< Timoteuj I 4 >

1 A NEN me kotin kokop melel, ni imwin kaua akai pan pupe wei jan pojon, ap id wuki on nen widin o padak en tewil akan,
Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
2 Me kin janjale mau ki liki, ap likilikam o injen arail kakaluakalar ki kijin mata karakar.
Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
3 Re kin inapwiedi kapapaud, o dene ren liki jan jon en mana, me Kot kotin wiadan irail, me danke, o pojon, o dedekila melel
Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
4 Pwe audepa karoj, en Kot me mau, o jota meakot me mal, ma aramaj pan tunole ap danke.
Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
5 Pwe a pan kajaraui kila majan Kot o kapakap.
kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
6 Ma koe pan padaki on ri atail akan, koe ap pan papa en Krijtuj Ieiuj mau amen, me kin keleki majan en pojon o padak mau, me koe dadaureta mau lel met.
Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
7 Ma koe pan kan kajoi likam en li laud akai o kaianeki pein uk me kon on Kot.
Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
8 Pwe kaiane kin uk pali war, a jota non katopa, a meid mau paieki Kot ni meakoaroj, pwe iei kaporopor en maur et o pil maur kokodo
Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
9 Nan melel kojoi pot et o a war on kitail en apwaliea.
Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
10 Pwe iet me je kin dodok on o kalokolokki, at kaporoporeki Kot ieiaj, me Jaunkamour en aramaj akan karoj, a maj on irail me pojon.
Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
11 Mepukat koe en katitiki o kaukaweweki.
Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
12 Jota amen me pan mamaleki om manakap, a wiala men kaalemoni on jaulan kan, ni om lokaia o wiawia kan, o limpok, o pojon, o makelekel.
Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
13 O nantion wadok, o panaui, o padak lao i pan pwar wei.
Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
14 Der kajamal la pai en mak o, me koe aleer ki deideikop o ni en jaunkoa kan ar pwil pa ar po om.
Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
15 Koe en podidi o jopijokki mepukat, pwe om lolekon en janjal on karoj.
Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
16 Kalaka pein uk o padak o, tenedi on jon pukat, pwe ma koe pan wiada due, koe ap pan dorela pein uk o pil, me kin ron uk.
Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.

< Timoteuj I 4 >