< Wiawia 27 >

1 A LAO kileledier, me je pan jerokelan Italien, re kajilaki Pauluj, o akai me jalidi, kaun en jaunpei amen, me ad a Iuliuj, kijan pwin en Aukujtuj.
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 Kit ari kereda pon jop en Adramitien pot, me pan jupi on kanim en Ajien akan, me mi pon oror, ap tan wei. Ari, Arijtarkuj, men Majetonien amen jan Tejalonik ian kit.
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 Mandan ran o je leler Jidon. A Iuliuj me kadek on Pauluj, ap mueid on i, en kotila ren kompokepa ko pwen kajarloleit.
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 Kit ari majelar jan waja o, ap tanatan pananen Jipern, aki an me u don kit.
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 Kit tanatan kotela lepen jed en Jilijia o Pampilien, je ap lel on Mira en Lijia,
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 I waja kaun en jaunpei o diarada jop en Alekjandrien pot, me pan majelan Italien, i ari kajau on kit poa.
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 A kit pwapwand kokola, pon toto meid apwal on kit lel on Kniduj, pwe an me kawela; kit ari tanatan pananen Kreta, tan won Jalmone.
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 A meid apwal at dauli waja o; kit ari lel on jap eu, me ad a Kapitau mau koren ion kanim Lajaa.
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 A anjau lao daulier o a apwalar on jailok jili, aki ran en kaijejol daulier, Pauluj ap kotin panaui o
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 Majani on irail: Ol oko, i ajaer me jailok wet pan juedela a pan apwal kaualap, kaidin on audepan jop o jop eta, pwe pil on maur atail.
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 A kaun en jaunpei o liki jaunilil o jaumaj en jop o jan majan en Pauluj.
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 A kapitau me jota non mau on jop en mimieta ni anjaun kapau. Koren ion karoj ari men jamala jan waja o, o re jon, ma re jota kak on lel Ponikj, pwen mimita waja o ni anjaun kapau, I kapitau en Kreta eu, me mi ni pali air o pali apan.
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 A an lao udo jan pali air, re ap kiki on, me re pan pwaida, ap apiada paipun ko tanala liman Kreta.
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 A madan melimel udo jan Kreta, me ad a alepip en kijinian.
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 A an lao kapeila jop o, o jop jolar kak on, kit ap nenenla o peila.
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 Ni at tanala pananen dake tikitik eu, me ad a Klauda, me tar kij, a je jolar kak on koledi pot o.
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 Irail apiada i, pwen kak piradi on ni jop o, ap lilidi, pwe re majak re de jerada nan Jirte, ap punipunidok jili.
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 Kit lao punipunidok jili kaualap, manda ap kamararadar jop o.
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 A ni ran kajilu irail kaje kila pein pa arail kapwa en jop o.
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 Kadekadeo ran totola jota katipin o jota uju, o melimel kalaimun u don kit, ap jolar at kaporopor en pitila.
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 A kit lao kaijejol warailar, Pauluj ap pwarada nan pun arail majani: Ol oko mak eta, komail en peiki on ia er o jo majel jan Kreta, pwe kitail ender lel don kaupatail.
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 A met i panaui komail, en kaporopor mau, pwe jota me pan mela, jop eta me pan ola.
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 Pwe tounlan en Kot, me japwilim a nai, o me i kin papa, me kotida imp ai pon,
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 Kotin majani: Pauluj, koe der majak, koe pan wijike won ren Jija. A kilan, Kot me kotiki on uk er karoj me ian uk.
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 Ari ol oko komail kaporopor mau, pwe i kin pojon Kot, me a majan pan pwaida.
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 A kitail pan jerada nin dake eu.
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 A lao pon naul pa pon lar, kit peipei jili nan jed Adria. Ni ailep en pon toun jop o kajauiada, me je koren ion jap eu.
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 A irail lao kajedi men jon, re ap diaradar, me nap rieijok, o re kaila ekij waja o kajedi men jon, re ap diaradar, me nap eijoklimau.
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 A re majak, je de jerada pon mut, rap kajedi paipon paieu jan in murin jop, ap mauki en ran pajan,
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 A toun jop o lao men pitila jan nin jop o, o re apiedi pot apot nan jed, dene re pan kajedi paipon kai ni mon jop o,
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 Pauluj ap majani on kaun o jounpei kan: Ma mepukat jota pan mimieta pon jop o, komail jota pan kak dorela.
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 Jaunpei kan ap leke jan pot o kajela o ari.
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 A lao pan ran pajan, Pauluj ap panaui irail, ren mana, majani: Nan a pon naul pa pon lar, me komail kin auiaui o kaijejol o jota mana.
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 Nai ari panauki komail, en mana, pwe i me komail pil pan piti kila. Pwe jota pit en mon pit pan pupedi jan amen komail.
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 A lao majanier met, ap ale prot, danke Kot mo’rail karoj. I lao pilitiki pajan ap jak.
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 Irail karoj ap kaporopor maular o pil mana.
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 A kit karoj me mi nan jop o, me riepuki ijiakan wonumen.
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 Irail lao medier, rap kamaradar jop o, kajedi on nan madau korn.
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 A lao waja ran pajan, re jaja jap o, A re diaradar kapitau me mad mia; i waja re lamedar en walan jop ia, ma re pan kak on.
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 Irail lao leke jan paipon ko, rap kaje ir ala nan madau, o lapwada padil akan, o apiadar p jerok en moa ni an o, ap tanala ni oror.
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 Irail lao lel on mad eu, jop o jerada o jolar mokid. Mon jop o tenela, a muri ola nan iluk kan.
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 Jaunpei ko ap men kamela me jalidi kan, pwe amen de pan pitila jan.
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 A kaun en jaunpei o men dorela Pauluj, ap jota mueid on irail me re men wia o majani: Me aja pampap, en lujedi on nan madau pap won jap o.
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 A me tei kan pon tenap de kijan jop o. A ap pwaida, me irail karoj dorelar o lel on jap o.
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.

< Wiawia 27 >