< خروج 35 >

موسی تمام قوم اسرائیل را دور خود جمع کرد و به ایشان گفت: «این است دستورهایی که خداوند به شما داده است تا از آن اطاعت کنید: 1
Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
فقط شش روز کار کنید و روز هفتم را که روز مقدّس خداوند است استراحت و عبادت نمایید. هر کس که در روز هفتم کار کند باید کشته شود. 2
Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
آن روز در خانه‌هایتان حتی آتش هم روشن نکنید.» 3
Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
سپس موسی به قوم اسرائیل گفت: «خداوند فرموده که 4
Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
از آنچه دارید برای او هدیه بیاورید. هدایای کسانی که از صمیم قلب به خداوند هدیه می‌دهند باید شامل این چیزها باشد: طلا، نقره، مفرغ؛ 5
Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
نخهای آبی، ارغوانی و قرمز؛ کتان ریزبافت؛ پشم بز؛ 6
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
پوست قوچ که رنگش سرخ شده باشد و پوست خز؛ چوب اقاقیا؛ 7
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
روغن زیتون برای چراغها؛ مواد خوشبو برای تهیهٔ روغن مسح؛ بخور خوشبو؛ 8
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
سنگ جزع و سنگهای قیمتی دیگر برای ایفود و سینه‌پوش کاهن. 9
vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
«شما ای صنعتگران ماهر، بیایید و آنچه را که خداوند امر فرموده است، بسازید: 10
“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
خیمهٔ عبادت و پوششهای آن، تکمه‌ها، چوب‌بست خیمه، پشت‌بندها، ستونها و پایه‌ها؛ 11
Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
صندوق عهد و چوبهای حامل آن، تخت رحمت، پردهٔ حایل بین قدس و قدس‌الاقداس؛ 12
Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
میز و چوبهای حامل آن و تمام ظروف آن، نان حضور؛ 13
meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
چراغدان با چراغها و روغن و لوازم دیگر آن؛ 14
kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
مذبح بخور و چوبهای حامل آن، روغن تدهین و بخور خوشبو؛ پردهٔ مدخل خیمه؛ 15
madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
مذبح قربانی سوختنی، منقل مشبک مفرغین مذبح و چوبهای حامل با تمام لوازم آن؛ حوض مفرغین با پایهٔ آن؛ 16
madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
پرده‌های دور حیاط، ستونها و پایه‌های آنها، پردهٔ مدخل حیاط؛ 17
pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
میخهای خیمه و حیاط خیمه و طنابهای آن؛ 18
vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
لباسهای بافته شده برای خدمت در قدس یعنی لباس مقدّس هارون کاهن و لباسهای پسرانش.» 19
mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
پس تمام قوم اسرائیل از نزد موسی رفتند، 20
Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
اما کسانی که تحت تأثیر قرار گرفته بودند با اشتیاق بازگشتند و هدایایی برای آماده ساختن لباسهای مقدّس، خیمۀ ملاقات و وسایل مورد نیاز جهت خدمت در آن، با خود آوردند تا به خداوند تقدیم کنند. 21
na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
مردان و زنان با اشتیاق زیاد آمدند و جواهراتی از قبیل سنجاق، گوشواره، انگشتر، گردنبند و اشیاء دیگری از طلا را به خداوند تقدیم کردند. 22
Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
برخی نیز نخهای آبی، ارغوانی و قرمز؛ کتان ریزبافت؛ پشم بز؛ پوست سرخ شدهٔ قوچ و پوست خز آوردند. 23
Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
عده‌ای دیگر نقره و مفرغ به خداوند تقدیم کردند. بعضی هم چوب اقاقیا برای ساختن خیمه با خود آوردند. 24
Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
زنانی که در کار ریسندگی و بافندگی مهارت داشتند، نخهای آبی و ارغوانی و قرمز و کتان ریزبافت با خود آوردند. 25
Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
همۀ زنانی که مایل بودند مهارتشان را به کار برند، از پشم بز، نخ ریسیدند. 26
Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
بزرگان قوم، سنگ جزع و سنگهای قیمتی دیگر برای تزیین ایفود و سینه‌پوش کاهن آوردند، 27
Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
و نیز عطریات و روغن برای روشنایی و روغن مسح و بخور معطر. 28
Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
بدین ترتیب تمام مردان و زنان بنی‌اسرائیل که مشتاق بودند در کاری که خداوند به موسی امر فرموده بود کمک کنند، با خرسندی خاطر هدایای خود را به خداوند تقدیم کردند. 29
Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
سپس موسی به بنی‌اسرائیل گفت: «خداوند، بِصَلئیل (پسر اوری) را که نوهٔ حور و از قبیلهٔ یهودا است برگزیده 30
Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
و او را از روح خود پر ساخته است و حکمت و توانایی و مهارت بخشیده، تا خیمهٔ عبادت و تمام وسایل آن را بسازد. 31
naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
او در ساختن ظروف طلا و نقره و مفرغ، 32
ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
همچنین در کار حکاکی و نجاری و جواهر سازی و هر صنعتی استاد است. 33
kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
خدا به او و اهولیاب (پسر اخیسامک از قبیلهٔ دان) استعداد تعلیم دادن هنر به دیگران را عطا فرموده است. 34
Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
خداوند به آنها در کار طراحی، نساجی و طرازی پارچه‌های آبی، ارغوانی، قرمز و کتان ریزبافت مهارت خاصی بخشیده است. ایشان صنعتگران ماهری هستند. 35
Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.

< خروج 35 >