< Ioanej I 2 >
1 JAMA ko, mepukat i intin won komail, pwe komail de wia dip, a ma amen wia dip, jauaja patail mia ren Jam, Iejuj Krijtuj, me pun.
Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.
2 Iei me tom en dip atail, a kaidin atail ta, pwe pil en toun jappa karoj.
Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.
3 I me kitail dedeki, me kitail ajaer i, ma kitail kapwaiada kujoned akan.
Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.
4 Me inda: I aja i, ap jota kapwaiada a kujoned akan, i me likam amen, melel jota mi re a.
Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.
5 A me kapwaiada a majan, i me limpok en Kot unjokelar re a, i me kitail ajaki, me kitail udan japwilim a.
Lakini mtu yeyote anayeshika neno la Mungu, huyo ndiye aliye na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hivi ndivyo tunavyoweza kuwa na hakika kwamba tunaungana naye:
6 Me kin inda: I potopot re a, mak eta, i en weweid wei dueta a kotin weweidier.
mtu yeyote anayesema kwamba ameungana na Mungu, anapaswa kuishi kama alivyoishi Yesu Kristo.
7 Kompok kan, kaidin kujoned kap eu, me i intin won komail, a kujoned en maj o, me mi re omail jan ni tapi o. Kujoned en maj, iei majan o, me komail roner.
Wapenzi wangu, amri hii ninayowaandikieni si amri mpya; ni amri ileile ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Amri hiyo ya zamani ni ule ujumbe mliousikia.
8 Pil eu kujoned kap, me i intin won komail, me melel re a o re omail, pwe rotorot mur tikitikla, a marain melel ap dakadar.
Hata hivyo, amri hii ninayowaandikieni ni amri mpya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu pia. Maana giza linatoweka, na mwanga wa ukweli umekwisha anza kuangaza.
9 Me inda, me a mi ni marain, ap kailon kin ri a, nan a mimieta ni rotorot lel met.
Yeyote asemaye kwamba yumo katika mwanga, lakini anamchukia ndugu yake, mtu huyo bado yumo gizani.
10 Me kin pok on ri a, pan mimieta ni marain, ap jolar men kamakar mi re a.
Yeyote ampendaye ndugu yake, yuko katika mwanga, na hamna chochote ndani yake kiwezacho kumkwaza mtu mwingine.
11 A me kin tataki ri a, ni rotorot, o weweid ni rotorot, ap kin jaja, waja a kin ko on ia, pwe rotorot karotonala maj a kan.
Lakini anayemchukia ndugu yake, yumo gizani; anatembea gizani, na hajui anakokwenda, maana giza limempofusha.
12 I intin won komail, jama ko, pwe dip omail lapwadar ki mar a.
Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.
13 I intin won komail, jam atail, pwe komail aja i, me kotikot eta jan ni tapi o. I intin won komail manakap akan, pwe komail kaloedier me jued o. I intin won komail er, jama ko, pwe komail ajaer Jam.
Nawaandikieni ninyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo, Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.
14 I intin won komail er, jam akan, pwe komail aja i, me kotikot jan ni tapi o. I intin won komail er, manakap akan, pwe komail me kelail, o majan en Kot en mimieta re omail, o komail kaloedier me jued o.
Nawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mnamjua Baba. Nawaandikieni ninyi kina baba, kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo. Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu; neno la Mungu limo ndani yenu na mmemshinda yule Mwovu.
15 Der pok on jappa, de dipijou mimi jappa. Ma amen pok on jappa, limpok en Jam me jota mi re a.
Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
16 Pwe meakaroj mi jappa, inon en ni uduk, o inon en ni maj oko, o linan mal en maur, a jota lapida jan ren Jam, a jan ni jappa.
Vitu vyote vya ulimwengu-tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali-vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.
17 A jappa pan jorola o a me jued akan, a me wia kupur en Kot, pan mimieta kokolata. (aiōn )
Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele. (aiōn )
18 Jama ko, metet imwin auer o, o duen omail roner, me krijtuj likam pan pwarado, nan anjau wet krijtuj likam me toto, me pwaradar, i me kitail ajaki, met imwin auer leler.
Watoto, mwisho u karibu! Mlikwisha sikia kwamba adui wa Kristo anakuja, na sasa adui wengi wa Kristo wamekwisha fika, na hivyo twajua kwamba mwisho u karibu.
19 Irail me kola jan kitail, a kaidin kij atail, pwe ma irail kij atail, re pan mimieta re atail. A irail kola jan kitail, pwen janjal, me kaidin irail karoj kij atail.
Watu hao wametokea kati yetu lakini hawakuwa kweli wa kwetu na ndiyo maana walituacha; Kama wangalikuwa wa kwetu, wangalibaki nasi. Lakini waliondoka, wakaenda zao, kusudi ionekane wazi kwamba hawakuwa kamwe wa kwetu.
20 A komail keidier ren me jaraui, o komail ajaer meakaroj.
Ninyi, lakini, mlipata kumiminiwa Roho Mtakatifu na Kristo, na hivyo mnaujua ukweli.
21 I jota intin won komail er, dene jota aja duen melel, a pwe komail aja, o likam jo tapida jan ni melel.
Basi, nawaandikieni, si kwa kuwa hamuujui ukweli, bali kwa sababu mnaujua; na pia mnajua kwamba uongo wowote haupatikani katika ukweli.
22 Ij me likam amen? Kaidin i, me kamamada me Iejuj udan Krijtuj. I me krijtuj likam, me kamama kida Jam o Na.
Mwongo ni nani? Ni yule anayekana kwamba Yesu ni Masiha. Mtu wa namna hiyo ni adui wa Kristo—anamkana Baba na Mwana.
23 Amen amen, me kamam kida Na, nan Jam pil jota mi re a, a me ponaja Na, i me pil japwilim en Jam.
Maana yeyote anayemkana Mwana, anamkana pia Baba; na yeyote anayemkubali Mwana, anampata Baba pia.
24 Me komail roner jan ni tapi o, en potopoteta re omail. Ma a pan mimi re omail, me komail roner jan ni tapi o, komail ap pil pan potopot ren Na o Jam.
Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.
25 A iet inau o, me a kotin inauki on kitail er: Maur joutuk. (aiōnios )
Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele. (aiōnios )
26 Mepukat me i intin won komail er duen irail, me kajapune komail.
Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha ninyi.
27 A omail kei, me komail aleer re a, pan mimieta re omail. Komail ap jolar mau on, amen en padaki on komail. A duen kei wet kin padaki on komail meakaroj, iduen me melel, a kaidin likam pot, o duen a padaki on komail er, iduen komail en dadaurata.
Lakini, kwa upande wenu ninyi, Kristo aliwamiminieni Roho wake. Na kama akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana Roho wake anawafundisheni kila kitu na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.
28 Ari jama ko, podidi on i, pwe ni a pan kotin pwarado, kitail en aima, a jo namenok mo a, ni a kotin pwarado.
Naam, watoto, kaeni ndani yake kusudi wakati atakapotokea tuwe hodari bila kuwa na sababu ya kujificha kwa aibu Siku ya kuja kwake.
29 Ma komail aja, me i me pun, komail en pil aja, meamen, me wia me pun, me ipwi jan i er.
Mnajua kwamba Kristo ni mwadilifu kabisa; basi, mnapaswa kujua pia kwamba kila mtu atendaye mambo adili ni mtoto wa Mungu.