< I Królewska 15 >
1 Roku tedy ośmnastego królowania Jeroboama, syna Nabatowego, królował Abijam nad Judą.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Trzy lata królował w Jeruzalemie; a imię matki jego było Maacha, córka Abisalomowa.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Ten chodził we wszystkich grzechach ojca swego, które czynił przed nim; a nie było serce jego doskonałe przy Panu, Bogu swoim, jako serce Dawida, ojca jego.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 Wszakże dla Dawida dał mu Pan, Bóg jego, pochodnią w Jeruzalemie, wzbudziwszy syna jego po nim, a utwierdziwszy Jeruzalem,
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 Przeto, że czynił Dawid, co było dobrego w oczach Pańskich, a nie uchylał się od wszystkiego, co mu rozkazał, po wszystkie dni żywota swego, oprócz sprawy z Uryjaszem Hetejczykiem.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 I była wojna między Roboamem, i między Jeroboamem po wszystkie dni żywota jego.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 A insze sprawy Abijamowe, i wszystko, co czynił, azaż nie jest napisane w kronikach o królach Judzkich, jako i wojna między Abijamem i między Jeroboamem?
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 A gdy zasnął Abijam z ojcy swymi, pochowano go w mieście Dawidowem. I królował Aza, syn jego, miasto niego.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 A tak roku dwudziestego Jeroboama, króla Izraelskiego, królował Aza nad Judą.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 Czterdzieści lat i jeden królował w Jeruzalemie, a imię matki jego było Maacha, córka Abisalomowa.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 I czynił Aza, co dobrego było w oczach Pańskich, jako Dawid ojciec jego.
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 Albowiem wytracił Sodomczyki z ziemi, i wyrzucił wszystkie bałwany, których byli naczynili ojcowie jego.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Nadto i Maachę, matkę swoję, zrzucił z panowania, bo była sprawiła strasznego bałwana w gaju; przetoż porąbał Aza tego strasznego bałwana jej, i spalił u potoku Cedron.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 A chociaż wyżyny nie były skażone, jednak serce Azy było doskonałe przy Panu po wszystkie dni jego.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 I wniósł rzeczy poświęcone ojca swego, i rzeczy, które sam poświęcił, do domu Pańskiego, srebro, i złoto, i naczynia.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 I była wojna między Azą i między Baazą, królem Izraelskim, po wszystkie dni ich.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Albowiem Baaza, król Izraelski, wyciągnął przeciw Judzie, a zbudował Ramę, aby nie dopuścił wychodzić i wchodzić nikomu do Azy, króla Judzkiego.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Ale wziąwszy Aza wszystko srebro i złoto, które było pozostało w skarbiech domu Pańskiego, i w skarbiech domu królewskiego, dał je w ręce sługom swoim; i posłał je król Aza do Benadada, syna Tabremonowego, syna Hezyjonowego, króla Syryjskiego, który mieszkał w Damaszku, mówiąc:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 Przymierze jest między mną i między tobą, między ojcem moim i między ojcem twoim; otoć posyłam dary, srebro i złoto; idźże, wzrusz przymierze twoje z Baazą, królem Izraelskim, aby odciągnął odemnie.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 I usłuchał Benadad króla Azy; a posławszy hetmany z wojski, które miał przeciw miastom Izraelskim, zburzył Hijon i Dan i Abelbetmaachę, i wszystko Cynnerot, i wszystkę ziemię Neftalim.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Co gdy usłyszał Baaza, przestał budować Ramy, i mieszkał w Tersie.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Tedy król Aza zebrał wszystek lud Judzki, nikogo nie wyjmując; a pobrali kamienie z Ramy i drzewo jego, z którego budował Baaza: a zbudował z niego król Aza Gabaa Benjaminowe, i Masfa.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 A inne wszystkie sprawy Azy, i wszystka moc jego, i cokolwiek czynił, i miasta, które zbudował, azaż to nie jest napisane w kronikach o królach Judzkich? Ale czasu starości swej chorował na nogi swoje.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 I zasnął Aza z ojcy swymi, a pochowany jest z nimi w mieście Dawida, ojca swego. A Jozafat, syn jego, królował miasto niego.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Ale Nadab, syn Jeroboama, nastąpił na królestwo Izraelskie roku wtórego Azy, króla Judzkiego, i królował nad Izraelem dwa lata;
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 I czynił złe przed oczyma Pańskiemi, chodząc drogami ojca swego, i w grzechach jego, któremi do grzechu przywodził Izraela.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 I zbuntował się przeciw niemu Baaza, syn Ahyjasza, z domu Isaschar; a poraził go Baaza u Giebbeton, które było Filistyńskie; bo Nadab ze wszystkim Izraelem obległ był Giebbeton.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 I zabił go Baaza roku trzeciego Azy, króla Judzkiego, a sam królował miasto niego.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 I stało się, gdy począł królować, że wymordował wszystek dom Jeroboamowy; a nie zostawił żadnej duszy z narodu Jeroboamowego, aż je wytracił według słowa Pańskiego, które był opowiedział przez sługę swego Achyjasza Sylonitczyka;
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 A to dla grzechów Jeroboamowych, który grzeszył, i który do grzechu przywiódł Izraelczyki, i dla przestępstwa, którem wzruszył ku gniewu Pana, Boga Izraelskiego.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 A inne sprawy Nadabowe, i wszystko co czynił, azaż to nie jest napisane w kronikach królów Izraelskich?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 I była wojna między Azą, i między Baazą, królem Izraelskim, po wszystkie dni ich.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 Roku trzeciego Azy, króla Judzkiego, królował Baaza, syn Achyjasza, nad wszystkim Izraelem w Tersie przez dwadzieścia i cztery lat.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 I czynił złe przed Panem, chodząc drogami Jeroboamowemi, i w grzechu jego, którym do grzechu przywiódł Izraelity.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.