< Men Korint I 15 >
1 RI ai kan i men kataman kin komail ronamau, me i padaki on komail er, me komail pil aleer o pil tinain kidar.
Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2 O me komail pil dore kila, ma komail pan dadaurata majan o, me i padaki on komail er, ma komail jo pojon mal.
Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3 Pwe i ujaki on komail er, me i pil aleer duen Krijtuj, me kamata kilar dip atail akan duen kijin likau kan.
Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4 O me a jaredier o kaiajadar ni kajilu en ran duen kijin likau kan,
kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5 O me a pwara won Kepaj, ap on irail me ekriamen ko,
kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6 Ap kotin pwara won jaulan limepuki jama ni anjau takij; kij arail me toto mimieta lei met, a akai mairedier.
Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7 Murin met a kotin pwara won Iakopuj, ap on wanporon akan karoj.
Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8 A ikmuri a kotin pwara don ia mon ai ip japal,
Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9 Pwe pokindidi ren wanporon akan nai, me jota war on kaindinda wanporon amen, pweki ai pei on momodijou en Kot.
Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10 A mak en Kot, me i wanoron kilar. A kaidin mak mal eu on ia, pwe i dodok laud jan irail karoj, ari kaidik nai, pwe mak en Kot, me mi re i.
Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11 Ari, ma nai de irail, pwe iduen at padaki wei, o iduen komail pojonlar.
Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12 A ma i aude pan at padak, me Krijtuj iajadar jan ren me melar akan, a da me akai re omail kin inda, dene me melar akan jolar pan mauredar?
Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13 A ma me melar akan jota pan maureda, nan Krijtuj pil jota iajadar.
Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14 O ma Krijtuj jota iajadar, at padak me mal, o omail pojon pil me mal.
na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15 O kitail pil pan diarokada, me je jaunkadede likam ren Kot, aki at kadededar, me Kot kotin kaiajadar Krijtuj, me a jo kaiajadar, ma me melar akan jota pan kamaureda.
Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16 Pwe ma me melar akan jota pan kamaureda, nan Krijtuj pil jo kaiajadar.
Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17 A ma Krijtuj jo kaiajadar, omail pojon me mal, o komail mimieta ni dip omail.
Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18 Iduen pil irail, me melar ren Krijtuj akan, lokidokila.
Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19 A ma kitail kaporoporeki Krijtuj nan maur et eta, nan kitail me jued jan aramaj akan karoj.
Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20 A melel, Krijtuj kaiajadar jan ren me melar akan, ap wiala mejeni nan pun en ir me mamair akan.
Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21 Pwe mela tapi jan aramaj ta men, iduen maureda jan ren me melar akan tapi jan aramaj ta men.
Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22 Pwe duen karoj me mela ki Adam, nan iduen karoj pan kamaurela ren Krijtuj,
Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23 A amen amen ni kakairokdo: Krijtuj maj ap me japwilim en Krijtuj, ni a pan kotin pwarado;
Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24 A murin mepukat pan imwi, a lao kotiki on Kot o Jam a wei, a lao kaloedier kaun akan karoj, o me poe kan, o manaman akan.
Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25 Pwe a pan kotin kaunda, lao a imwintiti karoj lodi on pan aluwilu a kan.
Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26 A ikmurin imwintiti iei mela.
Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27 Pwe a kotin mueid on meakaroj pan aluwilu a. Ari ni a kotin majanier me karoj lodier a janjaledar, me i jota ian me kotin kaloedi on i meakaroj.
Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28 A meakaroj lao lodi on i, Na ap pil pan upan i, me kotin kaloedi on i meakaroj, pwe Kot en kotin poedi meakan karujia.
Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29 A ma me melar akan jolar pan kamaureda, da me irail en wia, me kin paptaijeki on me melar akan? Menda re paptaijeki on irail?
Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30 O menda kit kin kalokolok anjau karoj?
Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31 Pwe ran karoj i kin mela, pweki kapin pa i, me i aleer ren Krijtuj Iejui atail Kaun.
Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32 A ma i pei on man laualo nan Epijuj, duen aramaj akan kin wiada, da kadepa on ia, ma me melar akan jota pan kamaureda? Kitail en mana o nim, pwe lakap kitail pan mela.
Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
33 Der duki on, me kajonejon komail! Kajoi jued kin kawela tiak mau.
Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34 Komail ari punala, o pirida o der wiada dip! Pwe akai jaja duen Kot. Mepukat i indai on komail, pwen kanamenokki komail.
Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35 A ele amen pan inda: Iaduen me melar akan ar pan kamaureda? O iaduen war ar, me re pan maur kida?
Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
36 Pweipwei men koe! Pwe me koe kin kamoredi, jota pan maureda, ma a jota pan mela.
Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37 O me koe kamoredi, kaidin war ota me pan para, pwe wan korn eu ta, ele wan wit de eu wa toror.
Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38 A Kot pan kotiki on war a, duen a kotin kupura, o eu eu en war akan pan ale udan mom a.
Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39 Uduk karoj kaidin jon ta ieu, pwe eu jon uduk en aramaj akan, a eu jon uduk en man akan, a eu jon en manpir akan, a eu jon en mam akan.
Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40 A war lan o war pwel akan mia, a linan en war lan eu jon o linan en war pwel eu jon.
Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41 A eu jon linan en katipin, o eu linan en maram, o eu linan en uju kan, pwe nan uju kan me wuki pajan ki ar linan eu eu.
Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42 Nan iduen en me melar akan ar pan maureda. A kin kamoremoredi ap mor pajan, o pan kamaureda jo mor pajan.
Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43 A kin kamoremoredi ni jo linan, o pan maureda ni linan; a kin kamoremoredi ni luet, o pan maureda ni manaman;
Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44 A pan kamoremoredi war pwel o pan kamaureda war nenin; pwe ma war pwel mia, nan a pil pan war nenin.
Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45 Duen a intinidier: Tapin aramaj Adam wiauier, pwen nen maur amen, a Adam tia mur, pwen nen en kamaur.
Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46 A war nenin kaidin i men maj pwe war pwel, a muri me nenin.
Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47 Tapin aramaj wiaui kida pwel, a aramaj kariamen kotido jan nanlan.
Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48 A duen tapin aramaj wiauiki pwel, iduen karoj me wiauiki pwel o duen men nanlan o, iduen men nanlan kan.
Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49 O duen kitail wa mom en pwel, iduen kitail pil pan wa mom en lan.
Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50 Ri ai kan, iet me i men inda: Uduk o nta jota kak jojoki wein Kot; o me mor pajan kan jota pan jojoki me jo mor pajan.
Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51 Kilan, nai me kadiarok on komail kaponepon eu: Kaidin kitail karoj pan mela, a kitail karoj pan nitwilida.
Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52 Madan ni marep ta ieu, koronete en muri lao popeuk. Pwe koronete pan popeuk, a me melar akan ap pan kamauredan jomor pajan a kitail pan kawilikapada.
wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53 Pwe mor pajan wet pan kiawikilan jo mor pajan; o mela wet kiawikilan jomela.
Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54 A mor pajan wet lao kia wikilan jo mor pajan o mela wet kiawikilan jomela, majan o ap pan pwaida, me intinidier: Maur kadalala mela.
Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
55 Mela koe, ia om tata? Mela ia om poedi? (Hadēs )
“Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs )
56 Mana en mela dip, a manaman en dip kapun.
Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57 Danke on Kot, pwe a kotiki on kitail, en poediki atail Kaun Iejuj Krijtuj.
Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58 Ari ri ai kompok kan, komail kelail kaukaule o der wukiwuk jili, a kakairida ni omail wiawia en Kaun o, pwe komail aja, me omail dodok on Kaun o kaidin dodok mal.
Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.