< زکریا 13 >
«در آن زمان برای خاندان داوود و مردم اورشلیم چشمهای جاری خواهد شد، چشمهای که ایشان را از همهٔ گناهان و ناپاکیهایشان پاک خواهد ساخت.» | 1 |
Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
خداوند لشکرهای آسمان میفرماید: «در آن روز هرگونه بتپرستی را در سراسر سرزمین اسرائیل برمیاندازم، به طوری که اثری از آن باقی نماند و نام بتها فراموش شود. سرزمین را به کلی از وجود انبیای دروغین و روح پلید پاک میکنم، | 2 |
Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
و اگر کسی باز به دروغ نبوّت کند، به دست پدر و مادر خودش کشته خواهد شد! به او خواهند گفت:”تو باید کشته شوی، چون به نام خداوند کاذبانه نبوّت میکنی.“ | 3 |
Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
«در آن روز انبیای دروغین از نبوّتهایشان خجالت خواهند کشید و دیگر برای فریب دادن مردم لباس انبیا را بر تن نخواهند کرد. | 4 |
Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
هر یک از آنها خواهند گفت:”من نبی نیستم، من یک کشاورزم و شغلم از جوانی کشاورزی بوده است.“ | 5 |
Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
و اگر کسی بپرسد:”پس این زخمها روی بدن تو چیست؟“جواب میدهد:”در نزاع با دوستان زخمی شدهام.“» | 6 |
Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
خداوند لشکرهای آسمان میفرماید: «ای شمشیر بر ضد شبان من، آن مردی که همدوش و همکار من است، برخیز! شبان را بزن تا گوسفندان پراکنده شوند. من قوم خود را خواهم زد | 7 |
Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
و دو سوم آنها از بین خواهند رفت. | 8 |
Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
یک سوم باقیمانده را از میان آتش میگذرانم و آنها را پاک میکنم، درست مثل طلا و نقره که بهوسیلۀ آتش، خالص میشوند. ایشان نام مرا خواهند خواند و من آنها را اجابت خواهم نمود. من خواهم گفت:”اینها قوم من هستند.“و ایشان خواهند گفت:”یهوه خدای ماست.“» | 9 |
Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”