< ایوب 18 >
آنگاه بلدد شوحی پاسخ داد: | 1 |
Bildadi Mshuhi akajibu:
تا کی میخواهی به این حرفها ادامه دهی؟ اگر میخواهی ما هم سخن بگوییم قدری عاقلانهتر صحبت کن. | 2 |
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
آیا تو فکر میکنی ما مثل حیوان بیشعور هستیم؟ | 3 |
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
چرا بیجهت خشمگین میشوی و به خود صدمه میزنی؟ آیا انتظار داری به خاطر تو زمین بلرزد و صخرهها واژگون شوند. | 4 |
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
چراغ مرد بدکار خاموش خواهد شد و شعلهاش نوری نخواهد داد. | 5 |
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
در هر خانهای که شرارت وجود داشته باشد، تاریکی حکمفرما خواهد بود. | 6 |
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
قدمهای شرور سست میشوند و او قربانی نقشههای خود میگردد. | 7 |
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
او با پای خود به دام میافتد و تله پاشنهٔ پای او را میگیرد و او را رها نمیکند. | 8 |
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
سر راه او تلهها پنهان شده است. | 10 |
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
ترسها از هر طرف به او هجوم میآورند و او را قدم به قدم تعقیب میکنند. | 11 |
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
مصیبت دهان خود را برای او باز کرده و فلاکت آماده است تا او را به کام خود فرو برد. | 12 |
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
مرض مهلک به جان او میافتد و او را به کام مرگ میکشاند. | 13 |
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
از خانهٔ امن خود جدا شده، نزد پادشاه مرگ برده میشود. | 14 |
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
خانهاش در زیر آتش گوگرد نابود میگردد. | 15 |
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
ریشه و شاخههایش میخشکند و از بین میروند. | 16 |
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
خاطرهٔ وجود او تمام از روی زمین محو میگردد و هیچکس او را به یاد نمیآورد. | 17 |
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
از دنیای زندگان بیرون انداخته شده، از نور به تاریکی رانده میشود. | 18 |
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
در میان قومش نسلی از او باقی نمیماند. | 19 |
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
قومهای مغرب و مشرق از سرنوشت او حیران و هراسان میشوند. | 20 |
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
آری، این بلایی است که بر سر گناهکاران میآید، بر سر آنانی که خدا را نمیشناسند. | 21 |
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”