kapłanowi; albowiem nie weźmie od ciebie mięsa warzonego, jedno surowe.
Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
16 A jeźliż mu odpowiedział on człowiek: Niech się pierwej spali tłustość, potem sobie weźmiesz, czego będzie żądała dusza twoje, tedy on mówił: Nic z tego; teraz daj! a nie daszli, wezmę gwałtem.
Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
17 I był to grzech onych sług bardzo wielki przed Panem; bo się odtrącali ludzie od ofiar Pańskich.
Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
18 Ale Samuel służył przed Panem, ubrane chłopiątko w efod lniany.
Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
19 A matka jego uczyniwszy mu sukienkę małą, przynaszała mu co rok, gdy chadzała z mężem swym sprawować ofiarę uroczystą.
Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
20 I błogosławił Heli Elkanie, i żonie jego, mówiąc: Niech ci da Pan potomstwo z tej niewiasty za oddanego, którego wyprosiła u Pana. I poszli na miejsca swoje.
Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
21 Tedy nawiedził Pan Annę, która poczęła i porodziła trzech synów, i dwie córek; a pacholę Samuel urósł przed Panem.
Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
22 Ale Heli zstarzał się był bardzo, i słyszał wszystko, co czynili synowie jego całemu Izraelowi, i jako sypiali z niewiastami, które się schadzały przede drzwi namiotu zgromadzenia.
Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
23 I rzekł do nich: Przeczże takie rzeczy czynicie? Cóż ja słyszę o waszych złych sprawach od wszystkiego ludu?
Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
24 Nie tak synowie moi; bo nie dobra sława, którą ja słyszę, że przywodzicie ku przestępstwu lud Pański.
Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
25 Gdy kto zgrzeszy przeciw człowiekowi, sądzić go będzie sędzia, ale jeźli przeciw Panu kto zgrzeszy, któż się za nim ujmie? Lecz nie usłuchali głosu ojca swego; bo je chciał Pan pobić.
Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
26 Ale pacholę Samuel postępował a rósł, i podobał się tak Panu jako i ludziom.
Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
27 Potem przyszedł mąż Boży do Heli, i rzekł mu: Tak mówi Pan: Azalim się nie jawnie objawił domowi ojca twego, gdy byli w Egipcie w domu Faraonowym?
Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
28 I obrałem go sobie ze wszystkich pokoleń Izraelskich za kapłana, aby ofiarował na ołtarzu moim, a kadził rzeczami wonnemi, i nosił efod przedemną, i dałem domowi ojca twego wszystkie ofiary palone od synów Izraelskich.
Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
29 Przeczżeście podeptali ofiarę moję, i śniedną ofiarę moję, którąm rozkazał sprawować w przybytku? i więcejś uczcił syny swoje nad mię, abyście się utuczyli z pierwocin wszystkich ofiar śniednych Izraela, ludu mego?
Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
30 Prztoż mówi Pan, Bóg Izraelski: Rzekłem wprawdzie: Dom twój i dom ojca twego będzie służył przedemną aż na wieki; ale teraz mówi Pan: Nie będzieć to, gdyż ja te, którzy nie czczą, czcić będę, a którzy mną gardzą, będą wzgardzeni.
“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
31 Oto, dni przychodzą, a odetnę ramię twe, i ramię domu ojca twego, aby nie było starca w domu twoim;
Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
32 I oglądasz wielki ucisk przybytku Pańskiego, miasto szczęścia, które Pan dawał Izraelowi, i nie będzie starca w domu twoim po wszystkie dni.
nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
33 Wszakże męża nie wytracę z ciebie do końca od ołtarza mego, abym utrapił oczy twe, a boleścią ścisnął duszę twoję; a wszystko mnóstwo domu twego pomrze, dorosłszy lat męskich.
Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
34 A toć będzie na znak, co przyjdzie na dwóch synów twoich, Ofni i Fineesa; dnia jednego pomrą ci oba.
“‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
35 I wzbudzę sobie kapłana wiernego, który według serca mego, i według myśli mojej czynić będzie, i zbuduję mu dom trwały, a będzie służył przed pomazańcem moim po wszystkie dni.
Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
36 I stanie się, ktokolwiek pozostanie z domu twego, przyjdzie, aby mu się ukłonił za pieniądz srebrny i za sztukę chleba, mówiąc: Przypuść mię proszę do jednej cząstki kapłańskiej, aby jadł sztuczkę chleba.
Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”

< I Samuela 2 >