< جامعه 10 >

همچنانکه مگسهای مرده می‌توانند یک شیشه عطر را متعفن کنند، همچنین یک حماقت کوچک می‌تواند حکمت و عزت شخص را بی‌ارزش نماید. 1
Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
دل شخص خردمند او را به انجام کارهای درست وا می‌دارد، اما دل شخص نادان او را به طرف بدی و گناه می‌کشاند. 2
Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
آدم نادان را می‌توان حتی از راه رفتنش شناخت. 3
Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
وقتی رئیس تو از دست تو خشمگین می‌شود از کار خود دست نکش. اگر در مقابل خشم او آرام بمانی از بروز اشتباهات بیشتر جلوگیری خواهی کرد. 4
Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
بدی دیگری نیز در زیر این آسمان دیده‌ام که در اثر اشتباهات برخی پادشاهان به وجود می‌آید: 5
Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
به اشخاص نادان مقام و منصب‌های عالی داده می‌شود؛ برای ثروتمندان اهمیتی قائل نمی‌شوند؛ 6
Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
غلامان سوار بر اسبند، ولی بزرگان مانند بردگان، پیاده راه می‌روند. 7
Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
آن که چاه می‌کَنَد ممکن است در آن بیفتد؛ کسی که دیوار را سوراخ می‌کند ممکن است مار او را بگزد. 8
Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
آن که در معدن سنگ کار می‌کند ممکن است از سنگها صدمه ببیند؛ کسی که درخت می‌برد ممکن است از این کار آسیبی به او برسد. 9
Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
تبر کُند، احتیاج به نیروی بیشتری دارد، پس کسی که تیغهٔ آن را از قبل تیز می‌کند، عاقل است. 10
Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
پس از اینکه مار کسی را گزید، آوردن افسونگر بی‌فایده است. 11
Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
سخنان شخص دانا دلنشین است، ولی حرفهای آدم نادان باعث تباهی خودش می‌گردد؛ 12
Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
ابتدای حرفهای او حماقت است و انتهای آن دیوانگی محض؛ 13
Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
او زیاد حرف می‌زند. ولی کیست که از آینده خبر داشته باشد و بداند که چه پیش خواهد آمد؟ 14
naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
آدم نادان حتی از انجام دادن کوچکترین کار خسته می‌شود، زیرا شعور انجام دادن آن را ندارد. 15
Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
وای بر سرزمینی که پادشاهش غلامی بیش نیست و رهبرانش صبحگاهان می‌خورند و مست می‌کنند! 16
Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
خوشا به حال مملکتی که پادشاه آن نجیب‌زاده است و رهبرانش به موقع و به اندازه می‌خورند و می‌نوشند و مست نمی‌کنند. 17
Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
در اثر تنبلی سقف خانه چکه می‌کند و فرو می‌ریزد. 18
Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
جشن، شادی می‌آورد و شراب باعث خوشی می‌گردد، اما بدون پول نمی‌شود اینها را فراهم کرد. 19
Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
حتی در فکر خود پادشاه را نفرین نکن و حتی در اتاق خوابت شخص ثروتمند را لعنت نکن، چون ممکن است پرنده‌ای حرفهایت را به گوش آنان برساند! 20
Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.

< جامعه 10 >