< لاویان 5 >
«هرگاه کسی از وقوع جرمی اطلاع داشته باشد ولی در مورد آنچه که دیده یا شنیده در دادگاه شهادت ندهد، مجرم است. | 1 |
“‘Ikiwa mtu atakuwa ametenda dhambi kwa sababu hakusema alipotakiwa kutoa ushahidi hadharani kuhusu jambo aliloona au kujua habari zake, yeye anastahili adhabu.
«هرگاه کسی لاشهٔ حیوان حرام گوشتی را لمس کند، حتی اگر ندانسته این کار را کرده باشد، نجس و مجرم است. | 2 |
“‘Au kama mtu akigusa kitu chochote ambacho ni najisi, iwe ni mizoga ya wanyama pori walio najisi, au ya wanyama wafugwao walio najisi, au ya viumbe vitambaavyo ardhini, hata akiwa hana habari, amekuwa najisi na mwenye hatia.
هرگاه کسی نجاست انسان را لمس کند، حتی اگر ندانسته این کار را کرده باشد، وقتی متوجه شد چه کرده است، مجرم میباشد. | 3 |
“‘Au kama akigusa kitu kilicho kichafu kinachotokana na binadamu, kitu chochote kile kinachoweza kumfanya awe najisi, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
«اگر کسی نسنجیده قولی دهد و قسم بخورد که آن را بجا آورد ولی بعد پی ببرد که قول بیجایی داده است، مجرم میباشد. | 4 |
“‘Au kama mtu ameapa kufanya kitu chochote bila kufikiri, kiwe chema au kibaya, kwa vyovyote mtu aweza kuapa bila kujali, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
در هر یک از این موارد، شخص باید به گناهش اعتراف کند | 5 |
“‘Wakati mtu yeyote atakapokuwa na hatia katika mojawapo ya haya, lazima akiri ni kwa njia gani ametenda dhambi,
و برای قربانی گناه خود یک بره یا بز ماده نزد خداوند بیاورد تا کاهن برایش کفاره کند. | 6 |
na kama adhabu ya dhambi aliyoitenda, lazima alete kwa Bwana kondoo jike au mbuzi jike kutoka kwenye kundi lake kama sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yake.
«اگر شخص مجرم تنگدست باشد و نتواند برهای بیاورد، میتواند دو قمری یا دو جوجه کبوتر برای کفارهٔ گناه خود به خداوند تقدیم کند، یکی برای قربانی گناه و دیگری برای قربانی سوختنی. | 7 |
“‘Lakini huyo mtu kama hataweza kumtoa mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana kuwa adhabu kwa ajili ya dhambi yake, mmoja wa hao ndege kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wa pili kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
کاهن پرندهای را که برای قربانی گناه آورده شده، بگیرد و سرش را ببرد، ولی طوری که از تنش جدا نشود. | 8 |
Atawaleta kwa kuhani, ambaye atamtoa kwanza ndege mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo na kuacha kichwa chake kikiningʼinia,
سپس قدری از خون آن را بر پهلوی مذبح بپاشد و بقیه را به پای مذبح بریزد. این، قربانی گناه است. | 9 |
naye atanyunyiza sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi kwenye pembe za madhabahu. Damu iliyobaki lazima ichuruzwe chini ya madhabahu. Hii ni sadaka ya dhambi.
پرندهٔ دیگر را به عنوان قربانی سوختنی طبق دستورالعملی که قبلا داده شده است قربانی کند. به این ترتیب کاهن برای گناه او کفاره خواهد کرد و گناه او بخشیده خواهد شد. | 10 |
Kisha kuhani atamtoa yule ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na hivyo kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
«اگر او فقیرتر از آنست که بتواند دو قمری یا دو جوجه کبوتر برای کفارهٔ گناه خود قربانی کند، میتواند یک کیلو آرد مرغوب بیاورد. ولی نباید آن را با روغن زیتون مخلوط کند یا کندر بر آن بگذارد، زیرا این، قربانی گناه است. | 11 |
“‘Ikiwa basi, hawezi kupata hua wawili au makinda mawili ya njiwa, ataleta sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kamwe asiweke mafuta wala uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya dhambi.
آرد را پیش کاهن بیاورد تا کاهن مشتی از آن را به عنوان نمونه بردارد و روی مذبح بسوزاند، درست مثل قربانیهایی که بر آتش به خداوند تقدیم میشود. این، قربانی گناه اوست. | 12 |
Atauleta unga kwa kuhani, ambaye atachukua konzi moja kama sehemu ya kumbukumbu na atauteketeza kwenye madhabahu juu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya dhambi.
به این ترتیب کاهن برای گناه او در هر یک از این موارد، کفاره خواهد کرد و او بخشیده خواهد شد. در این قربانی نیز مثل هدیهٔ آردی، بقیهٔ آرد به کاهن تعلق میگیرد.» | 13 |
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yoyote ya hizo alizotenda, naye atasamehewa. Sadaka iliyobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyokuwa ile sadaka ya nafaka.’”
خداوند این دستورها را به موسی داد: | 14 |
Bwana akamwambia Mose:
«هرگاه کسی در دادن هدیهای که در نظر خداوند مقدّس است ناخواسته قصور ورزد، باید یک قوچ سالم و بیعیب برای قربانی جبران به خداوند تقدیم نماید. قوچی که برای قربانی جبران اهدا میشود ارزش آن باید به مثقال نقره برحسب مثقال عبادتگاه برآورده شود. | 15 |
“Mtu anapokiuka na kutenda dhambi pasipo kukusudia kuhusu mojawapo ya mambo matakatifu ya Bwana, huyo mtu ataleta kwa Bwana kama adhabu kondoo dume mmoja kutoka kundi lake, asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Hii ni sadaka ya hatia.
او باید علاوه بر باز پرداخت هدیه، یک پنجم ارزش آن را نیز به آن افزوده، همه را به کاهن بدهد. کاهن با آن قوچ قربانی جبران، برایش کفاره خواهد کرد و او بخشیده خواهد شد. | 16 |
Ni lazima alipe kwa yale aliyoshindwa kufanya kuhusu vitu vitakatifu, kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani ile na kuitoa yote kwa kuhani, ambaye atamfanyia upatanisho kwa huyo kondoo dume kama sadaka ya dhambi, naye atasamehewa.
«اگر کسی مرتکب گناهی شده، یکی از قوانین خداوند را زیر پا بگذارد، ولی نداند که چنین کاری از او سر زده است، باز مجرم است و باید تاوان گناهش را پس بدهد. | 17 |
“Kama mtu akifanya dhambi na kufanya yale yaliyokatazwa katika mojawapo ya amri za Bwana, hata ikiwa hajui, yeye ana hatia na anastahili adhabu.
او باید برای قربانی جبران یک قوچ سالم و بیعیب نزد کاهن بیاورد. قیمت قوچ باید مطابق قیمت تعیین شده باشد. کاهن با این قربانی برای او کفاره کند تا گناهش بخشیده شود. | 18 |
Atamletea kuhani kama sadaka ya hatia kondoo dume kutoka kundi lake, kondoo asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa kosa alilotenda bila kukusudia, naye atasamehewa.
این قربانی جبران است برای جرمی که او نسبت به خداوند مرتکب شده است.» | 19 |
Hii ni sadaka ya hatia; amekuwa na hatia kwa kufanya kosa dhidi ya Bwana.”