< امثال 20 >

شراب انسان را به کارهای احمقانه وا می‌دارد و مشروب باعث عربده‌کشی می‌شود؛ چه نادانند کسانی که خود را اسیر مشروب می‌کنند. 1
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
غضب پادشاه همچون غرش شیر است. هر که خشم او را برانگیزاند جان خود را به خطر می‌اندازد. 2
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
اجتناب از نزاع برای شخص، عزت می‌آورد. فقط اشخاص نادان نزاع به پا می‌کنند. 3
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
آدم تنبل به موقع زمینش را شخم نمی‌زند، پس در هنگام برداشت محصول هر چه می‌گردد چیزی نمی‌یابد. 4
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
پند نیکو در اعماق دل مشورت دهنده مانند آب در ته چاه است و شخص فهمیده آن را بیرون می‌کشد. 5
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
بسیارند کسانی که ادعا می‌کنند خوب و باوفا هستند، ولی کیست که بتواند شخص واقعاً باوفایی پیدا کند؟ 6
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
فرزندان شخص امین و درستکار در زندگی سعادتمند خواهند شد. 7
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
پادشاهی که بر مسند قضاوت می‌نشیند به دقت جوانب امر را می‌سنجد و حق را از باطل تشخیص می‌دهد. 8
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
کیست که بتواند بگوید: «دل خود را پاک نگه داشته‌ام و از گناه مبرا هستم.» 9
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
خداوند از اشخاصی که در داد و ستد از وزنه‌ها و پیمانه‌های نادرست استفاده می‌کنند متنفر است. 10
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
حتی کودک را می‌توان از طرز رفتارش شناخت و فهمید که آنچه انجام می‌دهد پاک و درست است یا نه. 11
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
گوش شنوا و چشم بینا، هر دو بخشش خداوند هستند. 12
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
اگر خواب را دوست داشته باشی فقیر می‌شوی؛ پس بیدار بمان تا سیر شوی. 13
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
خریدار به جنس نگاه می‌کند و می‌گوید: «بد است!» اما بعد از خرید، از آن تعریف می‌کند. 14
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
سخنان حکیمانه گرانبهاتر از طلا و نادرتر از جواهر است. 15
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
از کسی که نزد تو ضامن شخص غریبی می‌شود گرو بگیر. 16
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
نانی که از راه کلاهبرداری به دست می‌آید لذیذ است، اما سرانجام کام را تلخ می‌کند. 17
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
نقشه‌هایت را بدون مشورت با دیگران عملی نکن و بدون تدبیر به جنگ نرو. 18
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
آدم سخن‌چین رازها را فاش می‌کند، پس با چنین شخصی معاشرت نکن. 19
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
چراغ زندگی کسی که پدر و مادر خود را لعنت کند، خاموش خواهد شد. 20
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
مالی که آسان به دست آمده باشد برکتی نخواهد داشت. 21
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
بدی را با بدی تلافی نکن، بلکه منتظر باش تا خداوند عمل کند. 22
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
خداوند از اشخاصی که در داد و ستد از ترازو و سنگهای نادرست استفاده می‌کنند متنفر است. 23
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
خداوند راه زندگی ما را تعیین می‌کند، پس انسان چگونه می‌تواند بفهمد زندگی او به کجا ختم می‌شود؟ 24
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
هرگز نسنجیده قولی به خداوند نده، زیرا ممکن است گرفتار شوی. 25
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
پادشاه دانا شریران را تشخیص می‌دهد و آنها را به شدت مجازات می‌کند. 26
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
وجدان انسان به منزلهٔ چراغ خداوند است که تمام انگیزه‌های پنهانی او را آشکار می‌سازد. 27
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
هرگاه پادشاهی مهربان و امین باشد، سلطنتش از محبت پایدار می‌ماند. 28
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
شکوه جوانان، قوت ایشان است و عزت پیران، تجربه ایشان. 29
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
تنبیه برای بدن دردناک است اما دل را از بدی پاک می‌کند. 30
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

< امثال 20 >