< خروج 39 >

سپس برای کاهنان از نخهای آبی، ارغوانی و قرمز لباسهایی بافتند. این لباسها را موقع خدمت در قدس می‌پوشیدند. لباس مقدّس هارون کاهن هم طبق دستوری که خداوند به موسی داده بود، تهیه شد. 1
Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
ایفود کاهن از کتان ریزبافت تابیده و نخهای آبی، ارغوانی و قرمز و رشته‌هایی از طلا درست شد. 2
Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
آنها ورقه‌های طلا را چکش زدند تا باریک شد، سپس آنها را بریده، به صورت رشته‌هایی درآوردند و با نخهای آبی، ارغوانی و قرمز و کتان ریزبافت در تهیه ایفود به کار بردند و روی ایفود را با دقت گلدوزی کردند. 3
Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
ایفود از دو قسمت، جلو و پشت، تهیه شد و با دو بند روی شانه‌ها، به هم وصل گردید. 4
Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
همان‌طور که خداوند به موسی دستور داده بود، بند کمر ایفود متصل به آن و از جنس خود ایفود بود، یعنی از رشته‌های طلا و کتان ریز‌بافت تابیده و نخهای آبی، ارغوانی و قرمز. 5
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
دو سنگ جزع در قابهای طلا گذاشتند و نامهای قبیلهٔ بنی‌اسرائیل را با مهارتی خاص روی آن دو قطعه سنگ حک کردند. 6
Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
سپس آنها را روی بندهای شانه‌های ایفود نصب کردند تا نشان دهد که کاهن نمایندۀ بنی‌اسرائیل است. همهٔ این کارها طبق دستوری که خداوند به موسی داد، انجام گرفت. 7
Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
سینه‌پوش را مثل ایفود از کتان ریزبافت تابیده، نخهای آبی، ارغوانی و قرمز، و رشته‌های طلا تهیه نموده، روی آن را با دقت گلدوزی کردند. 8
Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
آن را دولا، مثل یک کیسهٔ چهارگوش دوختند که طول هر ضلعش یک وجب بود. 9
Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
چهار ردیف سنگ قیمتی روی آن نصب شد. در ردیف اول، عقیق سرخ و یاقوت زرد و یاقوت آتشی بود. 10
Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
در ردیف دوم، زمرد و یاقوت کبود و الماس بود. 11
safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
در ردیف سوم، فیروزه و عقیق یمانی و یاقوت بنفش 12
safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
و در ردیف چهارم، زبرجد و جزع و یشم نصب شد. همهٔ این سنگهای قیمتی را در قابهای طلا جای دادند. 13
katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
هر یک از این سنگها علامت یکی از دوازده قبیلهٔ بنی‌اسرائیل بود و نام آن قبیله روی آن سنگ حک شد. 14
Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
برای نصب سینه‌پوش به ایفود دو رشته زنجیر تابیده از طلای خالص درست کردند. 15
Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
همچنین دو قاب و دو حلقه از طلا ساختند و حلقه‌ها 16
Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
و قسمت بالای سینه‌پوش را به‌وسیلۀ دو رشته زنجیر طلا به ایفود بستند. دو سر زنجیرها به حلقه‌های طلا که در گوشه‌های سینه‌پوش جاسازی شده بود، بسته شد، و دو سر دیگر زنجیرها را از جلو به قابهای طلای روی شانه‌ها وصل کردند. 17
Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
18
nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
دو حلقهٔ طلای دیگر نیز درست کردند و آنها را به دو گوشهٔ پایین سینه‌پوش، روی لایهٔ زیرین بستند. 19
Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
دو حلقه طلای دیگر هم درست کردند و آنها را در قسمت جلوی ایفود و کمی بالاتر از بند کمر نصب کردند. 20
Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
بعد، همان‌طور که خداوند به موسی فرموده بود، حلقه‌های سینه‌پوش را با نوار آبی رنگ به حلقه‌های ایفود که بالاتر از بند کمر قرار داشت بستند تا سینه‌پوش از ایفود جدا نشود. 21
Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
ردایی که زیر ایفود پوشیده می‌شد، تمام از پارچهٔ آبی تهیه شد. 22
Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
شکافی برای سر در آن باز کردند و حاشیهٔ شکاف را با دست بافتند تا پاره نشود. 23
na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
با نخهای آبی، ارغوانی و قرمز و کتان ریزبافت منگوله‌هایی به شکل انار درست کردند و آنها را دور تا دور لبهٔ دامن ردا آویختند. 24
Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
زنگوله‌هایی از طلای خالص نیز ساختند و دور دامن ردا میان انارها بستند. 25
Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
زنگوله‌ها و انارها یکی در میان دور دامن ردایی بود که هنگام خدمت می‌پوشیدند؛ همان‌طور که خداوند به موسی فرموده بود. 26
Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
آنها از کتان ریزبافت برای هارون و پسرانش پیراهنها دوختند. 27
Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
دستار و کلاه‌ها از کتان ریزبافت تهیه کردند و لباسهای زیر نیز از کتان ریزبافت تابیده بود. 28
na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
شال کمر را از کتان ریزبافت تابیده تهیه نموده، آن را با نخهای آبی، ارغوانی و قرمز گلدوزی کردند، همان‌طور که خداوند به موسی فرموده بود. 29
Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
نیم تاج مقدّس را از طلای خالص ساختند و این کلمات را روی آن نقش کردند: «مقدّس برای خداوند.» 30
Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
همان‌طور که خداوند به موسی گفته بود، نیم تاج را با یک نوار آبی رنگ به قسمت جلوی دستار بستند. 31
Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
سرانجام تمام قسمتها و لوازم خیمهٔ ملاقات طبق آنچه خداوند به موسی فرموده بود به‌وسیلۀ بنی‌اسرائیل آماده شد. 32
Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
سپس ایشان قسمتهای ساخته شده خیمه و همهٔ لوازم آن را پیش موسی آوردند: تکمه‌ها، چوب‌بست خیمه، پشت‌بندها، ستونها، پایه‌ها؛ 33
Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
پوشش از پوست سرخ شدهٔ قوچ و پوشش از پوست خز، پردهٔ حایل بین قدس و قدس‌الاقداس؛ 34
kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
صندوق عهد و ده فرمان خدا که در آن بود و چوبهای حامل آن، تخت رحمت؛ 35
Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
میز و تمام وسایل آن، نان حضور؛ 36
meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
چراغدان طلای خالص با چراغها، روغن و همهٔ لوازم آن؛ 37
kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
مذبح طلایی، روغن تدهین و بخور معطر؛ پردهٔ مدخل خیمه؛ 38
madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
مذبح مفرغین با منقل مشبک مفرغین و چوبهای حامل و سایر لوازم آن؛ حوض و پایه‌اش؛ 39
madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
پرده‌های دور حیاط با ستونها و پایه‌های آنها، پردهٔ مدخل حیاط؛ طنابها و میخهای خیمۀ ملاقات، و تمام ابزارهایی که در ساختن خیمه به کار می‌رفت. 40
mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
آنها همچنین لباسهای بافته شده برای خدمت در قدس یعنی لباسهای مقدّس هارون کاهن و پسرانش را از نظر موسی گذراندند. 41
na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
به این ترتیب بنی‌اسرائیل تمام دستورهای خداوند را که برای ساختن خیمه به موسی داده بود، به کار بستند. 42
Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
موسی تمام کارهای انجام شده را ملاحظه کرد و به خاطر آن، قوم را برکت داد، چون همه چیز مطابق دستور خداوند ساخته شده بود. 43
Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

< خروج 39 >