< Tituj 1 >
1 PAULUJ ladun Kot o wanporon en Iejuj Krijtuj amen, duen pojon en me pilipildar en Kot akan o duen erpit en melel on pai ren Kot;
Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
2 O kaporoporeki maur joutuk, me Kot jo likam inaukidar mon tapin kaua. (aiōnios )
ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati, (aiōnios )
3 A ni a anjau a kotin kajanjaledar a majan ki padak, me ko on ia, duen kujoned en Kot atail Jaunkamaur.
na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
4 On Tituj nai jeri melel ni ata pojon ta ieu: Mak o popol jan ren Kot Jam o Krijtuj Iejuj atail Jaunkamaur en mi re om!
Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
5 let karepen ai kamodan uk edi Kreta, pwe koe en kapwaiada, me kaikenta wiauier o kajapwilada jaunkoa kan ni kanim karoj, due i kakaliki on uk.
Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
6 Jaunkoa amen en indand mau, o warok en li ta men, o me na jeri kan pojonla, o jo kaindandeki, me re kamom de jopeik.
mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
7 Pwe pijop en punla, duen jaunkoa en Kot amen, der katiwo, der purianikom, der kamom wain, der pamara, der norok moni.
Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
8 A ren apwali men kairu o pok on me mau, o kanonama, o pun, o jaraui, o makelekel.
Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
9 Kolekoleta majan, me udan pun o koiok on padak, pwen kak on panauiki padak en kamaur o kapun on me katiwo kan.
Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
10 Pwe ir me toto me malaun o kapei lokaia o me kaweid japun, iet eten, kijan men jirkomjaij.
Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
11 Me mau on au ar en pinapinla, pwe re kin kawukila toun im toto, o me kin padapadaki, me jota mau, pweki moni.
Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
12 Amen irail, pein arail jaukop amen inda: Men Kreta me kalap likam, man jued o laualo, nain mana.
Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: “Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!”
13 Kadede pot et me melel. Ari, i me koe en kapun kelail on irail, pwe ren kelailada ni pojon.
Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
14 O ren der injenoki en Juj oko ar kajoi mal akan o kujoned en aramaj akan, me muei jan melel.
Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
15 Karoj me kon on makelekel akan, a jota me kon on me jamin o jo pojon akan, pwe arail lamelame o pil injen arail me jamin.
Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
16 Re kin inda, me re aja Kot, a ni ar wiawia kan re kin ponjaja i. Irail meid jued, o jopeik, o jo koiok on jon en wiawia mau karoj.
Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.