< Wiawia 8 >
1 A JAULUJ pil peren kida a kamela. A ni ran ota anjaun kamekam en momodijou en Ierujalem tapida; karoj ap muei pajan nan jap en Iudaao Jamaria, wanporon akan me jo.
Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
2 A ol lelapok kai jarepedi Jtepanuj o maieiki i kaualap.
Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
3 A Jauluj me kamueit pajan momodijou o kuli on im karoj, wala ol o li karoj, kajedi on irail nan imaten.
Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
4 A irail me muei pajaner, kakan jili padapadak duen majan o.
Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
5 Pilipuj ap kotilan kanim en Jamaria eu o padaki on irail duen Krijtuj.
Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
6 A aramaj akan wiaki eu peiki on meakan, me Pilipuj padaki on irail. Re roneron i o kilan kilel akan me a wiadar.
Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
7 Pwe nen jaut keredi jan ren me toto ni ar weriwer laud. O me kokon madak o na danidan toto me kelailadar.
Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
8 O peren me lapalap nan kanim o.
Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
9 A ol amen ad a Jimon, me kin wun ani maj o, kotokotaue men Jamaria, me inda duen pein i, me i me lapalap.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
10 A irail karoj peiki on i, me tikitik o me lapalap akan katitiki: Men et iei manaman en Kot me lapalap.
Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, “Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa.”
11 A re kin peiki on i, pweki a kin kotokotaue irail jan maj kokodo.
Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
12 A re lao kamelele Pilipuj, me padaki duen ronamau en wein Kot o duen mar en Iejuj Krijtuj, rap paptaijela, ol o li akan.
Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
13 Jimon pil ian pojonlar, I lao paptaijelar, ap waroki on Pilipuj. A lao udial kilel o manaman akan, me wiauier, ap puriamuiki.
Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
14 Wanporon akan me kotikot Ierujalem lao mani, me Jamaria ian duki on majan en Kot, rap poronelan irail Petruj o Ioanej.
Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
15 Ira lao kotido, ap kapakapa kin irail, pwe re en tunole Nen jaraui.
Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
16 Pwe a jaikenta moredi on amen irail. Re paptaijelar eta ni mar en Kaun Iejuj.
maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
17 Ira ari kotiki on po’rail lim ar akan, irail ap aleer Nen jaraui.
Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
18 Jimon lao kilaner, me Nen jaraui kokido en wanporon oko ara pwil po’rail lim ar akan, ap men ki on ira kijin moni.
Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
19 Indada: Koma pil kotiki don ia manaman wet, pwe ma I pan pwiI pon amen pa i kat, i en ale Nen jaraui.
“Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu.”
20 A Petruj majani on i: Noum moni en ian uk lokidokila! pweki om kiki on, me mana en Kot kokido moni.
Lakini Petro akamjibu, “Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
21 Nan jota pwaij om de om tunol ni dodok wet, pwe monion om jota inen mon Kot.
Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
22 Ari, kalukila om jued wet, poeki ren Kaun o, ma a jota pan kotin makeki lamelam jued nan monion om.
Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
23 Pwe i kilaner, me koe me dir en edi katik o teniten ni me japun.
Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!”
24 Jimon ap japen indada: Koma kotin kapakapa kin ia ren Kaun o, pwe mepukat, me koma majani on ia, ender pwai don ia.
Simoni akajibu, “Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema.”
25 A ira lao katitiki o kotikida majan en Kaun o, ap purelan Ierujalem, o padak jili ronamau nan kijinkanim en Jamaria toto.
Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
26 A tounlan en Kaun o majani on Pilipuj: Uda kola pali air pon al o, me kodi jan Ierujalem, ko on Kaja me tan!
Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani.)
27 I ari uda japalewei. A kilan, ol en Etiopia, jaumaj manaman en Kandaje, li nanmarki en Etiojiia, me kokoaki a dipijou karoj, mo kotido, pwen kaudok nan Ierujalem.
Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
28 A ni a purela jap we, a kotikot pon dakepa o dondoropwe jaukop Iejaia.
Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
29 Nen o ap kotin majani on Pilipuj: Kai on o ianala dakepa!
Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”
30 Pilipuj ap tana won i, ap ronadar a dondoropwe jaukop Iejaia majani: Komui weweki, me komui doropwe?
Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”
31 I ari majani: Pala i pan aja, ma jota, me pan kawewe on ia? I ari poeki ren Pilipuj en kereda mondi re a.
Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
32 A iet waja nan kijin likau o me a wadoker: Duen jip amen, me pakara wei, pwen kamela, o duen jippul, me kin nenenlata pan me kote jan wun a, iduen a jota kotin dauaja pajan jilan i.
Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: “Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
33 A ni a karakarak a jolar pakadeikadar. A ij me pan kak kaweweda duen jau i kan? Pwe a ieiaj wijike janer jappa.
Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”
34 Jaumaj ap japen Pilipuj majani: I men poeki re omui, ij me jaukop katitiki met? Duen pein i de duen amen?
Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”
35 Pilipuj ap kotiki pajan au a, padaki on i ronamau en lejuj, tapiada nan kijin likau wet.
Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
36 A ni ara kokowei, ira lel on pil apot, a jaumaj o majani: Kilan pil o, da me karompa, me I jota paptaij ki?
Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, “Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?”
Filipo akasema, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Naye akajibu, “Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”
38 I ap majani dakepa en udi. Ira karoj ap kodi on pil o, Pilipuj o jaumaj o; i ari paptaij i.
Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
39 Ira lao kodado jan nan pil o, Nen en Kaun o ap pokada jan Pilipuj. Jaumaj o ap jolar kilan i. I ari daulul kokowei popol.
Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
40 Pilipuj ap diarokadar Ajdod; a dadaulular, padak jili ronamau nan kanim karoj lao a lele don Jajarea.
Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.