< خروج 28 >
«برادر خود هارون و پسرانش ناداب، ابیهو، العازار و ایتامار را از سایر مردم اسرائیل جدا کرده، به مقام کاهنی تعیین کن تا مرا خدمت کنند. | 1 |
“Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
لباسهای مخصوصی برای هارون تهیه کن تا معلوم باشد که او برای خدمت من جدا شده است. لباسهای او زیبا و برازندهٔ کار مقدّس او باشد. | 2 |
Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
به کسانی که استعداد و مهارت دوزندگی دادهام دستور بده لباسهای هارون را تهیه کنند لباسهایی که با لباسهای سایر مردم فرق داشته باشد و معلوم شود که او در مقام کاهنی به من خدمت میکند. | 3 |
Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
لباسهایی که باید دوخته شوند اینها هستند: سینهپوش، ایفود، ردا، پیراهن نقشدار، دستار و شال کمر. برای برادرت هارون و پسرانش هم باید از همین لباسها دوخت تا بتوانند در مقام کاهنی به من خدمت کنند. | 4 |
Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
پس طلا و نخهای آبی، ارغوانی و قرمز، و نیز کتان ریزبافت به آنها بده. | 5 |
Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
«صنعتگران باید ایفود را از کتان ریزبافت تابیده تهیه کرده، آن را ماهرانه با طلا، نخهای آبی، ارغوانی و قرمز گلدوزی کنند. | 6 |
“Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
«این جلیقهٔ بلند از دو قسمت، جلو و پشت، که روی شانهها با دو بند به هم میپیوندند، تشکیل شود. | 7 |
Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
بند کمر ایفود هم باید متصل به آن و از جنس خودش باشد، یعنی از رشتههای طلا و کتان تابیده ریزبافت و نخهای آبی، ارغوانی و قرمز. | 8 |
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
«دو سنگ جزع تهیه کن و نامهای دوازده قبیلهٔ بنیاسرائیل را روی آنها حک کن. | 9 |
“Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
یعنی روی هر سنگ شش نام به ترتیب سن آنها. | 10 |
kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
مثل یک خاتمکار و حکاک ماهر نامها را روی سنگها حک کن و آنها را در قابهای طلا بگذار. | 11 |
Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
سپس آنها را روی شانههای ایفود نصب کن تا بدین ترتیب هارون نامهای قبایل بنیاسرائیل را به حضور من بیاورد و من به یاد آنها باشم. | 12 |
na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
همچنین قابهای طلایی بساز | 13 |
Tengeneza vijalizo vya dhahabu
و دو زنجیر تابیده از طلای خالص درست کن و آنها را به قابهای طلایی که روی شانههای ایفود است وصل کن. | 14 |
na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
«برای کاهن یک سینهپوش جهت پی بردن به خواست خداوند درست کن. آن را مانند ایفود از کتان ریزبافت تابیده، نخهای آبی، ارغوانی و قرمز و رشتههای طلا بساز و روی آن را با دقت گلدوزی کن. | 15 |
“Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
این سینهپوش باید دولا و مثل یک کیسه چهارگوش به ضلع یک وجب باشد. | 16 |
Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
چهار ردیف سنگ قیمتی روی آن نصب کن. ردیف اول عقیق سرخ، یاقوت زرد و یاقوت آتشی باشد. | 17 |
Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
ردیف دوم زمرد، یاقوت کبود و الماس. | 18 |
katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
ردیف سوم فیروزه، عقیق یمانی و یاقوت بنفش. | 19 |
safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
ردیف چهارم زبرجد، جزع و یشم. همهٔ آنها باید قابهای طلا داشته باشند. | 20 |
na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
هر یک از این سنگها علامت یکی از دوازده قبیلهٔ بنیاسرائیل خواهد بود و نام آن قبیله روی آن سنگ حک خواهد شد. | 21 |
Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
«برای وصل کردن سینهپوش به ایفود، زنجیرهایی تابیده از طلای خالص درست کن. | 22 |
“Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
سپس دو حلقۀ طلایی بساز و آنها را بر دو گوشۀ سینهپوش بگذار. | 23 |
Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
دو زنجیر را در حلقههای دو گوشۀ سینهپوش بگذار، | 24 |
Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
و دو سر دیگر زنجیرها را از جلو به قابهای طلای روی شانهها وصل کن. | 25 |
nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
دو حلقهٔ طلای دیگر نیز درست کن و آنها را به دو گوشهٔ پایینی سینهپوش، روی لایهٔ زیرین، ببند. | 26 |
Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
دو حلقهٔ طلای دیگر هم درست کن و آنها را در قسمت جلوی ایفود و کمی بالاتر از بند کمر نصب کن. | 27 |
Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
بعد حلقههای سینهپوش را با نوار آبی رنگ به حلقههای ایفود که بالاتر از بند کمر قرار دارد ببند تا سینهپوش از ایفود جدا نشود. | 28 |
Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
«به این ترتیب وقتی هارون به قدس وارد میشود، نامهای تمام قبایل بنیاسرائیل را که روی سینهپوش کنده شده، با خود حمل خواهد کرد تا به این وسیله قوم همیشه در نظر خداوند باشند. | 29 |
“Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
اوریم و تُمّیم را داخل سینهپوش بگذار تا وقتی هارون به حضور من میآید آنها همیشه روی قلب او باشند و او بتواند خواست مرا در مورد قوم اسرائیل دریابد. | 30 |
Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
«ردایی که زیر ایفود است باید از پارچهٔ آبی باشد. | 31 |
“Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
شکافی برای سر، در آن باشد. حاشیهٔ این شکاف باید با دست بافته شود تا پاره نگردد. | 32 |
na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
با نخهای آبی، ارغوانی و قرمز، منگولههایی به شکل انار درست کن و دور تا دور لبهٔ دامن ردا بیاویز و زنگولههایی از طلا بین آنها قرار بده. | 33 |
Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
زنگولههای طلا و انارها باید یکی در میان، دور تا دور لبۀ دامن ردا باشند. | 34 |
Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
هارون در موقع خدمت خداوند باید ردا را بپوشد تا وقتی که به حضور من به قدس وارد میشود یا از آن بیرون میرود، صدای زنگولهها شنیده شود، مبادا بمیرد. | 35 |
Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
«یک نیم تاج از طلای خالص بساز و این کلمات را مانند مُهر، روی آن حک کن:”مقدّس برای خداوند“. | 36 |
“Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
این نیم تاج را با یک نوار آبی رنگ به دستارِ هارون ببند بهطوری که در جلوی دستار قرار گیرد. | 37 |
Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
این نیم تاج باید بر پیشانی هارون باشد تا او بار هر خطایی را که ممکن است بنیاسرائیل در حین تقدیم قربانیهای مقدّس انجام دهند، بر خود حمل کند. هارون باید همیشه این نیم تاج را روی پیشانی خود داشته باشد تا آن قربانیها مقبول خداوند واقع شوند. | 38 |
Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
«پیراهن هارون را از کتان ریزبافت بباف؛ همچنین دستار را. شال کمر گلدوزی شده نیز برای او درست کن. | 39 |
“Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
«برای پسران هارون نیز پیراهن، شال کمر و کلاه تهیه کن. این لباسها باید زیبا و برازنده کار مقدّس ایشان باشند. | 40 |
Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
این لباسها را به هارون و پسرانش بپوشان. با روغن زیتون آنها را مسح کن و ایشان را برای خدمت کاهنی تعیین و تقدیس نما. | 41 |
Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
برای پوشاندن برهنگی لگن تا ران ایشان، لباس زیر از جنس کتان بدوز که اندازهٔ آن از کمر تا بالای زانو باشد. | 42 |
“Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
هارون و پسرانش، وقتی به خیمۀ ملاقات داخل میشوند، یا نزدیک مذبح میآیند تا در قدس خدمت کنند، باید این لباسها را بپوشند، مبادا متحمل گناه شده، بمیرند. این آیین برای هارون و نسل او یک قانون جاودانی خواهد بود. | 43 |
Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.