< I Królewska 14 >

1 Tegoż czasu rozniemógł się Abijas, syn Jeroboama.
Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa sana.
2 I rzekł Jeroboam do żony swej: Wstań teraz, a odmień się, aby nie poznano, żeś ty żoną Jeroboamową, a idź do Sylo; oto tam jest Achyjasz prorok, który mi powiedział, żem miał zostać królem nad tym ludem.
Yeroboamu akamwambia mke wake, “amka ujibadilishe, ili wasikutambue kuwa wewe ndiye mke wangu, na uende Shilo, kwa sababu nabii Ahiya yuko huko, yeye ndiye aliyeninea mimi kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
3 A wziąwszy z sobą dziesięcioro chleba, i placków, i faskę miodu, idź do niego; on ci oznajmi, co się stanie dziecięciu.
Uchukue mikate kumi, na kaki na mtungi wa asali, na uende kwa Ahiya. Naye atakuambia kitakachotokea kwa mtoto.”
4 I uczyniła tak żona Jeroboamowa, a wstawszy poszła do Sylo, i weszła do domu Achyjaszowego; ale Achyjasz nie mógł już widzieć, bo mu były zaszły oczy dla starości jego.
Mke wa Yeroboamu akafanya hivyo; akaenda Shilo mpaka kwenye nyumba ya Ahiya. Wakati huo Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa kuwa macho yake yalikuwa yameishiwa nguvu kwa sababu ya umri wake.
5 A Pan rzekł do Achyjasza: Oto żona Jeroboamowa wchodzi, aby się od ciebie czego wywiedziała o synu swym, przeto że choruje; ale tak a tak rzeczesz jej, a stanie się, gdy będzie wchodziła, zmyśli się być inszą.
BWANA akamwambia Ahiya, “Tazama mke wa Ahiya anakuja kutafuta kutaka ushauri toka kwako kuhusiana na mwanae, kwa kuwa ni mgonjwa. Mwambie hivi na hivi, kwa sababu atakapofika atajifanya kuwa ni mwanamke mwingine.”
6 Przetoż gdy usłyszał Achyjasz tupanie nóg jej, wchodzącej we drzwi, rzekł: Wnijdź żono Jeroboamowa; przecz się zmyślasz być inszą? Jam bowiem srogim posłem do ciebie.
Naye Ahiya aliposikia sauti za miguu yake alipokuwa akiukaribia mlango, akasema, “karibu, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine? Nimetumwa kwako nikiwa na habaari mbaya.
7 Idź, powiedz Jeroboamowi: Tak mówi Pan, Bóg Izraelski: Ponieważem cię wywyższył z pośrodku ludu, a postanowiłem cię książęciem nad ludem moim Izraelskim;
Nenda ukamwambia Yeroboamu kwamba BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Nilikuinua kutoka kati ya watu na kukufanya uwe kiongozi wa watu wangu Israeli.
8 I oderwałem królestwo od domu Dawidowego, a dałem je tobie, tyś jednak nie był jako sługa mój Dawid, który strzegł rozkazania mego, i który chodził za mną całem sercem swojem, to tylko czyniąc, co jest dobrego w oczach moich;
Niliugawa ufalme kutoka kwa Daudi na kukupa wewe, lakini bado hutaki kuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alizishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, na kufanya kilichokuwa sawa mbele ya macho yangu.
9 Aleś czynił złe nad wszystkie, którzy byli przed tobą; albowiem odszedłszy, poczyniłeś sobie bogi cudze, i lane, abyś mię pobudził do gniewu, a mnieś zarzucił w tył sobie:
Badala yake, umefanya maovu, zaidi ya wote waliokutangulia. Umetengeneza miungu mingine, na umetengeneza sanamu za kuyeyushwa ili kunikasirisha na kunitupa nyuma yako.
10 Przetoż oto Ja przywiodę złe na dom Jeroboamowy, i wytracę z Jeroboama aż do najmniejszego szczenięcia, więźnia, i opuszczonego w Izraelu, i wymiotę ostatki domu Jeroboamowego, jako wymiatają gnój, aż do czysta.
Kwa hiyo, tazama, Nitaleta majanga kwenye familia yako; Nitawatupilia mbali watoto wako wote wa kiume katika Israeli, kama ni mtumwa au ni huru, na nitaiondoa familia yako, kama mtu anayechoma mavi mpaka yaishe.
11 Tego, który z domu Jeroboamowego umrze w mieście, zjedzą psy, a który umrze na polu, zjedzą ptaki powietrzne, ponieważ Pan wyrzekł.
Yeyote ambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini ataliwa na mbwa, na yeyote atakayefia shamabani ataliwa na ndege wa angani, kwa kuwa Mimi BWANA, nimesema;
12 A ty wstawszy idź do domu twego a gdy wchodzić będziesz do miasta, tedy umrze dziecię.
Kwa hiyo inuka wewe mke wa Yeroboamu, na uende nyumbani kwako; na mguu wako utakapokanyaga mjini, yule mtoto wa Abiya atakufa.
13 I będzie go płakał wszystek Izrael, i pochowają go; bo ten sam z domu Jeroboamowego wnijdzie do grobu, przeto iż się znalazło o nim samym słowo dobre od Pana, Boga Izraelskiego w domu Jeroboamowym.
Na Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Ni yeye pekee katika familia ya Abiya atakayepelekwa makaburini, kwa sababu ni yeye pekee yake kutoka kwenye nyumba ya Abiya, ambaye BWANA, Mungu wa Israeli alimwona kuwa ni mwema.
14 Wszakże postanowi sobie Pan króla nad Izraelem, który wykorzeni dom Jeroboamowy dnia tego; a co mówię, wzbudzi? I owszem już wzbudził.
Pia BWANA atainua mfalme katika Israeli ambaye ataifutilia mbali familia ya Yeroboamu katika siku hiyo. Leo ndiyo siku hiyo, sasa hivi.
15 I uderzy Pan Izraela, i zachwieje nim, jako się chwieje trzcina na wodach, a wykorzeni Izraela z ziemi tej dobrej, którą dał ojcom ich, i rozproszy je za rzekę, przeto iż sobie poczynili gaje, wzruszając Pana ku gniewu.
Kwa kuwa BWANA ataishambulia Israeli kama vile majani yanavyotikiswa majini, na ataing'oa Israeli katika nchi hii njema ambayo aliwpa mababu. Atawatawanya hata ng'ambo ya Mto Frati, kwa sababu wamefanya nguzo za Ashera kumkasirisha BWANA.
16 A tak wyda Izraela dla grzechu Jeroboamowego, który grzeszył, i który do grzechu przywiódł Izraela.
Ataiacha Israeli kwa sababu ya dhambi ya Yeroboamu, dhambi ambazo ametenda, na kwa hizo ameifanya Israeli kufanya dhambi.
17 Tedy wstała żona Jeroboamowa, i poszła, a przyszła do Tersa; a gdy wstępowała na próg domu, umarło dziecię.
Kwa hiyo mke wa Yeroboamu akainuka na akaondoka na akaenda mpaka Tirza. Naye alipofika kizingitini kwa nyumba yake, yule mtoto akafa.
18 I pochowali je, a płakał go wszystek Izrael według słowa Pańskiego, które opowiedział przez sługę swego Achyjasza proroka.
Isareli wote wakamzika na kumwombolezea, kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA ambalo amelisema kupitia mtumishi wake nabii Ahiya.
19 A inne sprawy Jeroboamowe, jako walczył, i jako królował, oto spisane są w kronikach o królach Izraelskich.
Na kwa mambo mengine yanayOmhusu Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na jinsi alivyotawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
20 A dni, których królował Jeroboam, było dwadzieścia i dwa lat, i zasnął z ojcy swymi, a Nadab, syn jego, królował miasto niego.
Yeroboamu alitawala kwa miaka ishirini na mbili naye akalala na babu zake, na Nadabu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
21 Roboam też, syn Salomona, królował w Judzie. A było Roboamowi czterdzieści lat i jeden, gdy począł królować, a siedmnaście lat królował w mieście Jeruzalemie, które Pan obrał ze wszystkich pokoleń Izraelskich, aby tam przebywało imię jego. A imię matki jego było Naama, Ammonitka.
Sasa Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mtawala wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipokuwa mfalme, na akatawala kwa miaka kumi na saba kule Yerusalemu, mji ambao BWANA alikuwa ameuchagua kati ya makabila yote ya Israeli ili aweke jina lake kule. Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori.
22 I czynił Juda złe przed Panem, a wzruszyli go ku gniewu grzechami swemi, któremi grzeszyli nad wszystko, co czynili ojcowie ich.
Yuda ikafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA; wakamtia wivu kwa makosa yao, zaidi ya yote ambayo baba zao walikuwa wamefanya
23 Albowiem i oni pobudowali sobie wyżyny, i słupy, i gaje na każdym pagórku wysokim, i pod każdem drzewem zielonem.
Kwa kuwa walijijengea wenyewe mahali pa juu, nguzo za mawe, na nguzo za Ashera katika kila mahali pa juu na katika kila mti wenye majani mabichi.
24 Byli też i Sodomczycy w onej ziemi, sprawujący się według wszystkich obrzydliwości poganów, które wyrzucił Pan od obliczności synów Izraelskich.
Pia kulikuwepo na ukahaba wa kipagani katika nchi. Walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo BWANA alikuwa amewafukuza kutoka kwa watu wa Israeli.
25 I stało się roku piątego królowania Roboama, że wyciągnął Sesak, król Egipski, przeciw Jeruzalemowi.
Ilitokea wakati wa mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu wakati Shishaki akiwa mfalme wa Misri, akaja kinyume na Yerusalemu.
26 I pobrał skarby domu Pańskiego, i skarby domu królewskiego, wszystko to pobrał; wziął też wszystkie tarcze złote, które był sprawił Salomon;
Akaichukua hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya BWANA, na ile hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya Mfalme. Akachukua kila kitu; Pia alizichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.
27 Miasto których król Roboam sprawił tarcze miedziane, i poruczył je przełożonym nad piechotą, którzy strzegli drzwi domu królewskiego.
Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi, ambao walilinda malango ya kuingia kwa mfalme.
28 A gdy wchodził król do domu Pańskiego, brała je piechota, i zasię odnosiła do komor swoich.
Na ikawa kila mfalme alipoingia kwenye nyumba ya BWANA, wale walinzi walizibeba na baadaye walizirudisha katika chumba cha walinzi.
29 A inne sprawy Roboamowe, i wszystko co czynił, azaż nie są napisane w kronikach o królach Judzkich?
Lakini katika mambo mengine kuhusiana na Rehoboamu, na yote yale aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
30 I była wojna między Roboamem i między Jeroboamem po wszystkie dni.
Kulikuwa na mapigano yasiyokoma kati ya nyumba ya Rehoboamu na nyumba ya Yeroboamu.
31 I zasnął Roboam z ojcy swymi, a pochowany jest z nimi w mieście Dawidowem; a imię matki jego było Naama, Ammonitka. I królował Abijam, syn jego, miasto niego.
Kwa hiyo Rehoboamu akalala na mababu zake naye akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori. Abiya mwanawe akawa mfalme mahali pake

< I Królewska 14 >