< ایوب 14 >
انسان چقدر ناتوان است. عمرش کوتاه و پر از زحمت است. | 1 |
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
مثل گل، لحظهای میشکفد و زود پژمرده میشود و همچون سایهٔ ابری که در حرکت است به سرعت ناپدید میگردد. | 2 |
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
ای خدا، آیا با انسانهای ضعیف بایستی اینچنین سختگیری کنی و از آنها بخواهی تا حساب پس دهند؟ | 3 |
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
چطور انتظار داری از یک چیز کثیف چیز پاکی بیرون آید؟ | 4 |
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
روزهای عمر او را از پیش تعیین کردهای و او قادر نیست آن را تغییر دهد. | 5 |
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
پس نگاه غضبآلود خود را از وی برگردان و او را به حال خود بگذار تا پیش از آنکه بمیرد چند صباحی در آرامش زندگی کند. | 6 |
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
برای درخت امیدی هست، چون اگر بریده شود باز سبز میشود و شاخههای تر و تازه میرویاند. | 7 |
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
اگر ریشههایش در زمین فرسوده شود و کندهاش بپوسد، باز مانند نهال تازه نشاندهای به مجرد رسیدن آب از نو جوانه زده، شکوفه میآورد. | 8 |
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
ولی وقتی انسان میمیرد، رمقی در او باقی نمیماند. دم آخر را برمیآورد و اثری از او باقی نمیماند. | 10 |
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
همانطور که آب دریا بخار میگردد و آب رودخانه در خشکسالی ناپدید میشود، همچنان انسان برای همیشه بخواب میرود و تا نیست شدن آسمانها دیگر برنمیخیزد و کسی او را بیدار نمیکند. | 11 |
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
ای کاش مرا تا زمانی که خشمگین هستی در کنار مردگان پنهان میکردی و پس از آن دوباره به یاد میآوردی. (Sheol ) | 13 |
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol )
وقتی انسان بمیرد، آیا دوباره زنده میشود؟ من در تمام روزهای سخت زندگی در انتظار مرگ و خلاصی خود خواهم بود. | 14 |
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
آنگاه تو مرا صدا خواهی کرد و من جواب خواهم داد؛ و تو مشتاق این مخلوق خود خواهی شد. | 15 |
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
مواظب قدمهایم خواهی بود و گناهانم را از نظر دور خواهی داشت. | 16 |
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
تو خطاهای مرا خواهی پوشاند و گناهانم را پاک خواهی نمود. | 17 |
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
کوهها فرسوده و ناپدید میشوند. آب، سنگها را خرد میکند و به صورت شن درمیآورد. سیلابها خاک زمین را میشوید و با خود میبرد. به همین گونه تو امید انسان را باطل میسازی. | 18 |
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
او را از توان میاندازی و پیر و فرتوت به کام مرگ میفرستی. | 20 |
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
اگر پسرانش به عزت و افتخار برسند او از آنها اطلاع نخواهد داشت و اگر به ذلت و خواری بیفتند از آن نیز بیخبر خواهد بود. | 21 |
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
نصیب انسان فقط اندوه و درد است. | 22 |
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”