< Psalms 78 >
1 KOMAIL nai aramaj akan, ron ai kujoned; komail kapaike don jalon omail padak en au ai!
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I pan ki pajan au ai, pwen padak, o pan kida kajoi en maj o,
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Me kitail ronadar o ajaer, o jam atail kajoi on kitail er,
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Pwe kitail ender karirila jan kadaudok arail, me pan pwarado mur, o kaparokki wau en leowa, o a manaman o a dodok kapuriamui kan.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Pwe a kotin kauada men kataman eu ren Iakop, o kotikida kapun eu ren men Ijrael, me u kotin kakaliki on jam atail akan, pwe ren ujelan nair jeri kan,
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 Pwe di en mur en aja due, o jeri ko, me pan ipwidi; o ni ar kokoda, ren pil kajoi on nair jeri kan
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 Pwe irail en kaporoporeki Kot, o ren der monokela en Kot a wiwia kan, o ren kapwaiada a kujoned akan.
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 O ren der dueta jam arail akan, me kainok kanudi o katiwo eu, me monion arail jota teneten, o nen arail jota melel on Kot.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Dueta kainok Epraim, me wa tatan mauin, ap purela jan nan pei.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Irail jota dadaurata inau en Kot, o re jota men weweideki duen a kujoned akan.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 O re monokelar a wiawia kan o a manaman akan, me a kotin kajaljale on irail er.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 A kotin wiadar manaman akai janjal mon jam arail akan nan Akipten, nan jap Joan.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 A kotin palan pajan madau o kotin mueid on ir, en kotela, o wiadar pil dueta kel takai eu.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 A kotin kalua kin irail tapik ni ran o, o ni pon umpul en kijiniai.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 A kotin palan pajan paip nan jap tan o kanim pile kin irail pil toto.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 O a kotin kapkapwile wei pilap kai jan nan paip, pwe ren pwile wei dueta pilap laud akan.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Ari jo, re dadaurata ni arail didi on I, o re kaonioni me Lapalap o nan jap tan.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 O re kajonejon Kot nan monion arail, ni ar inon ion kan arail mana.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 O re palian Kot ni ar inda: Melel Kot pan kak wiada tepel eu nan jap tan?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Kilan, a poki paip o, pe pil en pwarado o pilap akan pwilepwile wei, a iaduen, a pan kak kida prot o uduk on na aramaj akan?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Ieowa lao manier mepukat, ap kotin onionadar, o kijiniai wiauier ren Iakop, o onion lel on Ijrael,
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Pweki ar jo kamelele Kot, o jota kaporoporeki a jauaj.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 A ap kotin majani on tapok en poa kan, o ritinida wanim on lan akan.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 O kotin kamoredi on ir mana, pwe ren mana, o a kotiki on ir prot en lan.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Irail kanalar prot en tounlan kan; a kotin kadar on ir kijin mana toto.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 A kotin kapwaredar pan lan an en maj en lan, o ni a manaman a kotin kamokidada an en pali air.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 O a kotin kamoredi on ir uduk dueta pwel par, o manpir dueta pik en oror.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 O a kotin kapup irail di waja karoj, me irail kaujon ia.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Rap manamana o medilar kaualap, o a kotin mueid on ir ar inon.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 A ni ar kapwaiadar ar inon, o ni ar manamana.
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 Onion en Kot ap lel on irail er, o kamelar ol lapalap re’rail, o kotin wokiedi mana kap en Ijrael kajampwal akan.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 A re kalaudelar arail dip, o re jota kamelele a manaman akan.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 I me a kotin mueidoki ren mela, re jota paida, o ar apwal akan me toto arain ar maur.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Ni a kotin kame irail la, rap idok i, o wukila, o rapaki Kot.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 O re tamandar, me Kot kele parail o Kot lapalap ar jaundor.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 O re lik janjal mau on i ni au arail o re likam on i ni lo ar.
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 A monion arail jota teneten on i, o re jota dadaurata melel a inau.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Ari jo, a kotin kalanan on ir, o kotin makeki on ir dip arail, o jota kame irail la, o katukiedi a onion pan pak toto, o jota onioni melel.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Pwe a kotin kupura, me irail pali uduk, dueta kijinian, me pir wei o jolar puredo.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Pan pak toto re kanudi on i nan jap tan, o kakupur juedi i nan mal.
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Irail pur on anjau karoj kajonejon Kot, o re akapuni on me Jaraui ren men Ijrael.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Re jolar tamanda lim a manaman, me dore ir ala jan ar imwintiti kan ni ran o.
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 Duen a kotin wiadar a manaman akan nan Akipten o a dodok kapuriamui nan Joan.
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 A kotin kawuki on nta ar pil akan, rap jolar kak nima jan ar pilap akan.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Ni a kotin kapwaredar man jued akan nan pun arail, me kan ir ala, o proj akan, me kawe ir ala.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 A kotiki on muedi ar tuka kan, o ar wantuka on man jiek.
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 A kotin kawekilar akel ar wain o tuka kan ki akel tikitik.
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 A kotin kamekila ar man akel akan o ar pwin man akan liol.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 A kotin onion melel o porone won ir tounlan jued kai, o mueid on ir, ren linaranar, o morjued, o kainjenjued.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 A kotin kaonopa dan onion al apot, o jota dorelar maur arail jan mela, o kotin mueid on kilitop ni maur arail.
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 A kotin kamelar mejeni karoj nan Akipten, mejeni en ar kelail nan im en Am akan.
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 A kotin kaluala japwilim a kan dueta pwin jip eu nan jap tan.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 A kotin kalua irail ni pun, pwe ren der majak meakot, a madau kadupaledi ar imwintiti kan.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 A kotin wa ir ala lel ni irair en jap jaraui, lel nana wet, me lim a pali maun kileledier.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 O kotin pakipaki men liki kan mo’rail, o kotin nek on ir jap arail, pwen jojoki, o a kotiki on kainok en Ijrael akan, en kaukaujon nan im arail.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 A re jonejon? o kaonion Kot lapalap, o jota peiki on i, o jota duki on a majan akan.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 O re muei jan o mamaleki meakaroj, dueta jam arail akan, o re jota teneten, dueta kajik katieu luet eu.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 O re kaonion i ni ar kaudok pon dol akan, o re kupur juedeki i ki arail dikedik en ani kan.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 A Kot lao kotin mani mepukat, ap kotin onionada o kajapok ir ala melel.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 A kotin muei jan tanpaj a nan Jilo, im pwal o, waja a kotikot ia ren aramaj akan.
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 A kotiki wei japwilim akan nan imaten, o a linan nan pa en imwintiti kan.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 A kotiki wei japwilim a aramaj akan ni kodlaj, o kotin onioni japwilim a jojo.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Kijiniai kanala ar manakap akan, o ar peinekap akan jolar kak papaud.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Arail jamero kan mekilar kodlaj, a jolar li odi kan, me kin maiei.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Ieowa ap kotin opala waja dueta amen me mairelar, dueta ol komad amen kin nijinij ni a kan wain.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 A kotin kaloedier a imwintiti kan o kanamenok ir ala kokolata.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 A kotin kajelar im en Iojep, o jota piladar kainok en Epraim.
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 Pwe a kotin piladar kainok en Iuda, kol Jion, me a koti kupura.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 O a kotin kauadar tanpaj a im jaraui waja ileile, dueta jappa me pan teneten ea kokolata.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Ap kotin piladar japwilim a ladu Dawid, o a kotin ale i jan nan deun jip akan.
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 A kotin kalua i jan ren jip en kadidi kan, pwen kamana japwilim a kainok en Iakop o a jojo men Ijrael.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 O a kotin apapwali ir ni tiak en monion melel o pun, o kakaun irail ada ni koiok en lim a kan.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.