< پیدایش 30 >

راحیل وقتی فهمید نازاست، به خواهر خود حسد برد. او به یعقوب گفت: «به من فرزندی بده، اگر نه خواهم مرد!» 1
Raheli alipoona hamzalii Yakobo watoto, akamwonea ndugu yake wivu. Hivyo akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, la sivyo nitakufa!”
یعقوب خشمگین شد و گفت: «مگر من خدا هستم که به تو فرزند بدهم؟ اوست که تو را نازا گردانیده است.» 2
Yakobo akamkasirikia, akamwambia, “Je, mimi ni badala ya Mungu, ambaye amekuzuia usizae watoto?”
راحیل به او گفت: «با کنیزم بلهه همبستر شو تا از طریق او صاحب فرزندان شوم.» 3
Ndipo Raheli akamwambia, “Hapa yupo Bilha, mtumishi wangu wa kike. Kutana naye kimwili ili aweze kunizalia watoto na kwa kupitia yeye mimi pia niweze kuwa na uzao.”
پس کنیز خود بِلهه را به همسری به یعقوب داد و او با وی همبستر شد. 4
Hivyo Raheli akampa Yakobo Bilha awe mke wake. Yakobo akakutana naye kimwili,
بلهه حامله شد و پسری برای یعقوب زایید. 5
Bilha akapata mimba, naye akamzalia Yakobo mwana.
راحیل گفت: «خدا دعایم را شنیده و به دادم رسیده و اینک پسری به من بخشیده است»، پس او را دان (یعنی «دادرسی») نامید. 6
Ndipo Raheli akasema, “Mungu amenipa haki yangu, amesikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita Dani.
بلهه باز آبستن شد و دومین پسر را برای یعقوب زایید. 7
Bilha mtumishi wa kike wa Raheli akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
راحیل گفت: «من با خواهر خود سخت مبارزه کردم و بر او پیروز شدم»، پس او را نفتالی نامید. 8
Ndipo Raheli akasema, “Nilikuwa na mashindano makubwa na ndugu yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita Naftali.
وقتی لیه دید که دیگر حامله نمی‌شود، کنیز خود زلفه را به یعقوب به زنی داد. 9
Lea alipoona kuwa amekoma kuzaa watoto, alimchukua mtumishi wake wa kike Zilpa, naye akampa Yakobo awe mke wake.
زلفه برای یعقوب پسری زایید. 10
Mtumishi wa Lea yaani Zilpa, akamzalia Yakobo mwana.
لیه گفت: «خوشبختی به من روی آورده است»، پس او را جاد نامید. 11
Ndipo Lea akasema, “Hii ni bahati nzuri aje!” Kwa hiyo akamwita Gadi.
سپس زلفه دومین پسر را برای یعقوب زایید. 12
Mtumishi wa kike wa Lea akamzalia Yakobo mwana wa pili.
لیه گفت: «چقدر خوشحال هستم! اینک زنان مرا زنی خوشحال خواهند دانست.» پس او را اَشیر نامید. 13
Ndipo Lea aliposema, “Jinsi gani nilivyo na furaha! Wanawake wataniita furaha.” Kwa hiyo akamwita Asheri.
روزی هنگام درو گندم، رئوبین مقداری مِهرگیاه که در کشتزاری روییده بود، یافت و آن را برای مادرش لیه آورد. راحیل از لیه خواهش نمود که مقداری از آن را به وی بدهد. 14
Wakati wa kuvuna ngano, Reubeni akaenda shambani akakuta tunguja, ambazo alizileta kwa Lea mama yake. Raheli akamwambia Lea, “Tafadhali nakuomba unipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
اما لیه به او جواب داد: «کافی نیست که شوهرم را از دستم گرفتی، حالا می‌خواهی مِهرگیاه پسرم را هم از من بگیری؟» راحیل گفت: «اگر مِهرگیاه پسرت را به من بدهی، من هم اجازه می‌دهم امشب با یعقوب بخوابی.» 15
Lakini Lea akamwambia, “Haikukutosha kumtwaa mume wangu? Je, utachukua na tunguja za mwanangu pia?” Raheli akasema, “Vema sana! Yakobo atakutana nawe kimwili leo usiku, kwa malipo ya tunguja za mwanao.”
آن روز عصر که یعقوب از صحرا برمی‌گشت، لیه به استقبال وی شتافت و گفت: «امشب باید با من بخوابی، زیرا تو را در مقابل مِهر گیاهی که پسرم یافته است، اجیر کرده‌ام!» پس یعقوب آن شب با وی همبستر شد. 16
Kwa hiyo Yakobo alipokuja kutoka shambani jioni ile, Lea akaenda kumlaki, akamwambia, “Lazima ukutane nami kimwili. Nimekukodisha kwa tunguja za mwanangu.” Kwa hiyo akakutana naye kimwili usiku ule.
خدا دعاهای وی را اجابت فرمود و او حامله شده، پنجمین پسر خود را زایید. 17
Mungu akamsikiliza Lea, naye akapata mimba akamzalia Yakobo mwana wa tano.
لیه گفت: «چون کنیز خود را به شوهرم دادم، خدا به من پاداش داده است.» پس او را یساکار نامید. 18
Ndipo Lea akasema, “Mungu amenizawadia kwa kumpa mume wangu mtumishi wangu wa kike.” Kwa hiyo akamwita Isakari.
او بار دیگر حامله شده، ششمین پسر را برای یعقوب زایید، 19
Lea akapata mimba tena akamzalia Yakobo mwana wa sita.
و گفت: «خدا به من هدیه‌ای نیکو داده است. از این پس شوهرم مرا احترام خواهد کرد، زیرا برایش شش پسر زاییده‌ام.» پس او را زبولون (یعنی «احترام») نامید. 20
Ndipo Lea aliposema, “Mungu amenizawadia kwa zawadi ya thamani sana. Wakati huu mume wangu ataniheshimu kwa sababu nimemzalia wana sita.” Kwa hiyo akamwita Zabuloni.
مدتی پس از آن دختری زایید و او را دینه نامید. 21
Baadaye akamzaa mtoto wa kike akamwita Dina.
سپس خدا راحیل را به یاد آورد و دعای وی را اجابت نموده، فرزندی به او بخشید. 22
Ndipo Mungu akamkumbuka Raheli, akasikia maombi yake na akafungua tumbo lake.
او حامله شده، پسری زایید و گفت: «خدا این ننگ را از من برداشته است.» 23
Akapata mimba na akamzaa mwana na kusema, “Mungu ameniondolea aibu yangu.”
سپس افزود: «ای کاش خداوند پسر دیگری هم به من بدهد!» پس او را یوسف نامید. 24
Akamwita Yosefu na kusema, “Bwana na anipe mwana mwingine.”
بعد از آنکه راحیل یوسف را زایید، یعقوب به لابان گفت: «قصد دارم به وطن خویش بازگردم. 25
Baada ya Raheli kumzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani, “Nipe ruhusa nirudi katika nchi yangu.
اجازه بده زنان و فرزندانم را برداشته با خود ببرم، چون می‌دانی با خدمتی که به تو کرده‌ام بهای آنها را تمام و کمال به تو پرداخته‌ام.» 26
Nipe wake zangu na watoto, ambao nimetumika kuwapata, nami niende zangu. Unajua ni kazi kiasi gani ambayo nimekufanyia.”
لابان به وی گفت: «خواهش می‌کنم مرا ترک نکن، زیرا از روی فال فهمیده‌ام که خداوند به خاطر تو مرا برکت داده است. 27
Lakini Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, tafadhali ukae. Nimegundua kwa njia ya uaguzi kwamba Bwana amenibariki kwa sababu yako.”
هر چقدر مزد بخواهی به تو خواهم داد.» 28
Akaongeza kumwambia, “Taja ujira wako nami nitakulipa.”
یعقوب جواب داد: «خوب می‌دانی که طی سالیان گذشته با چه وفاداری به تو خدمت نموده‌ام و چگونه از گله‌هایت مواظبت کرده‌ام. 29
Yakobo akamwambia, “Unajua jinsi ambavyo nimekutumikia na jinsi ambavyo wanyama wako walivyolishwa vizuri chini ya uangalizi wangu.
قبل از اینکه پیش تو بیایم، گله و رمهٔ چندانی نداشتی ولی اکنون اموالت بی‌نهایت زیاد شده است. خداوند به خاطر من از هر نظر به تو برکت داده است. اما من الان باید به فکر خانوادهٔ خود باشم و برای آنها تدارک ببینم.» 30
Kidogo ulichokuwa nacho kabla sijaja kimeongezeka sana, naye Bwana amekubariki popote nilipokuwa. Lakini sasa, ni lini nitashughulikia mambo ya nyumba yangu mwenyewe?”
لابان بار دیگر پرسید: «چقدر مزد می‌خواهی؟» یعقوب پاسخ داد: «لازم نیست چیزی به من بدهی. فقط این یک کار را برای من بکن و من باز از گله‌هایت مراقبت خواهم کرد. 31
Labani akamuuliza, “Nikupe nini?” Yakobo akamjibu, “Usinipe chochote lakini kama utanifanyia jambo hili moja, nitaendelea kuchunga na kuyaangalia makundi yako.
اجازه بده امروز به میان گله‌های تو بروم و تمام گوسفندان ابلق و خالدار و تمام بره‌های سیاه رنگ و همهٔ بزهای ابلق و خالدار را به جای اجرت برای خود جدا کنم. اینها مزد من خواهد بود. 32
Niruhusu nipite katika makundi yako yote leo niondoe humo kila kondoo mwenye mabakabaka au madoadoa, kila mwana-kondoo mweusi na kila mbuzi mwenye madoadoa au mabakabaka. Hawa watakuwa ujira wangu.
از آن به بعد، اگر حتی یک بز یا گوسفند سفید در میان گلهٔ من یافتی، بدان که من آن را از تو دزدیده‌ام.» 33
Uadilifu wangu utanishuhudia siku zijazo, kila utakapochunguza ujira ambao umenilipa mimi. Mbuzi yeyote wangu ambaye hana mabakabaka wala madoadoa, au mwana-kondoo ambaye si mweusi, atahesabika ameibwa.”
لابان گفت: «آنچه را که گفتی قبول می‌کنم.» 34
Labani akasema, “Ninakubali na iwe kama ulivyosema.”
پس همان روز لابان تمام بزهای نری که خطّدار و خالدار بودند و بزهای ماده‌ای که ابلق و خالدار بودند و تمامی بره‌های سیاه رنگ را جدا کرد و به پسرانش سپرد. 35
Siku ile ile Yakobo akawaondoa beberu wote waliokuwa na mistari au madoadoa na mbuzi wake wote waliokuwa na mistari au madoadoa (wote waliokuwa na alama nyeupe juu yao) na wana-kondoo weusi wote, akawaweka chini ya uangalizi wa wanawe.
آنگاه آنها را به فاصلهٔ سه روز راه از یعقوب دور کرد. درضمن، خود یعقوب در آنجا ماند تا بقیهٔ گلهٔ لابان را بچراند. 36
Kisha Labani akamwacha Yakobo kwa mwendo wa safari ya siku tatu kati yake na Yakobo, wakati Yakobo akiendelea kuchunga lile kundi la Labani lililobaki.
آنگاه یعقوب شاخه‌های سبز و تازهٔ درختان بید و بادام و چنار را کَند و خطّهای سفیدی بر روی آنها تراشید. 37
Hata hivyo, Yakobo, akachukua fito mbichi zilizokatwa wakati huo huo za miti ya mlubna, mlozi na mwaramoni akazibambua ili mistari myeupe ionekane katika fito hizo.
این چوبها را در کنار آبشخور قرار داد تا وقتی که گله‌ها برای خوردن آب می‌آیند، آنها را ببینند. وقتی گله‌ها برای خوردن آب می‌آمدند، و می‌خواستند جفتگیری کنند، 38
Kisha akaweka fito alizozibambua kwenye mabirika yote ya kunyweshea mifugo, ili ziwe mbele ya makundi walipokuja kunywa maji. Wanyama walipokuja kunywa maji, hali wakiwa wanahitaji mbegu,
جلوی چوبها با یکدیگر جفتگیری می‌کردند و بره‌هایی می‌زاییدند که خطّدار، خالدار و ابلق بودند. 39
wakapandwa hizo fito zikiwa mbele yao. Wanyama waliopata mimba mbele ya hizo fito walizaa wanyama wenye mistari, madoadoa na mabakabaka.
یعقوب، این برّه‌ها را از گلهٔ لابان جدا می‌کرد و به گلهٔ خود می‌افزود. به این ترتیب او با استفاده از گلهٔ لابان، گلهٔ خودش را بزرگ می‌کرد. 40
Yakobo akawatenga wadogo wa kundi peke yao, lakini akazielekeza nyuso za hao waliobaki kwenye wale wenye mistari na weusi waliokuwa mali ya Labani. Hivyo akatenga makundi yake mwenyewe, na wala hakuwachanganya na wanyama wa Labani.
در ضمن هرگاه حیوانات مادهٔ قوی می‌خواستند جفتگیری کنند، یعقوب چوبها را در آبشخور جلوی آنها قرار می‌داد تا کنار آنها جفتگیری کنند. 41
Kila mara wanyama wenye nguvu walipohitaji mbegu, Yakobo aliweka zile fito kwenye mabirika mbele ya hao wanyama, ili wapandwe karibu na hizo fito,
ولی اگر حیوانات ضعیف بودند، چوبها را در آنجا نمی‌گذاشت. بنابراین حیوانات ضعیف از آنِ لابان و حیوانات قوی از آن یعقوب می‌شدند. 42
lakini ikiwa wanyama walikuwa wadhaifu hakuziweka hizo fito. Hivyo wanyama wadhaifu wakawa wa Labani, na wanyama wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
بدین ترتیب یعقوب بسیار ثروتمند شد و صاحب کنیزان و غلامان، گله‌های بزرگ، شترها و الاغهای زیادی گردید. 43
Kwa njia hii Yakobo akastawi sana, tena akawa na makundi makubwa, watumishi wa kike na wa kiume na ngamia na punda.

< پیدایش 30 >