< ایوب 18 >

آنگاه بلدد شوحی پاسخ داد: 1
Bildadi Mshuhi akajibu:
تا کی می‌خواهی به این حرفها ادامه دهی؟ اگر می‌خواهی ما هم سخن بگوییم قدری عاقلانه‌تر صحبت کن. 2
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
آیا تو فکر می‌کنی ما مثل حیوان بی‌شعور هستیم؟ 3
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
چرا بی‌جهت خشمگین می‌شوی و به خود صدمه می‌زنی؟ آیا انتظار داری به خاطر تو زمین بلرزد و صخره‌ها واژگون شوند. 4
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
چراغ مرد بدکار خاموش خواهد شد و شعله‌اش نوری نخواهد داد. 5
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
در هر خانه‌ای که شرارت وجود داشته باشد، تاریکی حکمفرما خواهد بود. 6
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
قدمهای شرور سست می‌شوند و او قربانی نقشه‌های خود می‌گردد. 7
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
او با پای خود به دام می‌افتد و تله پاشنهٔ پای او را می‌گیرد و او را رها نمی‌کند. 8
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
سر راه او تله‌ها پنهان شده است. 10
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
ترسها از هر طرف به او هجوم می‌آورند و او را قدم به قدم تعقیب می‌کنند. 11
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
مصیبت دهان خود را برای او باز کرده و فلاکت آماده است تا او را به کام خود فرو برد. 12
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
مرض مهلک به جان او می‌افتد و او را به کام مرگ می‌کشاند. 13
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
از خانهٔ امن خود جدا شده، نزد پادشاه مرگ برده می‌شود. 14
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
خانه‌اش در زیر آتش گوگرد نابود می‌گردد. 15
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
ریشه و شاخه‌هایش می‌خشکند و از بین می‌روند. 16
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
خاطرهٔ وجود او تمام از روی زمین محو می‌گردد و هیچ‌کس او را به یاد نمی‌آورد. 17
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
از دنیای زندگان بیرون انداخته شده، از نور به تاریکی رانده می‌شود. 18
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
در میان قومش نسلی از او باقی نمی‌ماند. 19
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
قومهای مغرب و مشرق از سرنوشت او حیران و هراسان می‌شوند. 20
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
آری، این بلایی است که بر سر گناهکاران می‌آید، بر سر آنانی که خدا را نمی‌شناسند. 21
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

< ایوب 18 >