< خروج 37 >
بِصَلئیل، صندوق عهد را از چوب اقاقیا که درازای آن یک متر و ۲۵ سانتی متر و پهنا و بلندی آن هر کدام هفتاد و پنج سانتی متر بود، ساخت. | 1 |
Bezaleli akafanya Sanduku la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
بیرون و درون آن را با طلای خالص پوشانید و نواری از طلا دور لبهٔ آن کشید. | 2 |
Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
برای صندوق چهار حلقه از طلا آماده کرد و آنها را در چهار گوشهٔ قسمت پایین آن متصل نمود، یعنی در هر طرف دو حلقه. | 3 |
Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine
سپس دو چوب بلند از درخت اقاقیا ساخت و آنها را با طلا پوشاند. | 4 |
Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
برای برداشتن و حمل صندوق، چوبها را در داخل حلقههای دو طرف صندوق گذاشت. | 5 |
Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.
سرپوش صندوق یعنی تخت رحمت را به درازای یک متر و ده سانتیمتر و پهنای هفتاد سانتیمتر، از طلای خالص درست کرد. | 6 |
Naye akafanya kifuniko cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.
سپس دو مجسمهٔ کروبی از طلا بر دو سر تخت رحمت ساخت. | 7 |
Bezaleli akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.
کروبیها را بر دو سر تخت رحمت طوری قرار داد که با آن یکپارچه شد. | 8 |
Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.
مجسمهٔ کروبیها، روبروی هم و نگاهشان به طرف تخت و بالهایشان بر بالای آن گسترده بود. | 9 |
Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao, nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.
آنگاه بِصَلئیل، میز نان حضور را از چوب اقاقیا به درازای یک متر و پهنای نیم متر و بلندی ۷۵ سانتی متر ساخت. | 10 |
Bezaleli akafanya meza ya mbao za mshita. Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
آن را با روکشی از طلای خالص پوشانید و قابی از طلا بر دور تا دور لبهٔ آن نصب کرد. | 11 |
Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
حاشیهٔ دور لبهٔ میز را به پهنای چهار انگشت درست کرد و دور حاشیه را با قاب طلا پوشانید. | 12 |
Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.
همچنین چهار حلقه از طلا برای میز ساخت و حلقهها را به چهار گوشهٔ بالای پایههای میز نصب کرد. | 13 |
Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.
این حلقهها برای چوبهایی بود که به هنگام برداشتن و جابهجا کردن میز میبایست در آنها قرار گیرد. | 14 |
Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.
این چوبها را از درخت اقاقیا با روکش طلا ساخت. | 15 |
Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.
همچنین بشقابها، کاسهها، جامها و پیالههایی از طلای خالص برای ریختن هدایای نوشیدنی درست کرد تا آنها را روی میز بگذارند. | 16 |
Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.
چراغدان را نیز از طلای خالص درست کرد. پایه و بدنهٔ آن را یکپارچه و از طلای خالص ساخت و نقش گلهای روی آن را نیز که شامل کاسبرگ و غنچه بود از طلا درست کرد. | 17 |
Kisha akafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.
بر بدنهٔ چراغدان شش شاخه قرار داشت، یعنی در هر طرف سه شاخه. | 18 |
Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.
روی هر شش شاخه که از چراغدان بیرون میآمد، گلهای بادام با جوانهها وغنچههای مربوط به آن قرار داشت. | 19 |
Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.
خود بدنه چراغدان با چهار گل بادامی شکل با جوانهها و غنچههایش تزیین شده بود. | 20 |
Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.
یک جوانه زیر هر جفت شاخه بود جایی که شش شاخه از بدنۀ چراغدان بیرون میآمد و همه یکپارچه بود. | 21 |
Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.
تمام این نقشها و شاخهها و بدنه از یک تکه طلای خالص بود. | 22 |
Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake, vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.
هفت چراغ آن و انبرها و سینیهایش را از طلای خالص ساخت. | 23 |
Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.
برای ساختن این چراغدان و لوازمش سی و چهار کیلو طلا به کار رفت. | 24 |
Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.
مذبح بخور را به شکل مربع به ضلع نیم متر و بلندی یک متر از چوب اقاقیا درست کرد. آن را طوری ساخت که در چهار گوشهٔ آن چهار برجستگی به شکل شاخ بود. | 25 |
Sasa akafanya madhabahu ya uvumba kutokana na mbao za mshita. Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.
روکش مذبح و شاخهای آن از طلای خالص بود. قابی دور تا دور آن از طلا درست کرد. | 26 |
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
در دو طرف مذبح، زیر قاب طلایی، دو حلقه از طلا برای قرار گرفتن چوبها ساخت تا با آنها مذبح را حمل کنند. | 27 |
Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.
این چوبها از درخت اقاقیا تهیه شده بود و روکش طلا داشت. | 28 |
Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
سپس روغن مسح مقدّس و بخور خالص معطر را با مهارت عطّاران تهیه کرد. | 29 |
Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba safi uliotiwa manukato, kazi ya mtengenezaji wa marhamu.