< استر 6 >
آن شب پادشاه خوابش نبرد، پس فرمود کتاب «تاریخ پادشاهان» را بیاورند و وقایع سلطنت او را برایش بخوانند. | 1 |
Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
در آن کتاب، گزارشی را به این مضمون یافت که بغتان و تارش که دو نفر از خواجهسرایان پادشاه بودند و جلوی در کاخ سلطنتی نگهبانی میدادند، قصد کشتن پادشاه را داشتند؛ ولی مردخای از سوء قصد آنها آگاه شد و به پادشاه خبر داد. | 2 |
Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
پادشاه پرسید: «در ازای این خدمت چه پاداشی به مردخای داده شد؟» خدمتگزاران پادشاه گفتند: «پاداشی به او داده نشد.» | 3 |
Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
پادشاه گفت: «آیا کسی از درباریان در کاخ هست؟» برحسب اتفاق هامان تازه وارد کاخ شده بود تا از پادشاه اجازه بگیرد که مردخای را دار بزند. | 4 |
Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
پس خدمتگزاران جواب دادند: «بله، هامان اینجاست.» پادشاه دستور داد: «بگویید بیاید.» | 5 |
Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
وقتی هامان آمد، پادشاه به او گفت: «شخصی هست که مایلم به او عزت ببخشم. به نظر تو برای او چه باید کرد؟» هامان با خود فکر کرد: «غیر از من چه کسی مورد عزت و احترام پادشاه است.» | 6 |
Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
پس جواب داد: «برای چنین شخصی باید ردای پادشاه و اسب سلطنتی او را که با زیورآلات تزیین شده است بیاورند. | 7 |
Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
آنگاه یکی از امیران عالی رتبهٔ پادشاه آن ردا را به او بپوشاند و او را بر اسب پادشاه سوار کند و در شهر بگرداند و جار بزند: به شخص مورد عزت پادشاه اینچنین پاداش داده میشود.» | 9 |
Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
پادشاه به هامان فرمود: «ردا و اسب را هر چه زودتر آماده کن و هر چه گفتی با تمام جزئیاتش برای مردخای یهودی که در دربار خدمت میکند انجام بده.» | 10 |
Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
پس هامان ردای پادشاه را به مردخای پوشانید و او را بر اسب مخصوص پادشاه سوار کرد و در شهر گرداند و جار زد: «به شخص مورد عزت پادشاه اینچنین پاداش داده میشود.» | 11 |
Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
سپس مردخای به دربار بازگشت، ولی هامان با سرافکندگی زیاد به خانهاش شتافت | 12 |
Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
و موضوع را برای زن خود و همهٔ دوستانش تعریف کرد. زنش و دوستان خردمند او گفتند: «مردخای یک یهودی است و تو نمیتوانی در مقابلش بایستی. اگر وضع به این منوال ادامه یابد شکست تو حتمی است.» | 13 |
naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
در این گفتگو بودند که خواجهسرایان دربار به دنبال هامان آمدند تا او را فوری به ضیافت استر ببرند. | 14 |
Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.