< اعداد 5 >

خداوند به موسی فرمود: 1
BWANA alinena na Musa. Akasema,
«به بنی‌اسرائیل دستور بده که تمام اشخاص جذامی و همهٔ کسانی را که عضو تناسلی‌شان جریان دائمی دارند و آنانی را که در اثر تماس با جنازه نجس شده‌اند، از اردوگاه بیرون کنند. 2
“Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti.
خواه مرد باشند خواه زن، ایشان را بیرون کنند تا اردوگاه شما که من در آن ساکنم نجس نشود.» 3
Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake,”
قوم اسرائیل طبق دستور خداوند عمل کرده، این اشخاص را بیرون راندند. 4
Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
سپس خداوند به موسی فرمود: 5
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
«این دستورها را به بنی‌اسرائیل بده: هر کس، چه مرد باشد چه زن، هرگاه به خداوند خیانت کرده، خسارتی به کسی وارد آورد، 6
“Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia.
باید به گناه خود اعتراف نموده، علاوه بر جبران کامل خسارت، یک پنجم خسارت وارده را نیز به شخص خسارت دیده بپردازد. 7
Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
ولی اگر شخصی که خسارت دیده است بمیرد و قوم و خویش نزدیکی نداشته باشد تا به او خسارت پرداخت شود، در آن صورت باید آن را برای خداوند به کاهن بپردازد. درضمن خطاکار باید یک قوچ نیز برای کفاره به کاهن بدهد. 8
Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.
تمام هدایای مقدّس که بنی‌اسرائیل برای کاهن می‌آورند، مال کاهن خواهد بود. 9
Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake.
هر کاهنی می‌تواند تمام هدایای مقدّس را که می‌گیرد، برای خود نگه دارد.» 10
Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake.”
و خداوند به موسی فرمود: 11
Tena BWANA akanena na Musa. Akasema,
«این دستورها را به بنی‌اسرائیل بده: اگر زنِ کسی از او برگشته، به وی خیانت ورزد، 12
“Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
و با مردی دیگر همبستر شود، ولی شوهرش یا کسی دیگر از این ماجرا آگاه نشود، آن زن خود را نجس ساخته، هرچند که شاهدی نبوده و او در حین عمل گرفتار نشده باشد. 13
Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika.
اگر شوهرش غیرتی شده، به زنش شک کند و بخواهد بداند زنش خود را نجس ساخته یا نه، 14
Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
او باید برای روشن شدن حقیقت، زن خود را پیش کاهن بیاورد. در ضمن آن مرد باید یک کیلو آرد جو هم با خود بیاورد، ولی آن را با روغن یا کندر مخلوط نکند، چون این هدیهٔ بدگمانی است و برای تشخیص گناه تقدیم می‌شود. 15
Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
«کاهن، آن زن را به حضور خداوند بیاورد، 16
Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA.
و قدری آب مقدّس در کوزه‌ای سفالین بریزد و مقداری از غبار کف خیمۀ عبادت را با آن مخلوط کند. 17
Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
سپس زن را در حضور خداوند بر پا داشته، موی بافتهٔ سر او را باز کند و هدیهٔ بدگمانی را در دستهایش بگذارد تا معلوم شود که آیا بدگمانی شوهرش بجاست یا نه. کاهن در حالی که کوزهٔ آب تلخ لعنت را در دست دارد جلوی زن بایستد. 18
Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu.
آنگاه از آن زن بخواهد قسم بخورد که بی‌گناه است و به او بگوید:”اگر غیر از شوهرت مرد دیگری با تو همبستر نشده است، و اگر در مدتی که زیر اقتدار شوهرت بوده‌ای، از شوهرت برنگشته‌ای و خود را نجس نساخته‌ای، از اثرات این آب تلخ لعنت مبرا باش. 19
Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
ولی اگر از او برگشته و به او خیانت کرده‌ای و با همبستر شدن با مردی دیگر خود را نجس ساخته‌ای…“ 20
Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe,
«در اینجا کاهن زن را وادارد تا سوگندِ لعنت بخورد و به زن بگوید:”لعنت خداوند در میان قومت گریبانگیر تو شود و او رَحِمت را بخشکاند و شکمت را متورم سازد. 21
ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba.
و این آبِ لعنت به بدن تو داخل شده شکمت را متورم سازد و رَحِمت را بخشکاند.“و زن باید بگوید:”آری، اینچنین شود.“ 22
Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
بعد کاهن این لعنتها را در یک طومار بنویسد و آنها را در آب تلخ بشوید. 23
Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
سپس آن آب تلخ را به زن بدهد تا بنوشد. 24
Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu.
«سپس کاهن هدیهٔ بدگمانی را از دست زن بگیرد و آن را در حضور خداوند تکان داده، روی مذبح بگذارد. 25
Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni.
مشتی از آن را به عنوان نمونه روی آتش مذبح بسوزاند و بعد، از زن بخواهد آب را بنوشد. 26
Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
اگر او به شوهرش خیانت کرده باشد آب بر او اثر می‌کند و شکمش متورم شده، نازا می‌گردد و در میان قوم اسرائیل مورد لعنت قرار می‌گیرد 27
Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake.
ولی اگر او پاک بوده و زنا نکرده باشد، به او آسیبی نمی‌رسد و می‌تواند حامله شود. 28
Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
«این است قانون بدگمانی در مورد زنی که شوهرش نسبت به وی بدگمان شده باشد. 29
Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika.
همان‌طور که گفته شد در چنین موردی شوهر باید زن خود را به حضور خداوند بیاورد تا کاهن طی مراسمی قضیه را روشن سازد که آیا زن به شوهرش خیانت کرده یا نه. 30
Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
اگر زن مقصر شناخته شود، تاوان گناهش را پس خواهد داد، اما شوهرش در این مورد بی‌تقصیر خواهد بود، زیرا خود زن مسئول گناهش است.» 31
Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake.”

< اعداد 5 >