< اعداد 5 >

خداوند به موسی فرمود: 1
Bwana akamwambia Mose,
«به بنی‌اسرائیل دستور بده که تمام اشخاص جذامی و همهٔ کسانی را که عضو تناسلی‌شان جریان دائمی دارند و آنانی را که در اثر تماس با جنازه نجس شده‌اند، از اردوگاه بیرون کنند. 2
“Waamuru Waisraeli kumtoa nje ya kambi mtu yeyote ambaye ana ugonjwa wa ngozi uambukizao, au anayetokwa na majimaji ya aina yoyote, au ambaye ni najisi kwa utaratibu wa ibada kwa sababu ya maiti.
خواه مرد باشند خواه زن، ایشان را بیرون کنند تا اردوگاه شما که من در آن ساکنم نجس نشود.» 3
Hii itakuwa ni kwa wote, yaani, wanaume na wanawake; watoeni nje ya kambi ili wasije wakanajisi kambi yao, ambamo ninaishi miongoni mwao.”
قوم اسرائیل طبق دستور خداوند عمل کرده، این اشخاص را بیرون راندند. 4
Waisraeli wakafanya hivyo; wakawatoa nje ya kambi. Wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amemwelekeza Mose.
سپس خداوند به موسی فرمود: 5
Bwana akamwambia Mose,
«این دستورها را به بنی‌اسرائیل بده: هر کس، چه مرد باشد چه زن، هرگاه به خداوند خیانت کرده، خسارتی به کسی وارد آورد، 6
“Waambie Waisraeli, ‘Wakati mwanaume au mwanamke akimkosea mwenzake kwa njia yoyote, na kwa hivyo akawa si mwaminifu kwa Bwana, mtu huyo ana hatia,
باید به گناه خود اعتراف نموده، علاوه بر جبران کامل خسارت، یک پنجم خسارت وارده را نیز به شخص خسارت دیده بپردازد. 7
na ni lazima atubu dhambi aliyoifanya. Ni lazima atoe malipo kamili kwa ajili ya kosa lake, aongeze sehemu ya tano juu ya malipo hayo na kutoa yote kwa mtu aliyemkosea.
ولی اگر شخصی که خسارت دیده است بمیرد و قوم و خویش نزدیکی نداشته باشد تا به او خسارت پرداخت شود، در آن صورت باید آن را برای خداوند به کاهن بپردازد. درضمن خطاکار باید یک قوچ نیز برای کفاره به کاهن بدهد. 8
Lakini ikiwa mtu huyo hana jamaa ya karibu ambaye malipo yanaweza kufanywa kwa ajili ya kosa, malipo yatakuwa mali ya Bwana, nayo ni lazima apewe kuhani, pamoja na kondoo dume ambaye anatumika kufanyia upatanisho kwa ajili yake.
تمام هدایای مقدّس که بنی‌اسرائیل برای کاهن می‌آورند، مال کاهن خواهد بود. 9
Matoleo yote matakatifu ya Waisraeli wanayoleta kwa kuhani yatakuwa yake.
هر کاهنی می‌تواند تمام هدایای مقدّس را که می‌گیرد، برای خود نگه دارد.» 10
Kila kitu cha mtu kilichowekwa wakfu ni chake mwenyewe, lakini kile atoacho kwa kuhani kitakuwa cha kuhani.’”
و خداوند به موسی فرمود: 11
Kisha Bwana akamwambia Mose,
«این دستورها را به بنی‌اسرائیل بده: اگر زنِ کسی از او برگشته، به وی خیانت ورزد، 12
“Nena na Waisraeli uwaambie: ‘Ikiwa mke wa mtu amepotoka na si mwaminifu kwa mumewe,
و با مردی دیگر همبستر شود، ولی شوهرش یا کسی دیگر از این ماجرا آگاه نشود، آن زن خود را نجس ساخته، هرچند که شاهدی نبوده و او در حین عمل گرفتار نشده باشد. 13
kwa kukutana kimwili na mwanaume mwingine, tendo hili likafichika kwa mumewe na unajisi wake usigundulike (kwa kuwa hakuna ushahidi dhidi yake, naye hakukamatwa katika tendo hilo),
اگر شوهرش غیرتی شده، به زنش شک کند و بخواهد بداند زنش خود را نجس ساخته یا نه، 14
nazo hisia za wivu zikamjia mumewe na kumshuku mkewe, naye mke yule ni najisi, au mumewe ana wivu na akamshuku ingawa si najisi,
او باید برای روشن شدن حقیقت، زن خود را پیش کاهن بیاورد. در ضمن آن مرد باید یک کیلو آرد جو هم با خود بیاورد، ولی آن را با روغن یا کندر مخلوط نکند، چون این هدیهٔ بدگمانی است و برای تشخیص گناه تقدیم می‌شود. 15
basi atampeleka mkewe kwa kuhani. Huyo mume itampasa apeleke pia sadaka ya unga wa shayiri kiasi cha sehemu ya kumi ya efa kwa niaba ya mkewe. Huyo mwanaume kamwe asimimine mafuta juu ya huo unga wala asiweke uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu, sadaka ya ukumbusho ili kukumbushia uovu.
«کاهن، آن زن را به حضور خداوند بیاورد، 16
“‘Kuhani atamleta huyo mwanamke na kumsimamisha mbele za Bwana.
و قدری آب مقدّس در کوزه‌ای سفالین بریزد و مقداری از غبار کف خیمۀ عبادت را با آن مخلوط کند. 17
Kisha kuhani atachukua sehemu ya maji matakatifu ndani ya gudulia la udongo na kuchanganya na baadhi ya vumbi kutoka sakafu ya Maskani.
سپس زن را در حضور خداوند بر پا داشته، موی بافتهٔ سر او را باز کند و هدیهٔ بدگمانی را در دستهایش بگذارد تا معلوم شود که آیا بدگمانی شوهرش بجاست یا نه. کاهن در حالی که کوزهٔ آب تلخ لعنت را در دست دارد جلوی زن بایستد. 18
Baada ya kuhani kumsimamisha huyo mwanamke mbele za Bwana, atazifungua nywele za huyo mwanamke na kuweka sadaka ya ukumbusho mikononi mwake, ile sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu, huku kuhani mwenyewe akishikilia yale maji machungu yaletayo laana.
آنگاه از آن زن بخواهد قسم بخورد که بی‌گناه است و به او بگوید:”اگر غیر از شوهرت مرد دیگری با تو همبستر نشده است، و اگر در مدتی که زیر اقتدار شوهرت بوده‌ای، از شوهرت برنگشته‌ای و خود را نجس نساخته‌ای، از اثرات این آب تلخ لعنت مبرا باش. 19
Kisha kuhani atamwapiza huyo mwanamke, akimwambia, “Ikiwa hakuna mwanaume mwingine aliyekutana kimwili nawe, wala hujapotoka na kuwa najisi wakati ukiwa umeolewa na mumeo, maji haya machungu yaletayo laana na yasikudhuru.
ولی اگر از او برگشته و به او خیانت کرده‌ای و با همبستر شدن با مردی دیگر خود را نجس ساخته‌ای…“ 20
Lakini ikiwa umepotoka wakati ukiwa umeolewa na mume wako na umejinajisi mwenyewe kwa kukutana kimwili na mwanaume mwingine asiyekuwa mumeo”;
«در اینجا کاهن زن را وادارد تا سوگندِ لعنت بخورد و به زن بگوید:”لعنت خداوند در میان قومت گریبانگیر تو شود و او رَحِمت را بخشکاند و شکمت را متورم سازد. 21
hapa kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya laana ya kiapo akisema: “Bwana na awafanye watu wako wakulaani na kukukataa, wakati Bwana atakapolifanya paja lako kupooza na tumbo lako kuvimba.
و این آبِ لعنت به بدن تو داخل شده شکمت را متورم سازد و رَحِمت را بخشکاند.“و زن باید بگوید:”آری، اینچنین شود.“ 22
Maji haya yaletayo laana na yaingie ndani ya mwili wako ili tumbo lako livimbe na paja lako lipooze.” “‘Kisha mwanamke atasema, “Amen. Iwe hivyo.”
بعد کاهن این لعنتها را در یک طومار بنویسد و آنها را در آب تلخ بشوید. 23
“‘Kuhani ataandika laana hizi kwenye kitabu, kisha atazioshea laana hizo kwenye yale maji machungu.
سپس آن آب تلخ را به زن بدهد تا بنوشد. 24
Kuhani atamnywesha yule mwanamke yale maji machungu yaletayo laana, nayo maji haya yatamwingia na kumsababishia maumivu makali.
«سپس کاهن هدیهٔ بدگمانی را از دست زن بگیرد و آن را در حضور خداوند تکان داده، روی مذبح بگذارد. 25
Kuhani atachukua sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu kutoka mikononi mwa huyo mwanamke, naye ataipunga mbele za Bwana na kuileta madhabahuni.
مشتی از آن را به عنوان نمونه روی آتش مذبح بسوزاند و بعد، از زن بخواهد آب را بنوشد. 26
Kisha kuhani atachota sadaka ya nafaka mkono uliojaa kama sehemu ya kumbukumbu na kuiteketeza juu ya madhabahu, baada ya hayo, atamtaka huyo mwanamke anywe yale maji.
اگر او به شوهرش خیانت کرده باشد آب بر او اثر می‌کند و شکمش متورم شده، نازا می‌گردد و در میان قوم اسرائیل مورد لعنت قرار می‌گیرد 27
Kama amejitia unajisi na kukosa uaminifu kwa mumewe, wakati anapotakiwa anywe maji yale yaletayo laana, yatamwingia na kusababisha maumivu makali; tumbo lake litavimba na paja lake litapooza, naye atakuwa amelaaniwa miongoni mwa watu wake.
ولی اگر او پاک بوده و زنا نکرده باشد، به او آسیبی نمی‌رسد و می‌تواند حامله شود. 28
Hata hivyo, ikiwa huyo mwanamke hakujitia unajisi, naye ni safi, atasafishwa hatia na ataweza kuzaa watoto.
«این است قانون بدگمانی در مورد زنی که شوهرش نسبت به وی بدگمان شده باشد. 29
“‘Basi, hii ndiyo sheria ya wivu mwanamke anapopotoka na kujitia unajisi akiwa ameolewa na mumewe,
همان‌طور که گفته شد در چنین موردی شوهر باید زن خود را به حضور خداوند بیاورد تا کاهن طی مراسمی قضیه را روشن سازد که آیا زن به شوهرش خیانت کرده یا نه. 30
au hisia za wivu zinapomjia mwanaume kwa sababu ya kumshuku mkewe. Kuhani atamfanya huyo mwanamke kusimama mbele za Bwana na atatumia sheria hii yote kwa huyo mwanamke.
اگر زن مقصر شناخته شود، تاوان گناهش را پس خواهد داد، اما شوهرش در این مورد بی‌تقصیر خواهد بود، زیرا خود زن مسئول گناهش است.» 31
Mume atakuwa hana hatia ya kosa lolote, bali mwanamke atayachukua matokeo ya dhambi yake.’”

< اعداد 5 >