< یوشع 9 >

وقتی پادشاهان سرزمینهای همسایه از فتوحات بنی‌اسرائیل باخبر شدند، به خاطر حفظ جان و مال خود با هم متحد گشتند تا با یوشع و بنی‌اسرائیل بجنگند. اینها پادشاهان قبایل حیتی، اموری، کنعانی، فرزی، حوی و یبوسی بودند که در غرب رود اردن و سواحل دریای مدیترانه تا کوههای لبنان در شمال، زندگی می‌کردند. 1
Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
2
wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
اما مردم جبعون وقتی خبر پیروزی یوشع بر شهرهای اریحا و عای را شنیدند، برای نجات جان خود، عوض جنگ به حیله متوسل شدند. آنها گروهی را با لباسهای ژنده و کفشهای کهنه و پینه زده، الاغهایی با پالانهای مندرس و مقداری نان کپک زده خشک و چند مشک شراب که کهنه و وصله‌دار بودند نزد یوشع فرستادند. 3
Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
4
nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
5
Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
وقتی این گروه به اردوگاه اسرائیل در جلجال رسیدند، نزد یوشع و سایر مردان اسرائیلی رفته، گفتند: «ما از سرزمین دوری به اینجا آمده‌ایم تا از شما بخواهیم با ما پیمان صلح ببندید.» 6
Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
اما اسرائیلی‌ها گفتند: «ما چطور بدانیم که شما ساکن این سرزمین نیستید؟ چون اگر در این سرزمین ساکن باشید نمی‌توانیم با شما پیمان صلح ببندیم.» 7
Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
آنها به یوشع گفتند: «ما بندگان تو هستیم.» ولی یوشع از آنها پرسید: «شما چه کسانی هستید و از کجا آمده‌اید؟» 8
Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
گفتند: «ما بندگانت از یک سرزمین دور به اینجا آمده‌ایم؛ زیرا شهرت خداوند، خدایتان به گوش ما رسیده است و شنیده‌ایم که او چه کارهای بزرگی در مصر کرد 9
Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
و چه بلایی بر سر دو پادشاه اموری که در طرف شرق اردن بودند یعنی سیحون، پادشاه حشبون و عوج، پادشاه باشان که در عشتاروت حکومت می‌کرد، آورد. 10
pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
پس بزرگان و مردم ما از ما خواستند که توشه‌ای برای سفر طولانی بگیریم و به حضور شما بیاییم و بگوییم که ما بندگان شما هستیم و از شما می‌خواهیم با ما پیمان صلح ببندید. 11
Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
وقتی عازم سفر شدیم این نانها تازه از تنور درآمده بودند، اما حالا چنانکه می‌بینید خشک شده و کپک زده‌اند! 12
Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
این مشکهای شراب در آغاز سفر، نو بودند، اما حالا کهنه شده و ترکیده‌اند! لباسها و کفشهای ما به سبب طولانی بودن راه، مندرس شده‌اند.» 13
Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
یوشع و بزرگان اسرائیل با دیدن توشهٔ آنها، حرفهایشان را باور کردند و بدون آنکه با خداوند مشورت نمایند، یوشع با آنها پیمان صلح بست و قول داد که ایشان را از بین نبرد و بزرگان اسرائیل نیز قسم خوردند که این پیمان را نشکنند. 14
Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
15
Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
هنوز سه روز از این موضوع نگذشته بود که معلوم شد این گروه مسافر از همسایگانشان در آن سرزمین هستند و در همان نزدیکی زندگی می‌کنند! 16
Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
بنی‌اسرائیل در مسیر پیشروی خود، سه روز بعد به شهرهای ایشان رسیدند. (نام این شهرها جبعون، کفیره، بئیروت و قریه یعاریم بود.) 17
Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
اما به خاطر سوگندی که بزرگان اسرائیل به نام خداوند، خدای اسرائیل یاد کرده بودند نتوانستند آنها را از بین ببرند. اسرائیلی‌ها به بزرگان قوم اعتراض کردند، 18
Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
اما آنها در جواب گفتند: «ما به نام یهوه، خدای اسرائیل سوگند خورده‌ایم که به آنها صدمه‌ای نزنیم. 19
lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
پس باید به سوگند خود وفا نموده، بگذاریم که زنده بمانند؛ چون اگر پیمانی را که با آنان بسته‌ایم بشکنیم، خشم خداوند بر ما افروخته خواهد شد.» 20
Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
سپس اضافه کردند: «بگذارید ایشان زنده بمانند و برای ما هیزم بشکنند و آب بیاورند.» 21
Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
یوشع جبعونی‌ها را احضار کرده، گفت: «چرا ما را فریب داده، گفتید که از سرزمین بسیار دور آمده‌اید و حال آنکه همسایهٔ نزدیک ما هستید؟ 22
Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
پس شما زیر لعنت خواهید بود و بعد از این باید همیشه به عنوان غلام برای خانهٔ خدای ما هیزم بشکنید و آب مورد نیاز را تهیه کنید.» 23
Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
آنها گفتند: «چون شنیده بودیم که خداوند، خدای شما به خدمتگزار خود موسی دستور داده بود تمام این سرزمین را تصرف نماید و ساکنانش را نابود کند، پس بسیار ترسیدیم و به خاطر نجات جان خود این کار را کردیم. 24
Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
ولی حالا در اختیار شما هستیم، هر طور که صلاح می‌دانید با ما رفتار کنید.» 25
Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
یوشع به مردم اسرائیل اجازه نداد آنها را بکشند، 26
Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
و ایشان را برای شکستن هیزم و کشیدن آب برای مردم اسرائیل و مذبح خداوند تعیین نمود. ایشان تا امروز به کار خود در جایی که خداوند برای عبادت تعیین کرده است ادامه می‌دهند. 27
Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.

< یوشع 9 >