< تثنیه 29 >

این است شرایط عهدی که خداوند در سرزمین موآب توسط موسی با قوم اسرائیل بست. این عهد غیر از عهدی بود که قبلاً در کوه حوریب بسته شده بود. ‏ 1
Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
موسی تمام بنی‌اسرائیل را احضار کرد و به ایشان گفت: شما با چشمان خود بلاهایی را که خداوند بر سر فرعون و درباریانش آورد، دیدید 2
Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
و شاهد معجزات عظیم خداوند در سراسر مصر بودید. 3
mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
ولی تا امروز خداوند دلهایی که بفهمند و چشمانی که ببینند و گوشهایی که بشنوند به شما نداده است. 4
Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
من چهل سال شما را در بیابان هدایت کردم. در این مدت نه لباسهایتان کهنه شد و نه کفشهایتان پاره گشت. 5
Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
هر چند نانی برای خوردن و شرابی برای نوشیدن نداشتید، اما خداوند روزی شما را می‌رساند تا به شما بفهماند که او یهوه خدای شماست. 6
Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
زمانی که به اینجا رسیدیم سیحون (پادشاه سرزمین حشبون) و عوج (پادشاه سرزمین باشان) با ما به جنگ برخاستند، ولی ما ایشان را شکست دادیم 7
Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
و سرزمینشان را گرفتیم و به قبیله‌های رئوبین، جاد و نصف قبیلهٔ منسی دادیم. 8
Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
شرایط این عهد را اطاعت کنید تا در تمام کارهایتان موفق باشید. 9
Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
همگی شما یعنی رهبران، مشایخ، مردان قوم همراه با کودکان و همسرانتان و غریبانی که در بین شما زندگی می‌کنند یعنی کسانی که هیزم می‌شکنند و برایتان آب می‌آورند امروز در حضور خداوند، خدایتان ایستاده‌اید. 10
Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
11
watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
اینجا ایستاده‌اید تا به عهدی که یهوه خدایتان امروز با شما می‌بندد وارد شوید. 12
Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
امروز خداوند می‌خواهد شما را به عنوان قوم خود تأیید کند و خدای شما باشد، همان‌طور که به شما وعده داد و برای پدرانتان، ابراهیم و اسحاق و یعقوب سوگند خورد. 13
ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
این پیمان تنها با شما که امروز در حضور یهوه خدایمان ایستاده‌اید بسته نمی‌شود بلکه با تمام نسلهای آیندهٔ اسرائیل نیز بسته می‌شود. 14
Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
15
pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
شما به یاد دارید که چگونه در سرزمین مصر زندگی می‌کردیم و پس از خروج از آنجا چطور از میان قومهای دیگر گذشتیم. 16
Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
شما رسوم و بتهای قبیح آن سرزمینها را دیدید که از چوب و سنگ و نقره و طلا ساخته شده بودند. 17
Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
امروز در میان شما مرد یا زن، خاندان یا قبیله‌ای نباشد که از خداوند، خدایمان برگردد و بخواهد این خدایان را بپرستد و با این کار، به تدریج قوم را مسموم کند. 18
Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
کسی در میان شما نباشد که پس از شنیدن این هشدارها، آنها را سرسری بگیرد و فکر کند اگر به راههای گستاخانهٔ خود ادامه دهد صدمه‌ای نخواهد دید. این کار او همگی شما را نابود خواهد کرد؛ 19
Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
چون خداوند از سر تقصیرات او نمی‌گذرد بلکه خشم و غیرتش بر ضد آن شخص شعله‌ور خواهد شد و تمام لعنتهایی که در این کتاب نوشته شده بر سر او فرود خواهد آمد و خداوند اسم او را از روی زمین محو خواهد کرد. 20
Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
خداوند او را از تمامی قبیله‌های اسرائیل جدا خواهد نمود و کلیهٔ لعنتهایی را که در این کتاب ذکر شده، بر سر او نازل خواهد کرد. 21
Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
آنگاه فرزندان شما و نسلهای آینده و غریبانی که از کشورهای دور دست از سرزمین شما عبور کنند، بلاها و بیماریهایی را که خداوند بر این سرزمین نازل کرده است خواهند دید. 22
Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
آنها خواهند دید که تمام زمین، شوره‌زاری است خشک و سوزان که در آن نه چیزی کاشته می‌شود و نه چیزی می‌روید. سرزمینتان درست مثل سدوم و عموره و ادمه و صبوئیم خواهد بود که خداوند در خشم خود آنها را ویران کرد. 23
na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
قومها خواهند پرسید: «چرا خداوند با این سرزمین چنین کرده است؟ دلیل این خشم بی‌امان او چه بوده است؟» 24
watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
در جواب ایشان گفته خواهد شد: «چون مردم این سرزمین عهدی را که هنگام خروج از مصر خداوند، خدای پدرانشان با ایشان بسته بود، شکستند. 25
Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
ایشان به پرستش خدایانی پرداختند که آنها را قبلاً نمی‌شناختند و خداوند، پرستش آنها را منع کرده بود. 26
na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
پس خشم خداوند علیه این سرزمین افروخته شد و کلیهٔ لعنتهای او که در این کتاب نوشته شده، بر سرشان فرو ریخت. 27
Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
خداوند با خشم و غضب شدید خود، ایشان را از سرزمینشان ریشه‌کن ساخت و آنها را به سرزمین دیگری راند که تا امروز در آنجا زندگی می‌کنند.» 28
Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
اسراری هست که یهوه خدایمان بر کسی کشف نفرموده است، اما او قوانین خود را بر ما و فرزندانمان آشکار نموده است تا آنها را اطاعت کنیم. 29
Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.

< تثنیه 29 >