< دوم سموئیل 22 >
وقتی که خداوند داوود را از دست شائول و دشمنان دیگرش رهانید، او این سرود را برای خداوند سرایید: | 1 |
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
خداوند قلعهٔ من است. او صخرهٔ من است و مرا نجات میبخشد. | 2 |
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
خدایم صخرهٔ محکمی است که به آن پناه میبرم. او همچون سپر از من محافظت میکند، به من پناه میدهد و با قدرتش مرا میرهاند. نجاتدهندۀ من، مرا از ظلم میرهاند. | 3 |
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
او را به کمک خواهم طلبید و از چنگ دشمنان رهایی خواهم یافت. ای خداوند تو شایستهٔ پرستش هستی! | 4 |
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
مرگ، مرا در چنگال خود گرفتار کرده بود و موجهای ویرانگرش مرا در بر گرفته بود. | 5 |
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
مرگ برای من دام نهاده بود تا مرا به کام خود بکشد. (Sheol ) | 6 |
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
اما من در این پریشانی به سوی خداوند فریاد برآوردم و از خدایم کمک خواستم. فریاد من به گوش او رسید و او از خانهٔ مقدّسش نالهٔ مرا شنید. | 7 |
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
آنگاه زمین تکان خورد و لرزید و بنیاد آسمان مرتعش شد و به لرزه درآمد، زیرا خداوند به خشم آمده بود. | 8 |
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
دود از بینی او برآمد و شعلههای سوزانندهٔ آتش از دهانش زبانه کشید. | 9 |
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
او آسمان را شکافت و نزول کرد، زیر پایش ابرهای سیاه قرار داشت. | 10 |
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
بر ارابهٔ آسمانی خویش سوار شد و با سرعت باد پرواز نمود. | 11 |
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
او خود را با تاریکی پوشاند و ابرهای غلیظ و پر آب او را احاطه کردند. | 12 |
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
درخشندگی حضور او، شعلههای آتش پدید آورد. | 13 |
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
آنگاه خداوند، خدای متعال، با صدای رعدآسا از آسمان سخن گفت. | 14 |
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
او با تیرهای آتشین خود، دشمنانم را پراکنده و پریشان ساخت. | 15 |
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
آنگاه به فرمان او آب دریا به عقب رفت و با دمیدن نفس خداوند خشکی پدید آمد. | 16 |
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
خداوند از آسمان دست خود را دراز کرد و مرا از اعماق آبهای بسیار بیرون کشید. | 17 |
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
مرا از چنگ دشمنان نیرومندی که از من تواناتر بودند، رهانید | 18 |
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
وقتی در سختی و پریشانی بودم، دشمنان بر من هجوم آوردند، اما خداوند مرا حفظ کرد. | 19 |
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
او مرا به جای امنی برد، او مرا نجات داد، زیرا مرا دوست میداشت. | 20 |
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
خداوند پاداش درستکاری و پاکی مرا داده است، | 21 |
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
زیرا از دستورهای خداوند اطاعت نمودهام و به خدای خود گناه نورزیدهام. | 22 |
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
همهٔ احکامش را بجا آوردهام و از فرمان او سرپیچی نکردهام. | 23 |
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
در نظر خداوند بیعیب بودهام، خود را از گناه دور نگاه داشتهام. | 24 |
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
خداوند به من پاداش داده است، زیرا در نظر او پاک و درستکار بودهام. | 25 |
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
خدایا، تو نسبت به کسانی که به تو وفادارند، امین هستی و کسانی را که کاملند محبت میکنی. | 26 |
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
به اشخاص پاک، خود را پاک نشان میدهی، ولی با اشخاص حیلهگر، به زیرکی رفتار میکنی. | 27 |
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
تو افتادگان را نجات میدهی، اما متکبران را سرنگون میکنی. | 28 |
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
ای خداوند، تو نور من هستی، تو تاریکی مرا به روشنایی تبدیل میکنی. | 29 |
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
با کمک تو به سپاهیان دشمن حمله خواهم برد و قلعههای آنها را در هم خواهم کوبید. | 30 |
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
اعمال خداوند کامل و بینقص است و وعدههای او پاک و قابل اعتماد! خداوند از کسانی که به او پناه میبرند مانند سپر محافظت میکند. | 31 |
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
کیست خدا غیر از یهوه و کیست صخرهٔ مستحکم غیر از خدای ما؟ | 32 |
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
خدا به من قوت میبخشد و در راههایی که میروم مرا حفظ میکند. | 33 |
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
پاهایم را چون پاهای آهو میگرداند تا بتوانم بر بلندیها بایستم. | 34 |
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
او دستهای مرا برای جنگ تقویت میکند تا بتوانم کمان مفرغین را خم کنم. | 35 |
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
خداوندا، تو با سپرت مرا نجات دادهای، و از لطف توست که به این عظمت رسیدهام. | 36 |
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
زمین زیر پایم را وسیع ساختهای تا نلغزم. | 37 |
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
دشمنانم را تعقیب میکنم و آنها را شکست میدهم و تا آنها را از بین نبرم، باز نمیگردم. | 38 |
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
آنها را چنان بر زمین میکوبم که زیر پاهایم بیفتند و برنخیزند. | 39 |
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
تو برای جنگیدن مرا قوت بخشیدهای و دشمنانم را زیر پاهای من انداختهای. | 40 |
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
تو آنها را وادار به عقبنشینی و فرار مینمایی و من آنها را نابود میکنم. | 41 |
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
فریاد برمیآورند، ولی کسی نیست که آنها را برهاند. از خداوند کمک میخواهند، اما او نیز به داد ایشان نمیرسد. | 42 |
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
من آنها را خرد کرده، به صورت غبار درمیآورم، و آنها را مانند گل کوچهها لگدمال میکنم. | 43 |
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
تو مرا از شورش قومم نجات دادهای و مرا رهبر قومها ساختهای. مردمی که قبلاً آنها را نمیشناختم اکنون مرا خدمت میکنند. | 44 |
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
بیگانهها در حضور من سر تعظیم فرود میآورند و به محض شنیدن دستورهایم، آنها را اجرا میکنند. | 45 |
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
آنها روحیهٔ خود را باختهاند و با ترس و لرز از قلعههای خود بیرون میآیند. | 46 |
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
خداوند زنده است! شکر و سپاس بر خدای متعال باد که صخرهٔ نجات من است! | 47 |
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
خدایی که انتقام مرا میگیرد، قومها را مغلوب من میگرداند، | 48 |
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
و مرا از چنگ دشمنان میرهاند. خداوندا، تو مرا بر دشمنانم پیروز گردانیدی و از دست ظالمان رهایی دادی. | 49 |
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
ای خداوند، تو را در میان قومها خواهم ستود و در وصف تو خواهم سرایید. | 50 |
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
خدا پیروزیهای بزرگی نصیب پادشاه برگزیدهٔ خود، داوود، میسازد، و بر او و نسلش همیشه رحمت میفرماید. | 51 |
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”