< اشعیا 32 >

زمانی خواهد رسید که پادشاهی عادل بر تخت سلطنت خواهد نشست و رهبرانی با انصاف مملکت را اداره خواهند کرد. 1
Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu na watawala watatawala kwa haki.
هر یک از آنان پناهگاهی در برابر باد و طوفان خواهد بود. آنان مانند جوی آب در بیابان خشک، و مثل سایهٔ خنک یک صخرهٔ بزرگ در زمین بی‌آب و علف خواهند بود؛ 2
Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo na kimbilio kutokana na dhoruba, kama vijito vya maji jangwani na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.
و چشم و گوش خود را نسبت به نیازهای مردم باز نگه خواهند داشت. 3
Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.
آنان بی‌حوصله نخواهند بود بلکه با فهم و متانت با مردم سخن خواهند گفت. 4
Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa, nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.
در آن زمان، افراد پست و خسیس دیگر سخاوتمند و نجیب خوانده نخواهند شد. 5
Mpumbavu hataitwa tena muungwana, wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.
هر که شخص بدکاری را ببیند، او را خواهد شناخت و کسی فریب آدمهای ریاکار را نخواهد خورد؛ بر همه آشکار خواهد شد که سخنان آنان در مورد خداوند دروغ بوده و آنان هرگز به گرسنگان کمک نکرده‌اند. 6
Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu, moyo wake hushughulika na uovu: Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu, na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana; yeye huwaacha wenye njaa bila kitu, na wenye kiu huwanyima maji.
نیرنگ و چاپلوسی اشخاص شرور و دروغهایی که آنان برای پایمال کردن حق فقیران در دادگاه می‌گویند، افشا خواهد گردید. 7
Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu, hufanya mipango miovu ili kumwangamiza maskini kwa uongo, hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.
اما اشخاص خوب در حق دیگران بخشنده و باگذشت خواهند بود و خدا ایشان را به خاطر کارهای خوبشان برکت خواهد داد. 8
Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana, na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.
ای زنانی که راحت و آسوده زندگی می‌کنید، به من گوش دهید. 9
Enyi wanawake wenye kuridhika sana, amkeni na mnisikilize. Enyi binti mnaojisikia kuwa salama, sikieni lile ninalotaka kuwaambia!
شما که الان بی‌غم هستید، سال دیگر همین موقع پریشانحال خواهید شد، زیرا محصول انگور و سایر میوه‌هایتان از بین خواهد رفت. 10
Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja, ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka, mavuno ya zabibu yatakoma na mavuno ya matunda hayatakuwepo.
ای زنان آسوده خیال، بترسید و بلرزید، لباسهای خود را از تن درآورید و رخت عزا بپوشید 11
Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika, tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama! Vueni nguo zenu, vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.
و ماتم بگیرید، زیرا مزرعه‌های پر محصولتان به‌زودی از دست می‌روند و باغهای بارور انگورتان نابود می‌شوند. 12
Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri
بله، ای قوم من، برای خانه‌های شادتان و برای شهر پر افتخارتان گریه کنید، زیرا سرزمین شما پوشیده از خار و خس خواهد شد. 13
na kwa ajili ya nchi ya watu wangu, nchi ambayo miiba na michongoma imemea: naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.
کاخهایتان ویران و شهرهای پر جمعیت‌تان خالی از سکنه خواهند شد. برجهای دیدبانی‌تان خراب خواهند شد و حیوانات وحشی و گورخران و گوسفندان در آنجا خواهند چرید. 14
Ngome itaachwa, mji wenye kelele nyingi utahamwa, ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele, mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,
اما یک بار دیگر، خدا روح خود را از آسمان بر ما خواهد ریخت. آنگاه بیابان به بوستان تبدیل خواهد شد و بوستان به جنگل. 15
mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu, nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.
انصاف بر بیابان حکفرما خواهد شد و عدالت بر بوستان. 16
Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
و ما از صلح و آرامش و اطمینان و امینت همیشگی برخوردار خواهیم شد. 17
Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.
قوم خدا در کمال امنیت و آسایش در خانه‌هایشان زندگی خواهند کرد. 18
Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
حتی جنگل از بارش تگرگ صاف خواهد شد و شهر با خاک یکسان خواهد گردید. 19
Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,
بله، خدا قوم خود را برکت خواهد داد آن گونه که به هنگام کشت زمین، محصول فراوان خواهد رویید و گله‌ها و رمه‌هایشان در چراگاههای سبز و خرم خواهند چرید. 20
tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.

< اشعیا 32 >