< Ioanes 1 >
1 MASAN kotier ni tapi o, a masan kotier ren Kot, a masan me udan Kot.
Hapo Mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.
2 I me kotikot ren Kot ni tapi o.
Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.
3 I me dipisou karos tapi kidar, o sota man meakot mia, me kaidin i kotin wiadar.
Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.
4 Maur mi re a; o iei maur o marain en aramas.
Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.
5 A marain o me dakarada rotorot, a rotorot sota lingan kila.
Na mwanga huo huangaza gizani, nalo giza halikuweza kuushinda.
6 Aramas amen me pakadarador sang ren Kot ad a Ioanes!
Mungu alimtuma mtu mmoja jina lake Yohane,
7 I me pwara dong kadede, pwen kadede marain o pwe karos en poson pweki i.
ambaye alikuja kuwaambia watu juu ya huo mwanga. Alikuja ili kwa ujumbe wake watu wote wapate kuamini.
8 Kaidin i me marain o, a a kin kadede marain o.
Yeye hakuwa huo mwanga, ila alikuja tu kuwaambia watu juu ya huo mwanga.
9 Iei marain melel, me pwara dong sappa, ap kamaraini aramas karos.
Huu ndio mwanga halisi, mwanga unaokuja ulimwenguni, na kuwaangazia watu wote.
10 I me kotier sappa, o i me sappa tapi kidar, a sappa sasa i.
Basi, Neno alikuwako ulimwenguni; na kwa njia yake ulimwengu uliumbwa, lakini ulimwengu haukumtambua.
11 A koti dong udan sapwilim a, a sapwilim a kan me san i.
Alikuja katika nchi yake mwenyewe, nao walio wake hawakumpokea.
12 Karos, me kasamo i, a kotiki ong ir manaman, en wiala seri en Kot, ir, me poson mar a,
Lakini wale wote waliompokea na kumwamini, hao aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.
13 Me kaidin ipwidi sang nta, de inong en uduk, de inong en ol o, pwe ipwidier sang ren Kot.
Hawa wamekuwa watoto wa Mungu si kwa uwezo wa kibinadamu, wala kwa nguvu za kimwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali Mungu mwenyewe ndiye baba yao.
14 Masan me wia uduk ala o kotikot re atail, o kitail kilanger a lingan, lingan dueta lingan en Ieros eu sang ren Sam o, me dir en mak melel.
Naye Neno akawa mwanadamu, akakaa kwetu. Nasi tumeuona utukufu wake, utukufu wake yeye aliye Mwana wa pekee wa Baba; amejaa neema na ukweli.
15 Ioanes me kadede i ngil laudeda indada: Iei i, me i padaki wei: Me pan kotido mur i, iei me mier mo i, pwe a kotikotier mo i.
Yohane aliwaambia watu habari zake, akasema kwa sauti, “Huyu ndiye niliyemtaja wakati niliposema: Anakuja mtu mmoja baada yangu ambaye ni mkuu kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa.”
16 Pwe kitail karos ale sang nan audepa a mak sapan potopot.
Kutokana na ukamilifu wake sisi tumepokea neema mfululizo.
17 Pwe kapung me kokido sang Moses, a mak o melel sang Iesus Kristus.
Maana Mungu alitoa Sheria kwa njia ya Mose, lakini neema na kweli vimekuja kwa njia ya Kristo.
18 Sota me kilanger Kot kokodo, Ol ieros ta, me kin kotikot pan kupur en Sam o, i me kotin kasaledar i.
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote ule. Mwana wa pekee aliye sawa na Mungu ambaye ameungana na Baba, ndiye aliyetujulisha habari za Mungu.
19 A met en Ioanes a kadede, ni men Sus kadarala sang Ierusalem samero o lepit oko, pwen idok re a: Is koe?
Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa wakati viongozi wa Wayahudi kule Yerusalemu walipowatuma makuhani wa Walawi kwake wamwulize: “Wewe u nani?”
20 I ari kotin kadede; a sota likam; a kotin kadede: Kaidin Kristus ngai.
Yohane hakukataa kujibu swali hilo, bali alisema waziwazi, “Mimi siye Kristo.”
21 Irail idok re a: A is? Elias komui? A masani: Kaidin ngai i. Komui saukop o? A sapeng: Kaidin.
Hapo wakamwuliza, “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ni Eliya?” Yohane akajibu, “La, mimi siye.” Wakamwuliza, “Je, wewe ni yule nabii?” Yohane akawajibu, “La!”
22 Irail ap indang i: A is komui? Pwe sen sapeng irail me kadar kit dor. Da me komui kadedeki pein komui?
Nao wakamwuliza, “Basi, wewe ni nani? Wasema nini juu yako mwenyewe? Tuambie, ili tuwapelekee jibu wale waliotutuma.”
23 A masani: Ngai ngil eu, me likelikwir sili nan sap tan: Kaineneda al en Kaun o, duen saukop Iesaia masanier!
Yohane akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nabii Isaya alisema habari zake: Sauti ya mtu imesikika jangwani: Nyoosheni njia ya Bwana.”
24 A irail pakadaradoer sang ren Parisär akan.
Hao watu walikuwa wametumwa na Mafarisayo.
25 Irail ap idok re a indada: Da me komui wia paptaisiki, ma komui kaidin Kristus, o kaidin Elias, o pil kaidin saukop o?
Basi, wakamwuliza Yohane, “Kama wewe si Kristo, wala Eliya, wala yule nabii, mbona wabatiza?”
26 Ioanes sapeng irail masani: Ngai me paptaisiki pil, a amen kin kotikot nan pung omail, me komail sasa.
Yohane akawajibu, “Mimi nabatiza kwa maji, lakini yuko mmoja kati yenu, msiyemjua bado.
27 Iei i me kotido mur i, me ngai sowar ong, en lapwada sal en sapwilim a sut.
Huyo anakuja baada yangu, lakini mimi sistahili hata kumfungua kamba za viatu vyake.”
28 Mepukat wiauier Petapara palilan Iordan, wasa Ioanes kin wia paptais ia.
Mambo haya yalifanyika huko Bethania, ng'ambo ya mto Yordani ambako Yohane alikuwa anabatiza.
29 Mandan ran o a masani Iesus a koti dong i ap masani: Kilang Sippul en Kot, me kin wawei dip en sappa!
Kesho yake, Yohane alimwona Yesu akimjia, akasema, “Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu!
30 Iei i, me i padaki wei: Ol amen pan kotido mur i iei, me mier mo i, pwe a kotikotier mo i.
Huyu ndiye niliyesema juu yake: Baada yangu anakuja mtu mmoja aliye mkuu zaidi kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa!
31 A ngai so asa i, a pwe i en sansal dong Israel, iei me i kokido paptaisiki pil.
Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini nimekuja kubatiza kwa maji ili watu wa Israeli wapate kumjua.”
32 A Ioanes kadede masani: I kilanger Ngen o kotidido sang nanlang ni mom en muroi kotikot re a.
Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa: “Nilimwona Roho akishuka kama njiwa kutoka mbinguni na kutua juu yake.
33 A ngai so asa i, a me porone ia don wia paptaisiki pil, iei me kotin masani ong ia: Me koe pan kilang. Ngen piridi sok poa, o kotikoteta re a, iei i, me kin wia paptaisiki Ngen saraui.
Mimi sikumjua, lakini yule aliyenituma nikabatize watu kwa maji alikuwa ameniambia: Mtu yule utakayemwona Roho akimshukia kutoka mbinguni na kukaa juu yake, huyo ndiye anayebatiza kwa Roho Mtakatifu.
34 A i kilangadar ap kadedeki, me iei Sapwilim en Kot.
Mimi nimeona na ninawaambieni kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
35 Mandan ran o Ioanes pil kotida wasa o, o na tounpadak riamen iang i.
Kesho yake, Yohane alikuwa tena mahali hapo pamoja na wanafunzi wake wawili.
36 A ni a udial Iesus kotikot kokodo, ap masani: Kilang Sippul en Kot!
Alipomwona Yesu akipita akasema, “Tazameni! Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu.”
37 A tounpadak riamen rongadar a masan, ap idauen wei Iesus.
Hao wanafunzi walimsikia Yohane akisema maneno hayo, wakamfuata Yesu.
38 Iesus ap kotin saupeido masani ara idedauen, ap kotin masani ong ira: Da me koma rapaki? Ira potoan ong: Rapi (iet wewe: Saunpadak), ia wasa re kin kotikot ia?
Basi, Yesu aligeuka, na alipowaona hao wanafunzi wanamfuata, akawauliza, “Mnatafuta nini?” Nao wakamjibu, “Rabi (yaani Mwalimu), unakaa wapi?”
39 A kotin masani ong ira: Kodo kilang! Ira ap poto dong kilanger wasa, me a kotikot ia, ap mimieta re a ni ran o. Mepukat wiauier impan auer kaeisok.
Yesu akawaambia, “Njoni, nanyi mtaona.” Hao wanafunzi wakamfuata, wakaona mahali alipokuwa anakaa, wakashinda naye siku hiyo. Ilikuwa yapata saa kumi jioni.
40 Andreas, ri en Simon Petrus amen re ra, me rongadar sang ren Ioanes ap idedauen i.
Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa hao wawili waliokuwa wamemsikia Yohane akisema hivyo, wakamfuata Yesu.
41 I me diaradar mas udan ri a Simon, indai ong i: Se diaradar Mesias (iet wewe: Kristus).
Andrea alimkuta kwanza Simoni, ndugu yake, akamwambia, “Tumemwona Masiha” (maana yake Kristo).
42 I ap kalualang i ren Iesus. A Iesus lao masani i, ap masani: Simon, koe nain Iona, koe nok adaneki Kepas (iet wewe: Paip).
Kisha akampeleka Simoni kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama Simoni akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohane. Sasa utaitwa Kefa.” (maana yake ni Petro, yaani, “Mwamba.”)
43 Mandan ran o a pan kotilang Kaliläa, Iesus ap kotin diaradar Pilipus, masani ong i: Idauen ia do!
Kesho yake Yesu aliamua kwenda Galilaya. Basi, akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
44 Pilipus men Petsaida, kanim en Andreas o Petrus.
Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji wa akina Andrea na Petro.
45 Pilipus diaradar Natanael, ap indang i: Se diaradar i, duen me Moses intingiedier nan puk en kapung o saukop akan: Iesus men Nasaret, sapwilim en Iosep.
Naye Filipo akamkuta Nathanieli, akamwambia, “Tumemwona yule ambaye Mose aliandika juu yake katika kitabu cha Sheria, na ambaye manabii waliandika habari zake, yaani Yesu Mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti.”
46 A Natanael indai ong i: Pala maukot pan kak pwarada sang Nasaret? Pilipus indang i: Kodo kilang!
Naye Nathanieli akamwuliza Filipo, “Je, kitu chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
47 Iesus kotin masani Natanael koko dong i, ap masani duen i: Kilang, ol melel en Israel amen, me sota kin widing.
Yesu alipomwona Nathanieli akimjia alisema juu yake, “Tazameni! Huyo ni Mwisraeli halisi: hamna hila ndani yake.”
48 Natanael potoan ong i: Re kotin mangi ia sang ia? Iesus kotin sapeng masani ong i: Mon Pilipus a eker uk edo, ni om mod pan tuka pik o, I kilang uk ada.
Naye Nathanieli akamwuliza, “Umepataje kunijua?” Yesu akamwambia, “Ulipokuwa chini ya mtini hata kabla Filipo hajakuita, nilikuona.”
49 Natanael sapeng potoan ong i: Rapi, ir me Sapwilim en Kot, ir me Nanmarki en Israel.
Hapo Nathanieli akamwambia, “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu. Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
50 Iesus kotin sapeng masani ong i: Pweki I indai ong uk, me I kilang uk ada pan tuka pik o, iei me koe posonki, a koe nok kilang me lapa sang mepukat.
Yesu akamwambia, “Je, umeamini kwa kuwa nimekwambia kwamba nilikuona chini ya mtini? Utaona makubwa zaidi kuliko haya.”
51 A kotin masani ong i: Melel, melel I indai ong komail, sang met komail pan kilang nanlang a ritida o tounlang en Kot akan dauda o daudi pwarado ren Nain aramas.
Yesu akaendelea kusema, “Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu.”