< استر 4 >
وقتی مردخای از این توطئه باخبر شد، از شدت غم، لباس خود را پاره کرد و پلاس پوشیده خاکستر بر سر خود ریخت و با صدای بلند گریهٔ تلخی سر داده از میان شهر گذشت | 1 |
Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
تا به دروازهٔ کاخ سلطنتی رسید. اما نتوانست داخل شود، زیرا هیچکس اجازه نداشت با پلاس وارد کاخ بشود. | 2 |
Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
وقتی فرمان پادشاه به استانها رسید، یهودیان عزا گرفتند. آنها گریه و زاری کردند و لب به غذا نزدند و اکثر ایشان پلاس در برکرده، روی خاکستر دراز کشیدند. | 3 |
Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
وقتی ندیمههای استر و خواجهسرایان دربار از وضع مردخای خبر آوردند، استر بسیار محزون شد و برای مردخای لباس فرستاد تا به جای پلاس بپوشد، ولی مردخای قبول نکرد. | 4 |
Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
آنگاه استر، هتاک را که یکی از خواجهسرایان دربار بود و برای خدمتگزاری استر تعیین شده بود احضار کرد و او را فرستاد تا برود و از مردخای بپرسد که چه اتفاقی افتاده است و چرا پلاس پوشیده است. | 5 |
Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
هتاک به میدان شهر که روبروی دروازهٔ کاخ سلطنتی بود نزد مردخای رفت. | 6 |
Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
مردخای همه چیز را برای او تعریف کرد و از مبلغی که هامان در ازای کشتار یهودیان وعده داده بود به خزانهٔ سلطنتی بپردازد، خبر داد. | 7 |
Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
مردخای یک نسخه از فرمان پادشاه مبنی بر کشتار یهودیان را که در شوش صادر شده بود به هتاک داد تا به استر نشان دهد و از او بخواهد نزد پادشاه برود و برای قوم خود شفاعت کند. | 8 |
Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
هتاک برگشت و پیغام مردخای را به استر رسانید. | 9 |
Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
استر به هتاک دستور داد پیش مردخای برگردد و به او چنین بگوید: | 10 |
Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
«تمام مردم این مملکت میدانند که هر کس چه زن و چه مرد اگر بدون احضار از جانب پادشاه، وارد تالار مخصوص او بشود، طبق قانون کشته خواهد شد، مگر اینکه پادشاه عصای سلطنتی خود را به طرف او دراز کند. حال بیش از یک ماه است که پادشاه مرا احضار نکرده است تا شرفیاب شوم.» | 11 |
“Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
وقتی هتاک پیغام استر را به مردخای رساند، | 12 |
Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
مردخای در جواب گفت که به استر چنین بگوید: «خیال نکن وقتی تمام یهودیان کشته شوند، تو در کاخ سلطنتی جان به در خواهی برد! | 13 |
Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
اگر در این موقعیت، تو ساکت بمانی رهایی برای یهود از جایی دیگر پدید خواهد آمد، اما تو و خاندانت کشته خواهید شد. از این گذشته کسی چه میداند، شاید برای همین زمان ملکه شدهای.» | 14 |
Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
پس استر این پیغام را برای مردخای فرستاد: | 15 |
Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
«برو و تمام یهودیان شوش را جمع کن تا برای من سه شبانه روز روزه بگیرند. من و ندیمههایم نیز همین کار را میکنیم. سپس، من به حضور پادشاه خواهم رفت، هر چند این برخلاف قانون است. اگر کشته شدم، بگذار کشته شوم!» | 16 |
“Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
پس مردخای رفت و هر چه استر گفته بود انجام داد. | 17 |
Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.