< ایوب 32 >
آن سه دوست ایوب، دیگر به او جواب ندادند، چون ایوب بر بیگناهی خود پافشاری میکرد. | 1 |
Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
شخصی به نام الیهو، پسر برکئیل بوزی، از طایفهٔ رام، که شاهد این گفتگو بود خشمگین شد، زیرا ایوب نمیخواست قبول کند که گناهکار است و خدا به حق او را مجازات کرده است. | 2 |
Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
او از آن سه رفیق ایوب نیز خشمگین بود، چون بدون اینکه پاسخ قانع کنندهای برای ایوب داشته باشند، او را محکوم میکردند. | 3 |
Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
الیهو برای سخن گفتن با ایوب صبر کرده بود چون سایرین از او بزرگتر بودند. | 4 |
Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
اما وقتی که دید آنها دیگر جوابی ندارند، برآشفت. | 5 |
Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
الیهو به سخن آمده چنین گفت: من جوانم و شما پیر. به همین علّت لب فرو بستم و جرأت نکردم عقیدهام را برای شما بیان کنم، | 6 |
Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
زیرا گفتهاند که پیران داناترند. | 7 |
Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
ولی حکمت و دانایی فقط بستگی به سن و سال ندارد، بلکه آن روحی که در انسان قرار دارد و نفس خدای قادر مطلق است، به انسان حکمت میبخشد. | 8 |
Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
پس به من گوش بدهید و بگذارید عقیدهام را بیان کنم. | 10 |
Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
من در تمام این مدت صبر کردم و با دقت به سخنان و دلایل شما گوش دادم. هیچکدام از شما نتوانستید پاسخ ایوب را بدهید و یا ثابت کنید که او گناهکار است. | 11 |
Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
به من نگویید: «ایوب بسیار حکیم است. فقط خدا میتواند او را قانع کند.» | 13 |
Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
اگر ایوب با من به مباحثه پرداخته بود، با این نوع منطق پاسخ او را نمیدادم! | 14 |
Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
شما حیران نشستهاید و هیچ جوابی ندارید. | 15 |
Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
آیا حال که شما سکوت کردهاید من هم باید همچنان صبر کنم و ساکت بمانم؟ | 16 |
Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
نه، من به سهم خود جواب میدهم. | 17 |
La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
حرفهای زیادی برای گفتن دارم و دیگر نمیتوانم صبر کنم. | 18 |
Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
مانند مشکی هستم که از شراب پر شده و نزدیک ترکیدن است. | 19 |
Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
باید حرف بزنم تا راحت شوم. پس بگذارید من هم به سهم خود جواب بدهم. | 20 |
Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
من قصد ندارم از کسی طرفداری کنم و سخنان تملقآمیز بگویم، | 21 |
Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
چون انسان چاپلوسی نیستم و گرنه خالقم مرا هلاک میکرد. | 22 |
Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.